Wanaodai Serikali Haijafanya kitu huwa wanamaanisha nini?

yamindinda

JF-Expert Member
Jul 29, 2011
1,581
1,318
Unaposema Serikali haijafanya kitu unamanisha bado tuko kwenye enzi za ujima au?
Kwamba bado tuko kwenye CHUO KIKUU KIMOJA ?Unamanisha bado tuko kwenye barabara za 1961?
Unasema tunatumia zile Tv za Rangi moja?
Kutoka mkoa mmoja hadi mwingine bado tunatumia siku 7 kufika?
Unamanisha hata wewe mtindo wako wa MAISHA ni uleule mfano mavazi unavaa ya 1961?
Nyumba na magari tuliyonayo ni yale yale ya mwaka 1961?
Teknolojia kiujumla mfano ya simu ni ile ile bado iko kwa wafanyakazi wa serikali na watu wenye kipato cha sukari?
Na kampuni ni moja tu TTCL?
Unasema serikali haijafanya kitu,Kwamba huduma za maji na umeme nyumba ni zile zile za wachache 1961?
Unasema bado tuko mil 12 ya mwaka 1970?
Na sio Mil 50 na ya sasa?
Kituo cha radio ni Rtd pekee na kusikiliza habari mpaka twende kwa mwenyekiti au balozi au jirani mwenye nayo?
Unamanisha hatuna kituo cha tv hata kimoja maana miaka 50 serikali haifanya kitu?
Jaribu kurudi mika 50 nyuma njoo taaratibu mpaka hapa tulipo je tuko vilevile?
Maana ninavyojuwa mpaka hapa tulipo mabadiliko makubwa ktk sekta mbalimbali yamefanyika,
Kubwa kabisa hili la kisiasa,katka jambo kubwa ambalo serikali ya CCM imefanya na la kupigiwa makofi na kila mtu na Ambalo watu wengi HAWAJUI ni kukubali mfumo huu wa vyama vingi,
Tena CCM na serikali ili lazimisha maana kura ya hapana zilizidi za ndiyo namaanisha asilimia 80 walikataa na 20 kukubali,Kwa nini tukubali asilimia 20 wakati uwezo wa kukataa ulikuwepo na wa kimsingi kabisa,
Kwa hiyo wote mnaopiga kelele na kubeza serikali ya CCM haijfanya kitu ni VYEMA Mkaa na kupitia vyema historia ya nchi hii ili mjuwe tulipo na tumetoka wapi.
Baaadhi yenu ni ubishi tu wa kimmemko unajuwa kabisa hatua kubwa zilizofanywa na serikali kuleta maendeleo na kuleta mabadiliko makubwa kiutendaji na kiuwajibika serikalini,ili kuleta tija zaidi..
Kuona mnaona kinachofanyika Halafu mnasema serikali ya CCM Haijafanya kitu,
Tangu uhuru juhudi mbalimbali zimefanyika mpaka kwenye mageuzi ya kisiasa,maana uwezo wa kufata zile asilimia 80 ulikuwepo lakini wakaona wachukuwe na kukubali asilimia 20 ni jambo kubwa.
Sasa ukiacha hilo kubwa yako makubwa mengi ambayo mpaka sasa serikali ya CCM imefanya na wala huwezi kukwepa kuyasema,
utakwepa tu ukiwa na miwani ya mbao na pia uwe unatoka ktk chama ambacho mawazo yake ni kupinga tu kila kitu.
Nyanja zote na katka sekta mbali mbali serikali imejitahidi sana kuleta maendeleo na tumepiga hatua,
Kama ni swala la umasikini watu kuomba omba watu kulia lia maisha magumu ni la dunia kila nchi utakuta watu wanasema maisha ni magumu,
Wajibu wa serikali ni kutuwekea miudo mbinu mizuri huduma mbalimbali muhimu kiwajibu kijamii,na sisi kusaidia ktk maedeleo,
Huduma za kijamii zinazidi kuboreshwa miundo mbinu nk,
Ushirika wetu na serikali ni kusaidia kufanya kazi halali na kwa bidii Familia zetu maisha yaboreke na serikali ipate kodi pesa irudi kuleta maedeleo.
Serikali haitakuja kukutafutia chakula na kukuletea nyumbani kwako huku umekaa tu,
Unaposema hakuna kilichofanyika ni wajibu wako sasa kutueleza tulipo na tulipotoka kimaisha kimaendeleo kila nyanja yakoje maaa wengine ni viongozi wa vyama wana makampuni makubwa maisha yao ni ya kusaza lakni wamekuwa mstari wambele kubeza ni vyema wakatuambia sasa tulipo na na 1961 Si Kupayuka tu serikali ya CCM et haijafanya kitu kwa muhemko wao wa kisiasa.
Serikali ya awamu ya tao imejitahidi saa kupambana kuleta maendeleo kwa Watanzania wote tunaona juhudi za mh Rais anazofanya ni za kizalendo sana,
Wale mnaobeza inawezakana nia yenu si njema sana kwa nchi yetu,Rais anapigana sana kutetea masilahi ya wanyonge,
Tumuunge mkono Rais ni kweli maendeleo hayana chama mambo ya siasa kwenye masilahi ya nchi tuweke pembeni na tujenge Nchi yetu pendwa Tanzania.

MUNGU IBARIKI TANZANIA,
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.
Baraka Masaba
 
Yani hoja zako umezitoa wapi, poor kabisa. Hujiulizi wangapi tulioanza nao mbio za kiuchumi wapo wapi baada ya miaka 50 kupita? Unaikumbuka china miaka iyo? South afrika je, turudi namibia, tukumbushane majirani zetu kenya wapoje saiv.
Mkuu hii hoja yako inastahili kuwa FB
 
Kidumu chama cha.... na upupu ulioandika hapa vinafanana kabisa. Kama huna data keep your mouth shut. Kwanza hakuna mtu anayesema Serikali haijafanya kitu. Wengi wanauliza mbona serikali imekuwa ikifanya vitu kwa muda wa zaidi ya miaka 50 na Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini duniani? Kama unajua jibu lake tunaomba tusaidie tafadhali, badala ya kuandika ujinga usiokuwa na maana. Tanzania Hata haimo katika nchi ambazo per capita income zake imekua kwa haraka zaidi ndani ya kipindi cha miaka 15 iliyopita (Nchi zilizomo katika kundi hilo ni Ghana na Angola). Hebu linganisha pia: Nchi inayoongoza kwa utajiri Afrika (Kwa kutumia kiashiria cha per capita income) ni Mauritius ambayo per capital income yake ni $ 21,700. Inayofuata katika list hiyo ni South Africa yenye $10,300, na Namibia $10,200. Kwa taarifa yako per capita income ya Tanzania ni $1,100!
 
Yani hoja zako umezitoa wapi, poor kabisa. Hujiulizi wangapi tulioanza nao mbio za kiuchumi wapo wapi baada ya miaka 50 kupita? Unaikumbuka china miaka iyo? South afrika je, turudi namibia, tukumbushane majirani zetu kenya wapoje saiv.
Mkuu hii hoja yako inastahili kuwa FB
Tupe GDP ya nchi hizo 1960 tulinganishe na za Tz
 
Yani hoja zako umezitoa wapi, poor kabisa. Hujiulizi wangapi tulioanza nao mbio za kiuchumi wapo wapi baada ya miaka 50 kupita? Unaikumbuka china miaka iyo? South afrika je, turudi namibia, tukumbushane majirani zetu kenya wapoje saiv.
Mkuu hii hoja yako inastahili kuwa FB
Embu toa mifano ya hao tulioanza nao kiuchumi ????
 
Kidumu chama cha.... na upupu ulioandika hapa vinafanana kabisa. Kama huna data keep your mouth shut. Kwanza hakuna mtu anayesema Serikali haijafanya kitu. Wengi wanauliza mbona serikali imekuwa ikifanya vitu kwa muda wa zaidi ya miaka 50 na Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini duniani? Kama unajua jibu lake tunaomba tusaidie tafadhali, badala ya kuandika ujinga usiokuwa na maana. Tanzania Hata haimo katika nchi ambazo per capita income zake imekua kwa haraka zaidi ndani ya kipindi cha miaka 15 iliyopita (Nchi zilizomo katika kundi hilo ni Ghana na Angola). Hebu linganisha pia: Nchi inayoongoza kwa utajiri Afrika (Kwa kutumia kiashiria cha per capita income) ni Mauritius ambayo per capital income yake ni $ 21,700. Inayofuata katika list hiyo ni South Africa yenye $10,300, na Namibia $10,200. Kwa taarifa yako per capita income ya Tanzania ni $1,100!
Nadhani utakuwa hauna kumbukumbu nzuri......Wapinzani wa CCM wameitumia hii hoja ya kuwaaminisha wananchi kuwa CCM haijafanya kitu.
"Wengi wanauliza mbona serikali imekuwa ikifanya vitu kwa muda wa zaidi ya miaka 50 na Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini duniani?" sidhani kama kwenye knowledge ya uchumi kuna vipimo vya kupima muda ambao nchi inaweza kutoka kwenye stage moja ya maendeleo kwenda stage nyingne.....kama ipo tutajie???

"Kama unajua jibu lake tunaomba tusaidie tafadhali, badala ya kuandika ujinga usiokuwa na maana. " kama thread ni ujinga usio kuwa na maana nadhani ungeupuuzia......ila kwa kujibu kwako inamaanisha kuwa kuna hoja za msingi.
 
Kidumu chama cha.... na upupu ulioandika hapa vinafanana kabisa. Kama huna data keep your mouth shut. Kwanza hakuna mtu anayesema Serikali haijafanya kitu. Wengi wanauliza mbona serikali imekuwa ikifanya vitu kwa muda wa zaidi ya miaka 50 na Tanzania ni miongoni mwa nchi masikini duniani? Kama unajua jibu lake tunaomba tusaidie tafadhali, badala ya kuandika ujinga usiokuwa na maana. Tanzania Hata haimo katika nchi ambazo per capita income zake imekua kwa haraka zaidi ndani ya kipindi cha miaka 15 iliyopita (Nchi zilizomo katika kundi hilo ni Ghana na Angola). Hebu linganisha pia: Nchi inayoongoza kwa utajiri Afrika (Kwa kutumia kiashiria cha per capita income) ni Mauritius ambayo per capital income yake ni $ 21,700. Inayofuata katika list hiyo ni South Africa yenye $10,300, na Namibia $10,200. Kwa taarifa yako per capita income ya Tanzania ni $1,100!

"Tanzania Hata haimo katika nchi ambazo per capita income zake imekua kwa haraka zaidi ndani ya kipindi cha miaka 15 iliyopita (Nchi zilizomo katika kundi hilo ni Ghana na Angola). Hebu linganisha pia: Nchi inayoongoza kwa utajiri Afrika (Kwa kutumia kiashiria cha per capita income) ni Mauritius ambayo per capital income yake ni $ 21,700. Inayofuata katika list hiyo ni South Africa yenye $10,300, na Namibia $10,200. Kwa taarifa yako per capita income ya Tanzania ni $1,100!"[/QUOTE] Source ya hizi data zako ni wapi???? acha kudanganya watu

upload_2017-11-3_14-18-43.png

 
Hayo nayo utaita ni MAENDELEO?
Acha utani.
Tembea hapa hapa Afrika ujionee nchi zilizo endelea.
 
Ni vigumu mno kulielewesha linyumbu likakuelewa.John Kennedy aliwahi kusema usiulize Marekani itakufanyia nini bali jiulize wewe utaifanyia nini Marekani. Sasa haya Manyumbu yanashabikia wale wanaoenda kuwaambia wawekezaji kuwa tuna ndege yetu Canada ikamateni. Unategemea yataifanyia nini Tanzania zaidi ya kukwiba Raslimali zetu?
 
We unakiona
1.posho za wabunge wa upinzani zimeongezeka tofauti na za miaka 1960
2.ruzuku kwa vyama vya upinzani zimeongezeka kuliko kipindi cha akina nyerere
3.magari ya wabunge wanayopewa upinzani ni ya kifahari kuliko ya wakati wa nyerere
4.Kila mbunge ana simu zaidi ya moja za mkononi ambazo hazikuwepo wakati wa nyerere
 
Back
Top Bottom