Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Wananchi wasiburuzwe kudai Katiba mpya -Shivji
Thursday, 09 December 2010 19:59 newsroom
NA SELINA WILSON
BAADHI ya wanasiasa wanadaiwa kuwaburuza wananchi katika madai ya Katiba mpya, imeelezwa. Wanasiasa hao wametakiwa kuwaacha wananchi kupitia mijadala waamue wenyewe kuhusu mabadiliko ya Katiba ya nchi. Imeelezwa wanasiasa hao wanapaswa kuelekeza nguvu katika kujenga uchumi imara, ili taifa liweze kujitegemea. Profesa Issa Shivji, ambaye ni mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amesema baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanafikiri Katiba mpya ndiyo mahali pa kuanzia katika kuleta mabadiliko, lakini jambo la muhimu ni kujenga Tanzania mpya. Alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari katika Kigoda cha Mwalimu Nyerere, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya Uhuru. Pia alizindua kitabu chake cha Cheche.
ìWanasiasa wanataka hatua za haraka kuwaburuza wananchi kutaka Katiba mpya, kinachohitajika ni Katiba mpya ambayo wananchi wenyewe wataamua iweje kupitia mjadala,î alisema. Profesa Shivji aliyebobea katika masuala ya kisiasa na kijamii alisema mwaka 1961 Tanzania ilipopata Uhuru ilikuwa ni hatua ya kwanza. Alisema hatua ya pili ilikuwa kuwezesha uhuru wa wananchi katika ngazi ya jamii, ili wajenge uwezo wa kujiamulia mambo yao wenyewe, jambo alilosema bado halijafikiwa. Profesa Shivji alisema mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi vya siasa ulipoanzishwa, wananchi waliburuzwa na kuingia bila kujua nini cha kufanya. ìIlitakiwa wananchi wapewe hata miaka miwili kuamua juu ya mfumo huo,î alisema Profesa Shivji.
Naye Profesa Karim Hirj wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi za Tiba Muhimbili (MUHAS), alisema viongozi wanapaswa kujikita katika kuboresha sekta za madini na utalii, ili mapato yake yaweze kuinufaisha nchi kupiga hatua kimaendeleo. Alisema hoja ya kubadilisha Katiba si jambo muhimu, kwani Watanzania wanahitaji mabadiliko katika nyanja ya uchumi ili wanufaike na matunda ya rasilimali zilizopo nchi. ìMabadiliko ya Katiba yana umuhimu wake lakini jambo kubwa linalopaswa kutiliwa mkazo ni kuboresha uchumi, tunufaike na mazao ya sekta za madini na utalii,î alisema. Kumekuwa na malumbano miongoni mwa wanasiasa kuhusu mabadiliko ya Katiba, baadhi ya vyama, ikiwemo CHADEMA ikishinikiza wananchi kudai Katiba ya nchi ibadilishwe.
Akizungumzia kitabu cha Chehe, ambacho amekihariri, Profesa Hirj alisema kinatoa historia ya mambo yaliyotokea miaka iliyopita baada ya Uhuru, likiwemo jarida la Chehe lililokuwa likiandaliwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kabla ya kupigwa marufuku kutokana na kukemea ubepari.
Kitabu hicho kilizinduliwa na Mwenyekiti wa Jumuia ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), Dk. Adolf Kibogoya. Wasomi wengine walipata fursa ya kukifanyia mapitio kitabu hicho.
Thursday, 09 December 2010 19:59 newsroom
NA SELINA WILSON
BAADHI ya wanasiasa wanadaiwa kuwaburuza wananchi katika madai ya Katiba mpya, imeelezwa. Wanasiasa hao wametakiwa kuwaacha wananchi kupitia mijadala waamue wenyewe kuhusu mabadiliko ya Katiba ya nchi. Imeelezwa wanasiasa hao wanapaswa kuelekeza nguvu katika kujenga uchumi imara, ili taifa liweze kujitegemea. Profesa Issa Shivji, ambaye ni mhadhiri mstaafu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, amesema baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanafikiri Katiba mpya ndiyo mahali pa kuanzia katika kuleta mabadiliko, lakini jambo la muhimu ni kujenga Tanzania mpya. Alisema hayo jana alipozungumza na waandishi wa habari katika Kigoda cha Mwalimu Nyerere, ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya miaka 49 ya Uhuru. Pia alizindua kitabu chake cha Cheche.
ìWanasiasa wanataka hatua za haraka kuwaburuza wananchi kutaka Katiba mpya, kinachohitajika ni Katiba mpya ambayo wananchi wenyewe wataamua iweje kupitia mjadala,î alisema. Profesa Shivji aliyebobea katika masuala ya kisiasa na kijamii alisema mwaka 1961 Tanzania ilipopata Uhuru ilikuwa ni hatua ya kwanza. Alisema hatua ya pili ilikuwa kuwezesha uhuru wa wananchi katika ngazi ya jamii, ili wajenge uwezo wa kujiamulia mambo yao wenyewe, jambo alilosema bado halijafikiwa. Profesa Shivji alisema mwaka 1992 mfumo wa vyama vingi vya siasa ulipoanzishwa, wananchi waliburuzwa na kuingia bila kujua nini cha kufanya. ìIlitakiwa wananchi wapewe hata miaka miwili kuamua juu ya mfumo huo,î alisema Profesa Shivji.
Naye Profesa Karim Hirj wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi za Tiba Muhimbili (MUHAS), alisema viongozi wanapaswa kujikita katika kuboresha sekta za madini na utalii, ili mapato yake yaweze kuinufaisha nchi kupiga hatua kimaendeleo. Alisema hoja ya kubadilisha Katiba si jambo muhimu, kwani Watanzania wanahitaji mabadiliko katika nyanja ya uchumi ili wanufaike na matunda ya rasilimali zilizopo nchi. ìMabadiliko ya Katiba yana umuhimu wake lakini jambo kubwa linalopaswa kutiliwa mkazo ni kuboresha uchumi, tunufaike na mazao ya sekta za madini na utalii,î alisema. Kumekuwa na malumbano miongoni mwa wanasiasa kuhusu mabadiliko ya Katiba, baadhi ya vyama, ikiwemo CHADEMA ikishinikiza wananchi kudai Katiba ya nchi ibadilishwe.
Akizungumzia kitabu cha Chehe, ambacho amekihariri, Profesa Hirj alisema kinatoa historia ya mambo yaliyotokea miaka iliyopita baada ya Uhuru, likiwemo jarida la Chehe lililokuwa likiandaliwa na wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kabla ya kupigwa marufuku kutokana na kukemea ubepari.
Kitabu hicho kilizinduliwa na Mwenyekiti wa Jumuia ya Wanataaluma wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDASA), Dk. Adolf Kibogoya. Wasomi wengine walipata fursa ya kukifanyia mapitio kitabu hicho.