Wanaochochea siasa ya udini na ukabila siyo Waislamu na Wakristo bali pia wanaotafuta uongozi kama M

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797

Tuesday, December 17, 2013



lema+pix.jpg

Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema akichangia mjadala bungeni wa Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Mjini Dodoma jana. Picha na Emmanuel Herman


“Najua siku hizi zipo DvD za kutengeneza, kuna utaalamu wa kuzibaini kwa hiyo sina shaka yoyote,” alisema Ole Medeye.

Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi (CCM), alisema Lema yuko katika wakati mgumu kisiasa na kauli aliyoitoa ni ya mfa maji ambaye anakaribia kufa hivyo hutapatapa akitafuta mtu wa kufa naye.

Akichangia taarifa za kamati hizo mbili, Lema alitumia fursa hiyo kuhoji kwa nini Ole Medeye aliyehudhuria kikao cha kuchochea ukabila asitajwe kama mtu mhalifu wa kwanza duniani.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo DVD ya Naibu Waziri wa Ardhi akiwa kwenye kikao cha ukabila wakati wa uchaguzi katika kampeni za udiwani Arusha Mjini na kutoa maazimio ya kuwapa wageni sumu na kuwapiga mishale na mikuki,” alisema.

Alisema katika kikao hicho ambacho alidai Ole Medeye ndiye aliyekisimamia, pia kulitolewa maazimio ya kuhakikisha wageni hawauziwi mashamba.

“Taarifa hizo nilipeleka polisi, pia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, OCD (Kamanda wa Polisi wa Wilaya) na John Mongela (Mkuu wa Wilaya wa Arusha), ambaye nilimwambia na alikiri amelisikia na analifanyia kazi suala hilo lakini mpaka leo hakuna lolote....

“Naibu Waziri anakaa kwenye kikao na kuhamasisha ukabila kwa sababu tu chama chake kishinde uchaguzi. Mheshimiwa Mwenyekiti taifa hili litakwenda mahali pabaya sana.”

Lema alisema wanaochochea siasa ya udini na ukabila siyo Waislamu na Wakristo walioko misikitini na kanisani, bali ni wanasiasa wanaotafuta nafasi za kuongoza kama alivyofanya Ole Medeye katika kampeni hizo.
“Najua siku hizi zipo DvD za kutengeneza, kuna utaalamu wa kuzibaini kwa hiyo sina shaka yoyote,” alisema Ole Medeye.

Medeye ambaye pia ni Mbunge wa Arumeru Magharibi (CCM), alisema Lema yuko katika wakati mgumu kisiasa na kauli aliyoitoa ni ya mfa maji ambaye anakaribia kufa hivyo hutapatapa akitafuta mtu wa kufa naye.

Akichangia taarifa za kamati hizo mbili, Lema alitumia fursa hiyo kuhoji kwa nini Ole Medeye aliyehudhuria kikao cha kuchochea ukabila asitajwe kama mtu mhalifu wa kwanza duniani.

“Mheshimiwa Mwenyekiti, ninayo DVD ya Naibu Waziri wa Ardhi akiwa kwenye kikao cha ukabila wakati wa uchaguzi katika kampeni za udiwani Arusha Mjini na kutoa maazimio ya kuwapa wageni sumu na kuwapiga mishale na mikuki,” alisema.

Alisema katika kikao hicho ambacho alidai Ole Medeye ndiye aliyekisimamia, pia kulitolewa maazimio ya kuhakikisha wageni hawauziwi mashamba.

“Taarifa hizo nilipeleka polisi, pia kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama, OCD (Kamanda wa Polisi wa Wilaya) na John Mongela (Mkuu wa Wilaya wa Arusha), ambaye nilimwambia na alikiri amelisikia na analifanyia kazi suala hilo lakini mpaka leo hakuna lolote....

“Naibu Waziri anakaa kwenye kikao na kuhamasisha ukabila kwa sababu tu chama chake kishinde uchaguzi. Mheshimiwa Mwenyekiti taifa hili litakwenda mahali pabaya sana.”

Lema alisema wanaochochea siasa ya udini na ukabila siyo Waislamu na Wakristo walioko misikitini na kanisani, bali ni wanasiasa wanaotafuta nafasi za kuongoza kama alivyofanya Ole Medeye katika kampeni hizo.






MWANANCHI











 
Ole Madeye anatakiwa Wana Arusha wammabine tu basi

hapo mh.Lema hajakosea. Hili suala liliongelewa sana wakati wa uchaguzi wa madiwani kwenye vyombo vya habari na hiyo video mimi niliiangalia kwenye you tube. Mh Medeye ame wahamisha afisa ardhi Mtui na Mkurugenzi wake hawa walikuwa wanajaribu kutusaidia kupatikana makazi yaliyo pangwa kwa kuzungumza na wenye mashamba makubwa mfano ni Gomba na Burka kitu ambacho mabwana ardhi wengi wameshindwa kwani arusha ndo inaongoza kwa makazi yasiyo rasmi. Eneo la lakilaki mh medeye amepinga lisiuzwe kwa wananchi kwa sababu zisizo wazi imelazimu serikali kubeba deni la halmashauri. Wafuatiliaji wa mambo wanasema medeye ataki wageni wanunue ardhi kwenye jimbo lake kwani wengi hawapigii kura ccm. Vile vile amepiga marufuku hati za ardhi kutolewa kwa yeyote yule atakaye nunua kiwanja au shamba katika wilaya yake, ukitaka uthibitisho nenda ardhi arumeru au kanda pale moshi uone moto wake! Kwa kweli mh medeye sio mwanasiasa mzuri katika kizazi hiki anachukia watu wote wasio wamasai au waarusha wanoishi hapa jijini arusha, arumeru na vitongoji vyake. Na kwa kuwa ccm ni kulindana basi hakuna lolote litakalo fanywa juu yake
 
Back
Top Bottom