Wanaoishi kwenye vurugu za ndoa wasiajiriwe?

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,810
15,395
Wanawake ambao wana vurugu za kindoa na hasa kufujwa na waume zao, huwa wanapoteza saa nyingi za kazi kwa kiasi cha asilimia 40 ukilinganisha na wanawake ambao ndoa zao hazina vurugu. Muda huo hupotezwa na kule kutokuja kazini kutokana na vipigo au madhara mengine na pia kutokuwa kazini kiakili kutokana na mateso.

Wanawake ambao wako kwenye uhusiano au ndoa zenye vurugu huwa wanakabiliwa na matatizo ya kushindwa kuwa wazingativu, ufanyaji kazi wa polepole na pia kushindwa kabisa kufanya kazi katika baadhi ya nyakati.

Ingawa matatizo haya yanatazamwa kwa wanawake, lakini pia kuna idadi ya kutosha ya wanaume ambao hushindwa kazi zao kutokana na matatizo ya ndoa na zaidi ni kwa wanaume walioshikwa na wake zao na ambao hawafurukuti mbele ya wake zao.

Kutokana na kushikwa na wake zao, muda wao mwingi huutumia kuwafikiria wake zao au wapenzi. Lakini pia badala ya kufikiria kuzalisha hufikiria kupata zaidi ili kuwaridhisha wake au wapenzi wao .

Kwa hiyo unapotaka kuajiri mtu inabidi pia uchunguze kama hafujwi au hajashikwa na mpenzi au mkewe. Kama ukigundua kwamba, ameshikwa au anafujwa, basi ujue kwamba kuna hasara inakuja upande wako
 
mkuu uko rught
ila ni aina gani za ndoa unajua kuna ndoa nyingi zinafungishwa kanisan za majini lakini kutokana na wchungajiwengi kutokuwa na uwepo wa utambuzi wanaishia kuwavalisha pete majini..so hawa ni ngumu maana ujue shetan anamiliki dunia na wale wabaya wengi ndiowanaoishi maisha ya neema humuduniani ...
 
mkuu uko rught
ila ni aina gani za ndoa unajua kuna ndoa nyingi zinafungishwa kanisan za majini lakini kutokana na wchungajiwengi kutokuwa na uwepo wa utambuzi wanaishia kuwavalisha pete majini..so hawa ni ngumu maana ujue shetan anamiliki dunia na wale wabaya wengi ndiowanaoishi maisha ya neema humuduniani ...

Nimekupata mkuu, lakini, Je wale wanaoishi bila ndoa lakini maisha yao ya kinyumba yakawa na vurugu, inakuweaje?....................
 
Wanawake ambao wana vurugu za kindoa na hasa kufujwa na waume zao, huwa wanapoteza saa nyingi za kazi kwa kiasi cha asilimia 40 ukilinganisha na wanawake ambao ndoa zao hazina vurugu. Muda huo hupotezwa na kule kutokuja kazini kutokana na vipigo au madhara mengine na pia kutokuwa kazini kiakili kutokana na mateso.

Wanawake ambao wako kwenye uhusiano au ndoa zenye vurugu huwa wanakabiliwa na matatizo ya kushindwa kuwa wazingativu, ufanyaji kazi wa polepole na pia kushindwa kabisa kufanya kazi katika baadhi ya nyakati.

Ingawa matatizo haya yanatazamwa kwa wanawake, lakini pia kuna idadi ya kutosha ya wanaume ambao hushindwa kazi zao kutokana na matatizo ya ndoa na zaidi ni kwa wanaume walioshikwa na wake zao na ambao hawafurukuti mbele ya wake zao.

Kutokana na kushikwa na wake zao, muda wao mwingi huutumia kuwafikiria wake zao au wapenzi. Lakini pia badala ya kufikiria kuzalisha hufikiria kupata zaidi ili kuwaridhisha wake au wapenzi wao .

Kwa hiyo unapotaka kuajiri mtu inabidi pia uchunguze kama hafujwi au hajashikwa na mpenzi au mkewe. Kama ukigundua kwamba, ameshikwa au anafujwa, basi ujue kwamba kuna hasara inakuja upande wako

Hapo umenena mkuu, vurugu za ndoa husababisha hata uchumi wa nchi kuyumba.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom