Wananchi wasitishe kufungua Fixed Deposit account

technically

JF-Expert Member
Jul 3, 2016
11,975
48,843
Kwa mjibu Wa Rais ni kuwa fixed deposit account ni mbaya na zinasababisha ufisadi kwa maafisa Wa Serikali na Bank .

Hivyo mwananchi akifungua anawapa ulaji watu Wa bank .

Si tumeamua kupambana na ufisadi nashauri watu waache kufungua deposit account chukueni pesa zenu wekeni kwenye vyama mbali mbali mtaani maana mkifungua deposit pesa zinaibiwa na maafisa Wa bank kwa mjibu Wa rais.

Kichekesho kwa serikali ni kuzifungia pesa BOT na wananchi zifungieni pesa zenu kwenye vyama .

Eti hoja ni kuwa serikali uenda uko bank kuzikopa kwa riba kubwa!!

Hivi serikali haijiulizi ni watu wangapi wana fixed deposit account bank lakini bado wanaendelea kukopa kwenye hizo hizo bank kufanya mambo mengine?

Hivi mtu kama Mengi anakosa kweli fixed account bank? Je ni kweli hawezi kukopa bank? Akiwa na hiyo fixed deposit account?...

Sana sana sasa hivi kitakachofuata ni kuongeza makato kimya kimya ya bank transaction ili kuwabebesha mzigo wateja Wa kuzinusuru bank zisife moja kwa moja..

Swali ni kwamba kwa nini huu mzigo ubebwe na mwananchi pekee huku serikali ikijiweka pembeni wakati ndio yenye pesa kuliko watu Wa kawaida?
 
Wewe technically ni mpuuzi sana. Fedha za makusanyo yalitolewa maelekezo zipelekwe moja kwa moja BOT. Watu wakawekeza kinyume na maelekezo hayo. Kuweka deposit kwa MTU anayetafuta faida ya kibiashara ni sawa. Lakini kwa kesi hii ni tofauti! Ni utovu wa Nidhamu ulifanyika kupuuza maelekezo halali ya Rais. Ni sawa na wewe unapopuuza masharti aliyokupa baba yako lazima utandikwe bakora!!
 
Mmmmmmmh!!!!!! Thread zingine kwa kweli pasua kichwa. Waweza kurupuka kuichangia ukajikuta umeenda nje ya mada na maudhui halisi.

Hizo fixed accounts zenyewe tunazifungua kwa hela ipi mkuu, tarehe 30 ya sasa haina excess kabisaaa
 
Kwa mjibu Wa Rais ni kuwa fixed deposit account ni mbaya na zinasababisha ufisadi kwa maafisa Wa Serikali na Bank .

Hivyo mwananchi akifungua anawapa ulaji watu Wa bank .

Si tumeamua kupambana na ufisadi nashauri watu waache kufungua deposit account chukueni pesa zenu wekeni kwenye vyama mbali mbali mtaani maana mkifungua deposit pesa zinaibiwa na maafisa Wa bank kwa mjibu Wa rais.

Kichekesho kwa serikali ni kuzifungia pesa BOT na wananchi zifungieni pesa zenu kwenye vyama .

Eti hoja ni kuwa serikali uenda uko bank kuzikopa kwa riba kubwa!!

Hivi serikali haijiulizi ni watu wangapi wana fixed deposit account bank lakini bado wanaendelea kukopa kwenye hizo hizo bank kufanya mambo mengine?

Hivi mtu kama Mengi anakosa kweli fixed account bank? Je ni kweli hawezi kukopa bank? Akiwa na hiyo fixed deposit account?...

Sana sana sasa hivi kitakachofuata ni kuongeza makato kimya kimya ya bank transaction ili kuwabebesha mzigo wateja Wa kuzinusuru bank zisife moja kwa moja..

Swali ni kwamba kwa nini huu mzigo ubebwe na mwananchi pekee huku serikali ikijiweka pembeni wakati ndio yenye pesa kuliko watu Wa kawaida?

Mengi hana fixed account heka zake ziko Treasury Bills. Sijui unaongea mzigo upi kwa sababu mabenki yote yakipata hizo fixed deposits (yanalipia 5%) pale pale yanazihamishia Benki Kuu kununua Treasury Bills (serkali inalipa 19%). Huoni kuwa taasisi ya umma kuweka hela zake fixed deposits ni ufisadi wa kutisha? Si Rais alisema benki humpa chochotekitu huyo Chief Executive, hukusikia?
 
Back
Top Bottom