Wanaobakwa wasioge, wasibadili nguo

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
CHAMA cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimewatahadhalisha Wanawake watakaobakwa kutooga au kubadilisha nguo kwa sababu kufanya hivyo kunapoteza ushahidi wa kumtia hatiani Mtuhumiwa.

Taarifa iliyoandaliwa na Tamwa kupitia Mtandao wake wa kijamii zinasema, Madaktari nchini wameshauri wanaobakwa kufika haraka kituo cha polisi kuchukua PF3 na kuipeleka hospitali kwaajili ya kupata matibabu ikiwamo dawa za kuzuia maambukizi ya virusi vya ukimwi.


Akinuliwa na Chama hicho, Dk Zuberi Mzige wa hospitali ya Mwananyamala iliyopo jijini Dar es S alaam alisema , kumekuwa na tabia ya watoto wa kike wanaofikishwa hospitalini baada ya kubakwa kutokuwa na ushahidi kutokana na kuoga au kubadilisha nguo.

“Wengine wanafikishwa hospitalini wakiwa wamecheleweshwa hivyo kuwa kwenye hatari ya maambukizo ya HIV” taarifa ilimnukuu.Naye Dk Prisca Berege anayeshughulikia magonjwa ya watoto katika hospitali ya Mwananyama alisema , mji wa Dar es Salaam una tatizo la ubakaji hasa kwa watoto.

Alizungumza hayo na Wanahabari walioshiriki katika mkutano wa utafiti wa maswala ya ukatili wa kijinsia ulioandaliwa na TAMWA hivi karibuni katika Manispaa ya Kinondoni jijini Dar es Salaam.

“Kila siku hospitali ya Mwananyama lazima tupokee watu watatu waliobakwa ambao ni wanawake na watoto” alisema Dk Barege.

Dk Barege aliwashauri wazazi kuepuka kuwatuma watoto wao nyakati za usiku na kuwatahadharisha watoto wa kike kuwa makini na uhusiano baina yao na wanaume waliozoeana.

Alitoa mfano wa binti mmoja ambaye hivi karibuni alibakwa mchana na mwanaume aliyemwamini kama kaka n amwajiri wake baada ya kumwita nyumba ni kwake ili wapange kazi ya kufanya.
 
janabaaaaaaaaaaaaaaa jamaniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii...........lol haya sasa utapandaje gari na janaba? si utawanukia wengine?
 
Back
Top Bottom