Watanzania wenzangu tusicheze na mambo yanayoonekana kama mzaha, kumbe ndani yake kuna maafa.
Zaburi 1:1 heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki, wala hakusimama katika njia ya wakosaji; wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Swala hili la Rais kuongezewa muda limeanza kushika kasi kiasi kwamba tumelichukulia kama utani tu na mzaha, ila ukweli ni huu matamshi yote yanayotamkwa ya kumuongezea Rais muda ni uchochezi maana yanaenda kinyume na katiba. Je kama watu wangejitokeza na kusema Rais apunguziwe muda, vyombo vya dola vingechukulia kuwa ni mzaha na utani au mtu huyo angechukuliwa hatua za kisheria?
Je kama wangejitokeza watu wakabeba mabango yaliyoandikwa tunaomba bunge libadilishe vifungu vya katiba Rais apunguziwe muda wa kutawala iwe miaka mitatu tu, vyombo vya dola vingewavumilia?
Kumbukeni wakina Mgabe, Kagame na Museven walipata watu wachache walioanza kuchochea hivyo kuwa waendelee kuongoza na matokeo yake wamefanya hivyo.
Hatujaona Rais akikemea watu hao wanaotoa matamko ya kuvunja katiba na kuchochea fikra za watanzania, maana imani huja kwa kusikia.
Wanaosema Rais aongezewe muda sio wachochezi?
Zaburi 1:1 heri mtu yule asiyekwenda katika shauri la wasio haki, wala hakusimama katika njia ya wakosaji; wala hakuketi barazani pa wenye mizaha.
Swala hili la Rais kuongezewa muda limeanza kushika kasi kiasi kwamba tumelichukulia kama utani tu na mzaha, ila ukweli ni huu matamshi yote yanayotamkwa ya kumuongezea Rais muda ni uchochezi maana yanaenda kinyume na katiba. Je kama watu wangejitokeza na kusema Rais apunguziwe muda, vyombo vya dola vingechukulia kuwa ni mzaha na utani au mtu huyo angechukuliwa hatua za kisheria?
Je kama wangejitokeza watu wakabeba mabango yaliyoandikwa tunaomba bunge libadilishe vifungu vya katiba Rais apunguziwe muda wa kutawala iwe miaka mitatu tu, vyombo vya dola vingewavumilia?
Kumbukeni wakina Mgabe, Kagame na Museven walipata watu wachache walioanza kuchochea hivyo kuwa waendelee kuongoza na matokeo yake wamefanya hivyo.
Hatujaona Rais akikemea watu hao wanaotoa matamko ya kuvunja katiba na kuchochea fikra za watanzania, maana imani huja kwa kusikia.
Wanaosema Rais aongezewe muda sio wachochezi?