Wananchi zaidi ya 170 watozwa faini kwa kosa la kuuza na kununua bidhaa bila risiti

Donatila

JF-Expert Member
Oct 23, 2014
7,557
21,511
faini.jpg

Wananchi zaidi ya 170 wakiwemo wafanyabiashara waliokamatwa na mamlaka ya mapato nchini TRA mkoani Arusha kwa kosa la kuuza na kununua bidhaa bila kutoa risiti wametozwa faini ya zaidi ya milioni 900 na baadhi yao wameanza mchakato wa kulipa.

Wanachi hao ni wale waliokamatwa katika msako unaoendelea wa kukamata watu wanaouza na kununua bidhaa bila risiti unaofanywa na mamlaka ya mapato TRA mkoa wa Arusha.

Wakizungumzia hali hiyo wananchi hao licha ya kuomba kuwa wasamehewe kwani wamesahau,watendaji wa mamlaka hiyo wamesema zoezi linaendelea na wote wanatakaoendelea kukaidi agizo hilo watakamatwa.

Chanzo:
ITV
 
Serikali inatafuta mapato kwa njia ya faini faini tuu bidhaa zenyewe ziko wapi kwa hao wafanyabiashara mpaka mnatoza faini kila kukicha nendeni Zambia na SA hakuna ujinga huo cha msingi ni kusimamia kodi inapoingia na kutoa Elimu ya risiti na si kuwakomoa Wananchi Wakati kodi wanalipa bado mnabaki barabarani kuangalia risiti...
 
Tatizo la hii serikali ni kwamba inatumia 10 ili kukusanya 2. Hivi hao watu wanaozunguka kukamata wenzao wangepewa mashamba wakalime serikali si ingeingiza mara 100 zaidi?! Cha msingi ni kuhakikisha bidhaa inalipiwa kodi zote pale inapoingizwa nchini au inapozalishwa kiwandani palepale! Bidhaa isitoke bandarini au kiwandani bila kulipiwa kodi ZOTE! After all, wafanya biashara wote wa kati (secondary traders), ambao si waingizaji/wazalishaji wa bidhaa huwa wanaenda kudai warudishiwe pesa kutoka TRA kwa mizigo waliyonunua na mwisho wa siku kodi ambayo serikali inapata huwa inatoka kwa primary traders ambao ndio wazalishaji/ waagizaji wa bidhaa toka nje, VAT toka kwa wafanyabiashara wa kati huwa ni ndogo kulinganisha na hao wa primary. Hivyo serukali itafute mfumo wa kukusanya kodi zao zote bandarini na kwenye viwanda, hii inawezekana, iachane na kuwanyanyasa hawa distributors wa huku chini maana ni sawa na kutumia chambo cha sato mmoja ili kuvua dagaa mmoja, yaani mtu ana duka la mtaji wa laki tatuc halafu unamnunulisha mashine ya EFD kwa laki tisa kweli?!!!!! TUSIFANYE VITU KWA MAAZOEA, TUTUMIE AKILI!

Ni kama tulivyofanya kwenye road license, kutwa TRA walikuwa wanshinda mabarabarani kukagua road license, sasa hivi tunalipia moja kwa moja kwenye mafuta huko huko bandarini, yakiingia serikali inakua imeshavuta chake mapemaaa, wale mawakala wa TRA waliokua wanapoteza muda na kuota vitambi mabarabarani wapewe mashamba wakalime!
 
Safi sana TRA
Bila kodi taifa halitaweza kutimiza malengo yake, komaeni hivyo hivyo
 
Sasa ili swala lina ukakasi kidogo kuna wafanyabiashara apa kariakoo, wenyew ukinunua bidhaa wanakupa risiti ya sh 15.00 wakati bidhaa ni sh 150000
 
Sasa ili swala lina ukakasi kidogo kuna wafanyabiashara apa kariakoo, wenyew ukinunua bidhaa wanakupa risiti ya sh 15.00 wakati bidhaa ni sh 150000
Kwanini unaikubali hiyo risiti? Unatakiwa uikatae na kudai yote, vinginevyo wakurudishie pesa ukanunue kwingine unakotaka
 
Serikali ifanye ubunifu kama ilivyofanya kwenye kodi ya magari, usumbufu wote umeisha, kodi inalipwa lakini hatupati tena usumbufu
 
Safi sana TRA
Bila kodi taifa halitaweza kutimiza malengo yake, komaeni hivyo hivyo
Kodi zimeshindikana kulipika mnakimbilia kwenye faini!! Ambako mtu hata kubambikwa kosa ni rahisi?!!! Kuza uchumi. Biashara zifanyike ukusanye kodi za kutosha sasa, nchini biashara zimeporomoka, na ukusanyaji kodi lazima uwe mgumu kwani kodi inakusanywa kutokana na uzalishaji/mauzo.mauzo hamna kodi itakusanywa vipi ya kutosha ndio maana mnakimbilia kwenye notification za barabarani ambako watu wengi wana bambikwa makosa!! Nchi gani duniani inajisifia kwa kukusanya kiwango kikubwa cha faini za barabarani??? Kuza uchumi kusanya kodi
 
Tatizo la hii serikali ni kwamba inatumia 10 ili kukusanya 2. Hivi hao watu wanaozunguka kukamata wenzao wangepewa mashamba wakalime serikali si ingeingiza mara 100 zaidi?! Cha msingi ni kuhakikisha bidhaa inalipiwa kodi zote pale inapoingizwa nchini au inapozalishwa kiwandani palepale! Bidhaa isitoke bandarini au kiwandani bila kulipiwa kodi ZOTE! After all, wafanya biashara wote wa kati (secondary traders), ambao si waingizaji/wazalishaji wa bidhaa huwa wanaenda kudai warudishiwe pesa kutoka TRA kwa mizigo waliyonunua na mwisho wa siku kodi ambayo serikali inapata huwa inatoka kwa primary traders ambao ndio wazalishaji/ waagizaji wa bidhaa toka nje, VAT toka kwa wafanyabiashara wa kati huwa ni ndogo kulinganisha na hao wa primary. Hivyo serukali itafute mfumo wa kukusanya kodi zao zote bandarini na kwenye viwanda, hii inawezekana, iachane na kuwanyanyasa hawa distributors wa huku chini maana ni sawa na kutumia chambo cha sato mmoja ili kuvua dagaa mmoja, yaani mtu ana duka la mtaji wa laki tatuc halafu unamnunulisha mashine ya EFD kwa laki tisa kweli?!!!!! TUSIFANYE VITU KWA MAAZOEA, TUTUMIE AKILI!

Ni kama tulivyofanya kwenye road license, kutwa TRA walikuwa wanshinda mabarabarani kukagua road license, sasa hivi tunalipia moja kwa moja kwenye mafuta huko huko bandarini, yakiingia serikali inakua imeshavuta chake mapemaaa, wale mawakala wa TRA waliokua wanapoteza muda na kuota vitambi mabarabarani wapewe mashamba wakalime!
Mkuu pole sana nchi hii ina kodi nyingi yaani bidhaa moja kodi endelevu so usiwashangae TRA ni bunge ndio lilitunga huko bandarini kodi pia inalipwa kwa bidhaa hiyo hiyo na ikifika dukani ukainunua ni kodi mpya tena ndio hiyo wanayohangaika nayo si kwamba hiyo bidhaa haijalipiwa kodi na pia wewe ukainunua ukamuuzia mtu basi kodi pia serikali itataka hili ni tatizo kubwa wanatunga sheria na baadae ndio inakuwa sera ya uchaguzi ya kuifuta hiyo sheria na huziita kodi za Ajabu ajabu
 
Mkuu pole sana nchi hii ina kodi nyingi yaani bidhaa moja kodi endelevu so usiwashangae TRA ni bunge ndio lilitunga huko bandarini kodi pia inalipwa kwa bidhaa hiyo hiyo na ikifika dukani ukainunua ni kodi mpya tena ndio hiyo wanayohangaika nayo si kwamba hiyo bidhaa haijalipiwa kodi na pia wewe ukainunua ukamuuzia mtu basi kodi pia serikali itataka hili ni tatizo kubwa wanatunga sheria na baadae ndio inakuwa sera ya uchaguzi ya kuifuta hiyo sheria na huziita kodi za Ajabu ajabu
Yaaani ni 'TAX CHAIN' ya ajabu kabisa! Kwanini wasikate pesa yao immediately bidhaa inapozalishwa au kufika bandarini, waweke kodi kubwa wapendavyo, tutalipa, ila tuilipe yote pale pale bandarini au kiwandani yaishe, sio tuleteane kero kama zile za road license, ushenzi ushenzi tu!
 
Yaaani ni 'TAX CHAIN' ya ajabu kabisa! Kwanini wasikate pesa yao immediately bidhaa inapozalishwa au kufika bandarini, waweke kodi kubwa wapendavyo, tutalipa, ila tuilipe yote pale pale bandarini au kiwandani yaishe, sio tuleteane kero kama zile za road license, ushenzi ushenzi tu!
Kuna utata mwingi acha kodi ya mnunuzi mwenye mali Hataki kulipa ati bidhaa ikidoda itakuwa imekula kwake so ndio maana inasakwa kama hivo sasa isikwepwe
 
Kuna utata mwingi acha kodi ya mnunuzi mwenye mali Hataki kulipa ati bidhaa ikidoda itakuwa imekula kwake so ndio maana inasakwa kama hivo sasa isikwepwe
Kwani huko aliponunua si alilipa pesa? Sasa ikidoda si bado imekula kwake with or without tax?, au alipewa kwa mkopo ili ikidoda arudishe?
 
Back
Top Bottom