Mchimwachimego
JF-Expert Member
- Jun 15, 2020
- 358
- 271
Historia yangu na wanangu ni ya kusikitisha, kufurahisha, inatia huruma na kushangaza. Mwaka 2015 niliwaita wanangu wanieleze wanakerwa na jambo gani ambalo mimi baba yao silisimamii vyema, wengi zaidi 80% walisema hawapendendezwi na udhaifu wangu katika kusimamia shamba na walieleza mengi sana baadhi ya hayo yalikuwa kuwa shamba linatumiwa vibaya na baadhi yao, wapo wanaouza mazao bila kushirikisha wengine, wapo wanakata miti na kuuza,wapo wanaolima bhangi na kuvuta,wapo wanaochimbisha mchanga na kuuza, wapo wanaouza mifugo hovyo, wapo wanaofanya shamba njia ya wahuni, NK.
Baada tafakari ya muda nikawauliza kuwa lakini hayo yote si mnayafanya ninyi wenyewe miongoni mwenu na mnapata pesa na mnafurahia maisha ya starehe, wakajibu ni sawa lakini baba mambo haya hayawezi kuwa na faida za muda mrefu ni bora ukomeshe na uwe mkali ili hizi mali zitunufaishe wote.
Baada ya miaka mitano watoto wangu wamekuwa kama nyati aliyejeruiwa maana wanalalamika kwamba eti hapo zamani wakati shamba lilikuwa chini ya bibi walikuwa wanapata sana pesa za matanuzi na starehe tena bila kazi ngumu lakini tokea bibi yao amefariki na kunipa mimi usimamizi na uthibiti wamekuwa ombaomba wakati mali ipo pia wanalalamika kuwa nawajengea ukuta kuzunguka shamba na ninawajengea nyumba shambani, shule, mabwawa, vyote hivyo vya nini wakati pesa hawana wanasema.
Ni bora wapate pesa za matanuzi na starehe kuliko kuwafanyia maendeleo. Nimewauliza vipi mbona mmebadilika wakati ninyi mlisema kuwa nisimamie matumizi mabaya ya shamba ili mnufaike wote au mlidhani kuwa nikithibiti pesa itakuwa kama zamani?
Wakasema kabisa kumbe ukidhibiti uhalifu na pesa inapotea tulikuwa hatujui bora turudi tulikotoka hata kama shamba likiisha watoto wetu watajijua kivyao, sisi tunataka uhuru wa manyani yaani kila kitu ruksa hata tukiangamia au tukiishiwa sawa tu! walikuwa wanaongea huku wakiwa wanapiga kelele.
Sasa ndugu zangu, nimeona niwasimulie ili mnisaidie maana kuna mtoto mmoja yeye anaoneka yuko tofauti na wengine amenidokeza kuwa wamepanga waniue ili shamba walitumie wanavyotaka bila kubughudhiwa, sasa nawauliza wanajamvi wenzangu niwaachie ili wasiniue au nipambane nao ili kulitunza kwa ajili ya vizazi vyao baadaye nao walikute Shamba.
Asanteni.
Baada tafakari ya muda nikawauliza kuwa lakini hayo yote si mnayafanya ninyi wenyewe miongoni mwenu na mnapata pesa na mnafurahia maisha ya starehe, wakajibu ni sawa lakini baba mambo haya hayawezi kuwa na faida za muda mrefu ni bora ukomeshe na uwe mkali ili hizi mali zitunufaishe wote.
Baada ya miaka mitano watoto wangu wamekuwa kama nyati aliyejeruiwa maana wanalalamika kwamba eti hapo zamani wakati shamba lilikuwa chini ya bibi walikuwa wanapata sana pesa za matanuzi na starehe tena bila kazi ngumu lakini tokea bibi yao amefariki na kunipa mimi usimamizi na uthibiti wamekuwa ombaomba wakati mali ipo pia wanalalamika kuwa nawajengea ukuta kuzunguka shamba na ninawajengea nyumba shambani, shule, mabwawa, vyote hivyo vya nini wakati pesa hawana wanasema.
Ni bora wapate pesa za matanuzi na starehe kuliko kuwafanyia maendeleo. Nimewauliza vipi mbona mmebadilika wakati ninyi mlisema kuwa nisimamie matumizi mabaya ya shamba ili mnufaike wote au mlidhani kuwa nikithibiti pesa itakuwa kama zamani?
Wakasema kabisa kumbe ukidhibiti uhalifu na pesa inapotea tulikuwa hatujui bora turudi tulikotoka hata kama shamba likiisha watoto wetu watajijua kivyao, sisi tunataka uhuru wa manyani yaani kila kitu ruksa hata tukiangamia au tukiishiwa sawa tu! walikuwa wanaongea huku wakiwa wanapiga kelele.
Sasa ndugu zangu, nimeona niwasimulie ili mnisaidie maana kuna mtoto mmoja yeye anaoneka yuko tofauti na wengine amenidokeza kuwa wamepanga waniue ili shamba walitumie wanavyotaka bila kubughudhiwa, sasa nawauliza wanajamvi wenzangu niwaachie ili wasiniue au nipambane nao ili kulitunza kwa ajili ya vizazi vyao baadaye nao walikute Shamba.
Asanteni.