Wanaojitolea mashuleni waache mara moja la sivyo serikali haitaona umuhimu wa kuajiri.

fullcup

JF-Expert Member
Jun 21, 2016
806
2,182
Serikali kwa miaka mitano mfurulizo haikuajiri na wala haioni umuhimu huo kutokana na matokeo bora mashuleni. Kuna shule zina walimu watatu wakuajiriwa na saba wakujitolea na zinafanya vema matokeo ya mitihani yataifa.

Kutokana na ufaulu huo serikali haioni umuhimu wakuajiri wakati wanafikia malengo na mwaka huu karibia shule zote zimefanya vema.

Wito wangu ni hawa ndugu wanaojitolea waache mara moja ili tatizo halisi lionekane machoni pa wananchi na serikali.

Wakati shule ya watoto zaidi ya mia tano wakihudumiwa na walimu wawili itwaamusha wananchi na serikali na huenda nguvu ikaelekezwa huko. Nje ya hapo tuangalie mengine yakufanya.

Halafu mbinu yao yakusema wanaojitolea ndo watapewa kipaumbele kisiwapofushe na kujikuta mnafanya kazi miaka na miaka bila ajira huku kitaa mnafahamika kama walimu na mnaishia kula mihogo yakuchoma.


Ili kufikia malengo yetu yakuishi kwakunufaika na elimu zetu ni lazima tufanye kazi na kulipwa kulingana na taaluma.

Bora wakaajiriwa hata wachache lakini wanaolipwa kulingana na taaluma. Leo hata shule na sekta binafsi wanaajiri kwamishahara midogo kisa vijitamaa, tuache ili hata waajiri wapne thamani yetu.
 
Kuna wauguzi,wafamasia,wataalamu wa maabara na madaktari wanajitolea halafu wanalalamika ajira.......mara nyingi watu hawajiongezi kama mambo yanaenda shwari
 
Serikali kwa miaka mitano mfurulizo haikuajiri na wala haioni umuhimu huo kutokana na matokeo bora mashuleni. Kuna shule zina walimu watatu wakuajiriwa na saba wakujitolea na zinafanya vema matokeo ya mitihani yataifa.

Kutokana na ufaulu huo serikali haioni umuhimu wakuajiri wakati wanafikia malengo na mwaka huu karibia shule zote zimefanya vema.

Wito wangu ni hawa ndugu wanaojitolea waache mara moja ili tatizo halisi lionekane machoni pa wananchi na serikali.

Wakati shule ya watoto zaidi ya mia tano wakihudumiwa na walimu wawili itwaamusha wananchi na serikali na huenda nguvu ikaelekezwa huko. Nje ya hapo tuangalie mengine yakufanya.

Halafu mbinu yao yakusema wanaojitolea ndo watapewa kipaumbele kisiwapofushe na kujikuta mnafanya kazi miaka na miaka bila ajira huku kitaa mnafahamika kama walimu na mnaishia kula mihogo yakuchoma.
Kama mwalimu anajitolea kwa mwezi anatengeneza kiasi cha pesa Si chini ya shillingi laki mbili ambayo inamfanya alipe kodi apate hela ya kula na matumizi mengine madogo madogo

Je ikotokea ameacha kujitolea hiyo pesa utamsaidia
 
Kama mwalimu anajitolea kwa mwezi anatengeneza kiasi cha pesa Si chini ya shillingi laki mbili ambayo inamfanya alipe kodi apate hela ya kula na matumizi mengine madogo madogo

Je ikotokea ameacha kujitolea hiyo pesa utamsaidia
Bora hata huyo anaunafuu kuna watu huku kitaa toka mwaka juzi wanajitolea hawalipwi kabisaaa ila wamejazana kisa afisa elimu aliwaambia watapewa kipaumbele kwenye ajira mpya.
 
Kuna wauguzi,wafamasia,wataalamu wa maabara na madaktari wanajitolea halafu wanalalamika ajira.......mara nyingi watu hawajiongezi kama mambo yanaenda shwari
Kuna watu wanalipwa kidogo ndo wanapofushwa lakini tukikubali kuumia kidogo tutakua na furaha daima.
 
Hivi mtu kweli unakuwa umekwama kiasi gani hadi inafikia hatua unamua kupoteza muda wako na nguvu kwa njia ya kujitolea wakati hapo hapo yapo mambo muhimu ya kuhudumia watu nawe ukapata chochote kitu.

Shida iko pale ukiwa umesoma ualimu unajiwekea akili 100% huezi shika jambo lolote zaidi ya ualimu.Hivyo hivyo pia kwa secta nyingine.

Mana kama wajitolea hupewi chochote,jee hizo gharama unazotumia kwa nauli au chakula au mavazi au lolote kwanini usi Zitumie kwenye mambo mengine ili kujitoa stage moja kwenda nyingine.

Bora ujitolee ukiwa na imani unatafuta uzoefu ukiwa na uhakika utaenda ajiriwa Sector binafsi mana ndo wanaodai uzoefu. Ila ndo wakuta mtu anajitolea alafu akili zake zote zinawaza serikalini sa hiyo ndo ujinga gani?

Labda tuseme kuna hata hela nsogo wanapewa ila kama ndo bila bila ki kweli huo ni uwenda wazimu (mtanisamehe)
 
Thread ya wachawi na watu wenye roho mbaya!
Kwa taarifa yako mleta mada:
Zikitoka nafasi za ajira Wakurugenzi huwa wanatuma taarifa vituoni/idarani na kuwaambia wakuu wa vituo wawapitishie barua za maombi watu wanaojitolea hapo vituoni! Na ndio maana kuna uzi hapa JF wa malalamiko kuwa nafasi za kazi zinazotangazwa waombaji wanakuta zimejazwa au zingine hazitangazwi kabisa na watu wanaajiriwa!
ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO! by JK.
 
Kila mtu anapambana ili kutatua shida zake, wewe unaweza sema wasijitolee kumbe una kibiashara chako kinakupa pesa za kujikimu, na yeye hivyo hivyo anajitolea ili kupata pesa ya kujikimu.

Hili la wanao jitolea kupewa vipao mbele ni la kupuuzwa, ila mm sio mwalimu maana kazi za wito sizitakagi maishani mwangu.
 
Hivi mtu kweli unakuwa umekwama kiasi gani hadi inafikia hatua unamua kupoteza muda wako na nguvu kwa njia ya kujitolea wakati hapo hapo yapo mambo muhimu ya kuhudumia watu nawe ukapata chochote kitu.

Shida iko pale ukiwa umesoma ualimu unajiwekea akili 100% huezi shika jambo lolote zaidi ya ualimu.Hivyo hivyo pia kwa secta nyingine.

Mana kama wajitolea hupewi chochote,jee hizo gharama unazotumia kwa nauli au chakula au mavazi au lolote kwanini usi Zitumie kwenye mambo mengine ili kujitoa stage moja kwenda nyingine.

Bora ujitolee ukiwa na imani unatafuta uzoefu ukiwa na uhakika utaenda ajiriwa Sector binafsi mana ndo wanaodai uzoefu. Ila ndo wakuta mtu anajitolea alafu akili zake zote zinawaza serikalini sa hiyo ndo ujinga gani?

Labda tuseme kuna hata hela nsogo wanapewa ila kama ndo bila bila ki kweli huo ni uwenda wazimu (mtanisamehe)
Mtu anajitolea anapata kwa wiki 70,000 utamshauri vipi aache kujitolea akae nyumbani? Labda kama anaishi kwa wazazi wake.
 
Thread ya wachawi na watu wenye roho mbaya!
Kwa taarifa yako mleta mada:
Zikitoka nafasi za ajira Wakurugenzi huwa wanatuma taarifa vituoni/idarani na kuwaambia wakuu wa vituo wawapitishie barua za maombi watu wanaojitolea hapo vituoni! Na ndio maana kuna uzi hapa JF wa malalamiko kuwa nafasi za kazi zinazotangazwa waombaji wanakuta zimejazwa au zingine hazitangazwi kabisa na watu wanaajiriwa!
ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO! by JK.
Wewe hujui kinachoendelea kaendele kulima alizeti. Mwaka jana ajira elf 8 zilitoka katani kwetu vijana 16 wanaojitolea hakuna alieambulia zaidi ya mtoto wa afisa misitu, mtoto wa bwana afya na mtoto wa mstaafu ambao hawajawahi kujitolea popote ndo walienda. Tunaposema waache namanisha bora tukaumia mwanzoni lakini mwisho tunufauishe na kuiheshimisha taaluma.
 
Mtu anajitolea anapata kwa wiki 70,000 utamshauri vipi aache kujitolea akae nyumbani? Labda kama anaishi kwa wazazi wake.
Hapo sawa mbona hyo hela ni nusu ya take home ya mwalimu aloajiriwa serikalini... naongela mtu unakuta kwa mwezi anakula laki au elfu 70 au wanapokea maneno tuu kuwa hakuna
 
Mtu anajitolea anapata kwa wiki 70,000 utamshauri vipi aache kujitolea akae nyumbani? Labda kama anaishi kwa wazazi wake.
Lakini akiajiriwa kwa taaluma yake anapata mara mbili au tatu kwanini tusivumilie lakini tufikie malengo.
 
Wewe hujui kinachoendelea kaendele kulima alizeti. Mwaka jana ajira elf 8 zilitoka katani kwetu vijana 16 wanaojitolea hakuna alieambulia zaidi ya mtoto wa afisa misitu, mtoto wa bwana afya na mtoto wa mstaafu ambao hawajawahi kujitolea popote ndo walienda. Tunaposema waache namanisha bora tukaumia mwanzoni lakini mwisho tunufauishe na kuiheshimisha taaluma.
Mkuu nimetoka kwenye ajira sina miaka zaidi ya 4, nimekuwa mtumishi wa umma kwa miaka 16+ Nakutumia salary slip yangu huko PM...tumewatumia hawa watu wa kujitolea sana tu bila kusahau wengi wao wameajiliwa! CV ya mtu aliyejitolea sio sawa na yako unayeshinda JF, mwenzako ana kitu cha kuandika pia anaye mtu wa ku- endorse barua yake ya maombi ya kazi!
Mara ya mwisho nipo kazini...Agha Khan Foundation walianzisha mradi hapo kitoni...watu waliokuwa wanajitolea walikula shavu kwenye huo mradi na sasa hivi ni watumishi!
 
Back
Top Bottom