Wananchi wengi waiponda CHADEMA kwa kutokuwashirikisha baada ya uchaguzi...

eliesikia

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
787
755
Habari,
Utafiti uliopatikana hivi karibuni umefumbua yaliyofichwa... Wengi wamekuwa wakisikitika kwa CHADEMA kutoka bungeni bila kuwa na baraka za wananchi.. Mengi yameongelewa lakini wengi wamesema kitendo cha CHADEMA kutoka bungeni kimeonyesha kutokuwa na adabu kwa wananchi wao..

Wao wamesema wengi wao walitegemea CCM kuiba kura lakini walijitayarisha kuleta mgomo nchi nzima wakiaamini CHADEMA wangelisimamia hilo ili waliemtaka kwa kura awe kweli raisi.. .. Kwa kuwa huo ndio utaratibu mzuri kwa nchi za kiafrika ... Mpaka kiwake ndio kieleweke!!! Lakini CHADEMA hawakuamua kutenda yale waliyotegemea na woga walionyesha mkubwa saana hasa kwa jeshi la polisi licha ya wao wanachi kulinda kura siku zote za uchaguzi hadi matokeo...
Wengi wanaamini njia sahihi ni kutangaza kuigomea serikali kwa kila kitu ili haki itendeke lakini CHADEMA wameogopa kulifanya hili...
Pia wamelalamikia pia kutokushirikishwa kwenye kudai Katiba na tume huru ili hali CHADEMA wanadai wao wana NGUVU YA UMMMA... Sasa badala wawashirikishe wao ili waigomee serikali lakini wao wanaogopa matamko ya Said Mwema na jeshi la polisi...

Wamesikitika sana wengi wao wakidai kuwa HAKI HAIWEZI KUJA KWENYE KISAHANI... Sasa wanadai hatua watachukua wao wenyewe kama wananchi au wafanyakazi kuleta mgomo nchi nzima kwa kuwa aliechaguliwa si chaguo lao bali ni Ggabgo wa Tanzania.. Kajitangaza mwenyewe wala hakuna aliyempa kura....

Maamuzi magumu wanasubiria kutoka CHADEMA na wengi wanadai wako tayari kukaa barabarani ili mradi UFISADI na UFEDHULI ufikie ukomo japo CHADEMA wanageuza maneno kuwa hawatambui uchaguzi lakini Raisi wana...??? Sielewi kabisa... Mjadala huu hauwezi kufikia kama chakula kwenye kisahani ni lazima pawake moto ili kila mtu ajue kinachotusibu.....

Pamoja
SITAKI KUCHOCHEA LAKINI NAPENDA KUWASILISHA..
 
Tupe details za huo utafiti, taasisi gani ilifanya, lini, na akina nani walihojiwa. Kama ni REDET au Synovate pia utaje ili tupate kuelewa, ama sivyo twamuomba mods aiondoe hii topic ya kizushi.

After all suala la CDM kutoka bungeni lilishazungumzwa sana humu JF, sijui kwa nini unalileta tena.
 
Huo utafiti umefanyia wapi au chumbani, halafu toka Kikwete aibe kura ameshakushirikisha mara ngapi.
 
Tupe details za huo utafiti, taasisi gani ilifanya, lini, na akina nani walihojiwa. Kama ni REDET au Synovate pia utaje ili tupate kuelewa, ama sivyo twamuomba mods aiondoe hii topic ya kizushi.

After all suala la CDM kutoka bungeni lilishazungumzwa sana humu JF, sijui kwa nini unalileta tena.

hana jipya!
 
U hav stand to only one point (Chadema kutoka Bungeni) kati ya Tano nilizoainisha... Too saad!!!! Halafu kwa Tanzania utafiti lazima ufanywe na Taasisi moja tuu REDET na synovate??? Acha kukeremisha kabisa.... Hebu angalia hiyo thread vizuri kisha watumie akina-MOD meseji waifute... Sitaki kukufundisha kwa kuwa angekuwa mwalimu wako Azaveli basi angekuita bogasi.. japo sio vibaya kuelekezwa....
 
Buddy don't be a great whisper,be a great thinker. Lete chanzo na ripoti ya huo utafiti kujustify your thread.
 
Kaka Eliesikia!

Bila ajizi hebu tumwagie mautafiti hayo hapa tuyadadavue.
Halafu "wananchi wengi" maana yake nini???

Umezungumza CDM waligomea hotuba bila kuwa na baraka ya wananchi, kumbe hiyo baraka CDM wangeipata wapi zaidi sanduku la kura??
Au walitakiwa kina Slaa na wenzake waanze kampeni na kuomba ridhaa ya kuwalk out wakati JK anahutubia??

Am afraid to say your post should have been on Uhuru newspaper not in here kwa sababu haitupi kufikiri.
 
Chadema, viongozi si madikteta, hata wale "kumi" waliopinga wamewekwa kiti moto na wameamrishwa wasiongee tena na waandishi wa habari mpaka Mwenyekiti atavyo amuwa.

Kwenye udikteta na kuendesha chama kama unaendesha night club unategemea kushauriwa? Ni udikteta na maamuzi ya papo kwa papo kwenda mbele. Nawahurumia Chadema.
 
CDM wangewashirikisha vp wananchi maana hata mikutano yao nchi nzima imezuiwa na ccm. Mahakamani hawawezi kwenda kwa kuwa Katiba inakataza! Na huo utafiti nyanya unaodai kuwa "watu wengi wamesema" ulifanywa na nani?
 
Kaka Eliesikia!

Bila ajizi hebu tumwagie mautafiti hayo hapa tuyadadavue.
Halafu "wananchi wengi" maana yake nini???

Umezungumza CDM waligomea hotuba bila kuwa na baraka ya wananchi, kumbe hiyo baraka CDM wangeipata wapi zaidi sanduku la kura??
Au walitakiwa kina Slaa na wenzake waanze kampeni na kuomba ridhaa ya kuwalk out wakati JK anahutubia??

Am afraid to say your post should have been on Uhuru newspaper not in here kwa sababu haitupi kufikiri.

Uhuru wanaandika CCM wameiba kura???? Utafiti hata kitaaani ni utafiti... Lakini Uhuru huwa liandika HAKI INAKUJA KWENYE KISAHANI??
 
Mawazo yamtu mmoja hayawezi kuchukuliwa kama utafiti......Thread imekosa mashiko

Kumbe huna PhD ndio maana... wenzio pale faculty ya Political Science Harvard utafiti unafanywa hata na Undergraduate....
¨Thread imekosa mashiko¨, kweli uelewa wako unahitaji kalamu tena na miaka mitatu juuu
 
CDM wangewashirikisha vp wananchi maana hata mikutano yao nchi nzima imezuiwa na ccm. Mahakamani hawawezi kwenda kwa kuwa Katiba inakataza! Na huo utafiti nyanya unaodai kuwa "watu wengi wamesema" ulifanywa na nani?

CDM wangewashirikisha vp wananchi maana hata mikutano yao nchi nzima imezuiwa na ccm. .... Haki haiji kwenye kisahani na usifikiri kuna siku CCM watawapa hata nafasi ya kupumua kama hawajaanzisha Kamati ya kikatiba kabisa ili wawe masultani kabisa.... Lazima KIWAKE ili kieleweke
 
Buddy don't be a great whisper,be a great thinker. Lete chanzo na ripoti ya huo utafiti kujustify your thread.

Hivi kumbe hapa JF wengi hamjapata PhD ndio maana hamwamini kuwa utafiti hufanywa na mtu yeyote ili mradi anajua miiiko....
1. Wewe umeonaje kuhusu CHADEMA sasa hivi baada ya uchaguzi?? Jibu
2. Je umeridhika na matokeo??
3. Je uko tayari kusimamia ukweli unaouamini???
4. Je CHADEMA wamewashirikisha katika harajkati za kudai katiba na tume huru?
5. Unadhani ni hatua gani ungependa wachukue au uchukue??
Basi mimi nime-summarise tuu hapo
 
Back
Top Bottom