Bashir Yakub
Member
- May 27, 2013
- 84
- 1,561
BRELA INAKIMBIZA WAWEKEZAJI.
Na Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241
Mfumo kama mfumo wa kusajili kampuni ni mzuri na unarespond haraka ila watendaji bado kabisa.
Nitatoa mfano na sina shaka kila mdau ambaye anasajili ama amewahi kusajili kampuni au biashara kupitia mfumo mpya wa Brela atakubaliana nami.
Ni hivi, unakamilisha docmnts na kusubmit online Brela. Unasubiri majib na baada ya muda unajibiwa ufanye marekebisho(Additional Information/correction is required.
Unafanya marekebisho yote uliyoelekezwa na unasubmit upya. Baada ya siku au siku mbili dcmnt zinarejeshwa tena kuwa ufanye tena marekebisho(Additional Information/correction is required.
Kinachouma sana na kukera sana ni kwamba haya marekebisho unayoambiwa ufanye kwa hii mara ya pili ni MAPYA. Kwa maana dcmnt zilivyorejeshwa mara ya kwanza hayakuwa matatizo ila mara ya pili yameonekana ni matatizo.
Unarekebisha mara ya pili na kusubmit tena. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required.
Haya ya mara ya tatu nayo unakuta ni MAPYA. Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili yameonwa mara ya tatu.
Unarekebisha tena na kusubmit. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required.
Haya ya mara ya nne nayo ni marekebisho MAPYA.
Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili, hayakuona uliporudishwa mara ya tatu, sasa yameonwa mara ya nne.
Mchezo unaendelea hivyo mpaka mwezi au zaidi. Halafu unasikia Mtendaji Mkuu wa Brela inaiambia Serikali, Dunia, na Wawekezaji kuwa sasa Tanzania Brela inasajili Kampuni na Biashara ndani ya saa 24. Ni aibu sana.
Hoja sio kwamba marekebisho yasifanywe ama usajili ufanyike bila sifa kutimia, Laa hasha.
Hoja ni kwamba, huyu anayesoma dcmnt na kuzirejesha anashindwaje kupitia dcmnt nzima yote kwa umakini, akaorodhesha yoooote yanayotakiwa kufanyiwa marekebisho, ukairudisha ili yote yafanyike kwa pamoja.
Inakuwaje marekebisho yasionwe dcmnt ziliporudishwa mara ya kwanza yaje kuonwa mara ya pili na ya tatu na kuendelea.
Na bora ingekuwa kwamba kile ulichoambiwa kurekebisha umekirekebisha vibaya kwahiyo unatakiwa ukirekebishe vizuri zaidi, hapana. Hiki ulichoambiwa kurekebisha kinaachwa kwa maana kuwa umekirekebisha vizur unaletewa kipya kabisa ambacho hakikuwa kimeonwa mara ya kwanza, ama ya pili, ama ya tatu. Ni kero, usumbufu, na aibu kwa watendaji.
Msichojua ni kwamba wengi wanaosajili Makampuni na biashara ni Wawekezaji.
Anakuja mwekezaji kutoka nje unamuhakikishia kuwa ndani ya siku moja,mbili,tatu utakuwa umemsajilia Kampuni. Anasubiri siku, wiki, wiki mbili, tatu, mwezi mwezi na zaidi hakuna kitu.
Mimi kama Wakili, ama mtu mwingine aliyepewa kazi ya kusajili siwezi kukubali kuaibika kwa mteja wangu. Nitamwita, nitamuonesha majibu ya Brela kwenye system. Nitamuonesha marekebisho mapya ambayo hayakuwa yameletwa mwanzoni yanavyoletwa kila baada ya siku mbili au wiki.
Ataelewa kosa sio langu ni la BRELA. Ataondoka sababu hawez kusubiri zaidi anaingia gharama kubwa za Malazi. Ataenda kufungua Kampuni Rwanda au Kenya ambako kwa dhati yake kampuni inasajiliwa ndani au chini ya Saa 24. Hivi ndivyo tunavyopoteza wawekezaji kupitia Brela.
Lakini ni kero zaidi sababu kila marekebisho yanahitaji wanahisa ama wakurugenzi wasaini. Utawaita kusaini mara ngapi. Na vipi kama walisaini wakaondoka na kwenda mbali.
Kuna mda unawaza labda pengine aliyepitia kazi mara ya kwanza siye aliyeipitia mara ya pili, na siye aliyepitia mara ya tatu, pengine ndo maana kila mtu ametaka marekebisho yake tofauti.
Kama ndivyo, basi hiki ndicho kirusi chenyewe. Ina maana Brela haina STANDARD moja ya kazi kiasi kwamba kila mtu ana marekebisho yake. Yaani marekebisho sio STANDARD bali mtazamo wa mtendaji. Utumishi wa hovyo na wa Kijima kabisa.
Inakuwaje jambo ambalo jana mtendaji fulani alipitia na kuliona sio la marekebisho, mtendaji aliepitia leo akaona ni la marekebisho, na mwingine anayepitia kesho kutwa akaona jingine ambalo wa jana hakuona, na mwingine wa mtondogoo akaona jingine ambalo wa juzi hakuona, hivyo na hivyo na kuendelea. Wallah kazi haziwezi kufanyika hivyo. Huu ni mchezo na masihala.
Au mpaka mtu amuone mtu, ujinga mtupu. Waulizeni wadau wa usajili hasa Mawakili na Wanasheria kama hiki nilichoeleza ni tatizo ama hapana mtapata majawabu.
Tunataka mtu akisubmit kazi, mtendaji anayeshika hiyo kazi aipitie kwa umakini na kuainisha marekebisho yooote lwa pamoja(kama yapo), na asiache hata moja.
Kisha arejeshe hiyo kazi ili yafanyiwe marekebisho na mhusika. Kama yamerekebishwa vizur mpatie Certificate. Kama sio mrejeshee tena yale yale yamaliziwe na sio umletee mapya.
Ukileta mapya tafsiri yake ni kwamba ile mara ya kwanza hukupitia kwa umakini. Ulizembea na hiki ndicho tunachopinga kwa nguvu zote. Kampuni itachukua mwezi na zaidi kusajiliwa.
Pengine hamjui umuhimu wenu katika Uwekezaji Tanzania. Ni hivi, Brela ndio mlango ama hodi ya uwekezaji. Sababu mwekezaji hawezi kwenda hata TIC au Immigration kama hana certificate ya Brela. Mwekezaji lazima aanzie Brela kwanza ndo aende kwingine.
TAFADHALI Brela Acheni Kukimbiza Wawekezaji.
Zaidi, soma: BRELA ( Business Registration and Licensing Agency) kuna matatizo makubwa! Waziri wa Viwanda na Biashara tunakuomba uingilie kati haraka!
Pia soma >Ufafanuzi juu ya madai ya BRELA kukimbiza wawekezaji
Na Bashir Yakub, WAKILI.
+255 714 047 241
Mfumo kama mfumo wa kusajili kampuni ni mzuri na unarespond haraka ila watendaji bado kabisa.
Nitatoa mfano na sina shaka kila mdau ambaye anasajili ama amewahi kusajili kampuni au biashara kupitia mfumo mpya wa Brela atakubaliana nami.
Ni hivi, unakamilisha docmnts na kusubmit online Brela. Unasubiri majib na baada ya muda unajibiwa ufanye marekebisho(Additional Information/correction is required.
Unafanya marekebisho yote uliyoelekezwa na unasubmit upya. Baada ya siku au siku mbili dcmnt zinarejeshwa tena kuwa ufanye tena marekebisho(Additional Information/correction is required.
Kinachouma sana na kukera sana ni kwamba haya marekebisho unayoambiwa ufanye kwa hii mara ya pili ni MAPYA. Kwa maana dcmnt zilivyorejeshwa mara ya kwanza hayakuwa matatizo ila mara ya pili yameonekana ni matatizo.
Unarekebisha mara ya pili na kusubmit tena. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required.
Haya ya mara ya tatu nayo unakuta ni MAPYA. Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili yameonwa mara ya tatu.
Unarekebisha tena na kusubmit. Unasubiri tena siku ama siku mbili au zaidi. Inarudishwa tena ikihitaji marekebisho(Additional Information/correction is required.
Haya ya mara ya nne nayo ni marekebisho MAPYA.
Maana yake hayakuonwa uliporudishwa mara ya kwanza, hayakuona uliporudishwa mara ya pili, hayakuona uliporudishwa mara ya tatu, sasa yameonwa mara ya nne.
Mchezo unaendelea hivyo mpaka mwezi au zaidi. Halafu unasikia Mtendaji Mkuu wa Brela inaiambia Serikali, Dunia, na Wawekezaji kuwa sasa Tanzania Brela inasajili Kampuni na Biashara ndani ya saa 24. Ni aibu sana.
Hoja sio kwamba marekebisho yasifanywe ama usajili ufanyike bila sifa kutimia, Laa hasha.
Hoja ni kwamba, huyu anayesoma dcmnt na kuzirejesha anashindwaje kupitia dcmnt nzima yote kwa umakini, akaorodhesha yoooote yanayotakiwa kufanyiwa marekebisho, ukairudisha ili yote yafanyike kwa pamoja.
Inakuwaje marekebisho yasionwe dcmnt ziliporudishwa mara ya kwanza yaje kuonwa mara ya pili na ya tatu na kuendelea.
Na bora ingekuwa kwamba kile ulichoambiwa kurekebisha umekirekebisha vibaya kwahiyo unatakiwa ukirekebishe vizuri zaidi, hapana. Hiki ulichoambiwa kurekebisha kinaachwa kwa maana kuwa umekirekebisha vizur unaletewa kipya kabisa ambacho hakikuwa kimeonwa mara ya kwanza, ama ya pili, ama ya tatu. Ni kero, usumbufu, na aibu kwa watendaji.
Msichojua ni kwamba wengi wanaosajili Makampuni na biashara ni Wawekezaji.
Anakuja mwekezaji kutoka nje unamuhakikishia kuwa ndani ya siku moja,mbili,tatu utakuwa umemsajilia Kampuni. Anasubiri siku, wiki, wiki mbili, tatu, mwezi mwezi na zaidi hakuna kitu.
Mimi kama Wakili, ama mtu mwingine aliyepewa kazi ya kusajili siwezi kukubali kuaibika kwa mteja wangu. Nitamwita, nitamuonesha majibu ya Brela kwenye system. Nitamuonesha marekebisho mapya ambayo hayakuwa yameletwa mwanzoni yanavyoletwa kila baada ya siku mbili au wiki.
Ataelewa kosa sio langu ni la BRELA. Ataondoka sababu hawez kusubiri zaidi anaingia gharama kubwa za Malazi. Ataenda kufungua Kampuni Rwanda au Kenya ambako kwa dhati yake kampuni inasajiliwa ndani au chini ya Saa 24. Hivi ndivyo tunavyopoteza wawekezaji kupitia Brela.
Lakini ni kero zaidi sababu kila marekebisho yanahitaji wanahisa ama wakurugenzi wasaini. Utawaita kusaini mara ngapi. Na vipi kama walisaini wakaondoka na kwenda mbali.
Kuna mda unawaza labda pengine aliyepitia kazi mara ya kwanza siye aliyeipitia mara ya pili, na siye aliyepitia mara ya tatu, pengine ndo maana kila mtu ametaka marekebisho yake tofauti.
Kama ndivyo, basi hiki ndicho kirusi chenyewe. Ina maana Brela haina STANDARD moja ya kazi kiasi kwamba kila mtu ana marekebisho yake. Yaani marekebisho sio STANDARD bali mtazamo wa mtendaji. Utumishi wa hovyo na wa Kijima kabisa.
Inakuwaje jambo ambalo jana mtendaji fulani alipitia na kuliona sio la marekebisho, mtendaji aliepitia leo akaona ni la marekebisho, na mwingine anayepitia kesho kutwa akaona jingine ambalo wa jana hakuona, na mwingine wa mtondogoo akaona jingine ambalo wa juzi hakuona, hivyo na hivyo na kuendelea. Wallah kazi haziwezi kufanyika hivyo. Huu ni mchezo na masihala.
Au mpaka mtu amuone mtu, ujinga mtupu. Waulizeni wadau wa usajili hasa Mawakili na Wanasheria kama hiki nilichoeleza ni tatizo ama hapana mtapata majawabu.
Tunataka mtu akisubmit kazi, mtendaji anayeshika hiyo kazi aipitie kwa umakini na kuainisha marekebisho yooote lwa pamoja(kama yapo), na asiache hata moja.
Kisha arejeshe hiyo kazi ili yafanyiwe marekebisho na mhusika. Kama yamerekebishwa vizur mpatie Certificate. Kama sio mrejeshee tena yale yale yamaliziwe na sio umletee mapya.
Ukileta mapya tafsiri yake ni kwamba ile mara ya kwanza hukupitia kwa umakini. Ulizembea na hiki ndicho tunachopinga kwa nguvu zote. Kampuni itachukua mwezi na zaidi kusajiliwa.
Pengine hamjui umuhimu wenu katika Uwekezaji Tanzania. Ni hivi, Brela ndio mlango ama hodi ya uwekezaji. Sababu mwekezaji hawezi kwenda hata TIC au Immigration kama hana certificate ya Brela. Mwekezaji lazima aanzie Brela kwanza ndo aende kwingine.
TAFADHALI Brela Acheni Kukimbiza Wawekezaji.
Zaidi, soma: BRELA ( Business Registration and Licensing Agency) kuna matatizo makubwa! Waziri wa Viwanda na Biashara tunakuomba uingilie kati haraka!
Pia soma >Ufafanuzi juu ya madai ya BRELA kukimbiza wawekezaji