Uhalifu ni kufanya kinyume na katiba na sheria za nchi. Katiba ya nchi yetu imetoa vipindi viwili vya miaka 5 kila kipindi cha mtu kuwa Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania, kwa hiyo kufanya kinyume na hilo ni uhalifu na kuvunja katiba na sheria za nchi.
Sioni kama kuna sababu ya vyombo vya dola kunyamaza na kushindwa kuwachukulia hatua wale wote wanaojitokeza hadharani kutamka wazi kwamba Rais Magufuli aongezewe muda baada ya kipindi chake kwisha. Watu hawa wanahatarisha amani ya nchi kwani nchi nyingi za Afrika zimeingia ktika vita ya wao kwa wao kwa sababu ya marais kujiongezea muda kinyume na matakwa ya nchi, hivyo kupuuzia kauli hizi ni kutengeneza bomu katika taifa.
Inawezekana watu hawa wametumwa au wanafanya hivyo kwa makusudi ili kupima upepo.
Niwaambie wazi hata wanaccm wengi hawaipendi hii kauli maana wapo vijana waliokuwa kuwa wamejikeza kwa wingi 2015 kutaka kugombea kupitia ccm ila JPM akateuliwa na chama chake, kwa akili nyepesi wanaosema lugha hizi wanadhani ni wapinzani tu ndio wanaweza kuzipinga la hasha hata wana ccm wengi hawataki hizi kauli.
Mbaya zaidi kama kauli hizi zitaendelea bila kuchukuliwa hatua, muda simrefu watajitokeza watu barabarani au mtu mmoja mmoja watakao dai kuwa JPM apunguziwe muda asiongoze hadi 2020 polisi mtawakamata na kuwaita wachochezi je hawa nao hawachochei?
Sioni kama kuna sababu ya vyombo vya dola kunyamaza na kushindwa kuwachukulia hatua wale wote wanaojitokeza hadharani kutamka wazi kwamba Rais Magufuli aongezewe muda baada ya kipindi chake kwisha. Watu hawa wanahatarisha amani ya nchi kwani nchi nyingi za Afrika zimeingia ktika vita ya wao kwa wao kwa sababu ya marais kujiongezea muda kinyume na matakwa ya nchi, hivyo kupuuzia kauli hizi ni kutengeneza bomu katika taifa.
Inawezekana watu hawa wametumwa au wanafanya hivyo kwa makusudi ili kupima upepo.
Niwaambie wazi hata wanaccm wengi hawaipendi hii kauli maana wapo vijana waliokuwa kuwa wamejikeza kwa wingi 2015 kutaka kugombea kupitia ccm ila JPM akateuliwa na chama chake, kwa akili nyepesi wanaosema lugha hizi wanadhani ni wapinzani tu ndio wanaweza kuzipinga la hasha hata wana ccm wengi hawataki hizi kauli.
Mbaya zaidi kama kauli hizi zitaendelea bila kuchukuliwa hatua, muda simrefu watajitokeza watu barabarani au mtu mmoja mmoja watakao dai kuwa JPM apunguziwe muda asiongoze hadi 2020 polisi mtawakamata na kuwaita wachochezi je hawa nao hawachochei?