Wanaokiri kuleta maafa kiuchawi waburuzwe mahakamani

East African Eagle

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
3,759
2,205
Kuna watu wamekuwa wakikiri waziwazi kuwa wamehusika na mauaji ya watu nchini kama vile wasanii maarufu,watu maarafu na kuleta majanga kama ya kuzamisha meli zilizoua watu kibao na maajali mengine kwa uchawi.

Kwa kuwa wanakuwa wao wenyewe wanatamka hakuna sababu ya kutafuta mashahidi polisi wawakamate wawaburuzwe mahakamani kwa kesi ya mauaji.Na majaji wasihangaike kuuliza walitumia mbinu gani kuua wala kuwahoji waendesha mashtaka wao wawahoji hao waliotamka je ulihusika kwenye hayo mauaji? Wakisema ndio jaji aingie kusoma hukumu moja kwa moja.Kwa kuwa mhusika kakiri kosa mwenyewe hivyo kumhukumu kwa kukiri kwake mwenyewe.
 
Back
Top Bottom