Vodacom Tanzania mnakera sana na hizi sms za bahati nasibu, unaamka asubuhi tu unapanga ratiba zako za kwenda kutafuta mkate wa kila siku mara ujumbe unaingia kwenye simu, unakimbilia simu ukidhani ni mchongo wa kazi au interview unakutana na sms ya mojaspesho 😡. Mchana hujakaa sawa instamoja wametuma, ukigeuka huku boompesa nao wanakutumia. Hii imekua kero na TCRA wako kimya kama vile hawaskii malalamiko haya.
Mimi nimeamua kila wakinitumia sms hizi napost katika uzi huu kama ishara ya kupaza sauti yangu juu ya kero hii toka mitandao ya simu. Kama na wewe unakerwa ungana nami kupaza sauti yako
Mimi nimeamua kila wakinitumia sms hizi napost katika uzi huu kama ishara ya kupaza sauti yangu juu ya kero hii toka mitandao ya simu. Kama na wewe unakerwa ungana nami kupaza sauti yako