Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,886
- 6,883
Wananchi wanaohudhiria Tamasha la 10 la Jinsia, wamependekeza utaratibu wa kupata wabunge kupitia majimbo , viti maalum na kuteuliwa na Rais ufutwe, na badala yake zianzishwe wilaya zisizozidi 150 ambazo zitakuwa ndiyo majimbo ya uchaguzi.
Washiriki zaidi ya 100 kwenye tamasha kutoka mikoa mbali mbali waliohudhuria warsha ambayo jana iliangalia katiba inavyopaswa kulinda haki za uchumi, usawa na usalama wa jamii katika maazimio yao, walisema katika utaratibu wa sasa Bunge linakuwa na wabunge wengi bila kuzingatia ufanisi na usawa kati ya wanawake na wanaume na makundi maalum wakiwepo walemavu.
Wamesema kwa sasa ambapo kuna wabunge zaidi ya 300, fedha nyingi za taifa zinapotea kwa ajili ya kuwalipa wabunge ambapo baadhi yao hawana ufanisi wowote katika kuendeleza ustawi wa jamii. "Tunataka Bunge la Jamhuri lenye watu wasiozidi 150, nusu wakiwa ni wanawake na nusu wanaume waliochaguliwa na wananchi kutoka kwenye wilaya Tanzania Bara na Visiwani," alipendekeza Peter Nalopori, kutoka Mkoa wa Kagera na kuungwa mkono na washiriki. Kadhalika washiriki wengine 39 waliozungumza na kuungwa mkono na wenzao walisema Katiba Mpya inapaswa izuie mbunge kupewa uwaziri na kwamba idadi ya wizara iwekwe kwenye katiba ili fedha za umma zielekezwe zaidi kwenye shughuli za maendeleo ya wananchi badala ya kuhudumia idadi kubwa ya mawaziri.
Wametaka pia Katiba Mpya iweke ukomo wa muda wa mtu kuwa mbunge kuwa ni vipindi viwili vya miaka mitano na kwamba mtu akishafikia umri wa miaka 70 katiba mpya ikataze kuwa asipewe kazi hiyo ya utumishi wa umma badala yake aachwe apunzike na kubaki kuwa mashauri wa taifa.
Kuhusu Spika, wametaka Katiba Mpya ibadilishe utaratibu wa kumpata Spika wa bunge ili asiwe mbunge na mwanachama wa chama chochote cha siasa.
Kuhusu uongozi wa wilaya na mikoa, wananchi hao wamependekeza kuwa Katiba Mpya iwe na kipengeke kinachowapa wananchi mamlaka ya kuwachagua wakuu wao wa wilaya na mikoa.
Katika ngazi za vijiji wamependekeza kuwa viongozi wake wawe ni wale wenye sifa ikiwa ni pamoja na elimu na kwamba katiba mpya iweke bayana kuwa mtu asiye na elimu ya sekondari hana sifa ya kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi.
Ili kuimarisha haki na usawa kwa wananchi wote kwenye elimu, wamependekeza kuwa Katiba Mpya iweke wazi kuwa kila mwananchi atapata elimu hadi chuo kikuu. "Tuna rasilimali nyingi za nchi zinazotumika vibaya, zikielekezwa kwenye elimu kila mtoto wa taifa hili anaweza kusoma bure hadi chuo kikuu", alisema Andres Njau.
Kuhusu madaraka ya Rais, walipendekeza kuwa Katiba Mpya impunguzie Rais madaraka ikiwa ni pamoja na yale ya kuteua majaji na viongozi wa Tume ya Uchaguzi badala yake viwekwe vyombo huru ambavyo vitapewa madaraka ya kuteua watu hao kwa kuzingatia vigezo .
Kuhusu haki za kijamii na kiuchumi wamependekeza vipendele maalum viwekwe kwenye katiba mpya vinavyoahinisha haki za wananchi katika masuala ya afya, ajira, usalama na haki lugha ya alama kwa walemavu wasioona kutambulika kitaifa na kwamba katiba iweke kipengele ambapo kitaunda chombo cha kufuatilia utekelezaji wa katiba mpya. Wananchi hao walitoa mapendekezo hayo baada ya watoa mada za uchokozi Magdalena Mkolere na na Annmarie Mavenjina kutoka FemAct kueleza jinsi ambavyo katiba na sheria za sasa hapa nchi zisivyokidhi haki za kiuchumi na kijamii.
IPPMedia
Washiriki zaidi ya 100 kwenye tamasha kutoka mikoa mbali mbali waliohudhuria warsha ambayo jana iliangalia katiba inavyopaswa kulinda haki za uchumi, usawa na usalama wa jamii katika maazimio yao, walisema katika utaratibu wa sasa Bunge linakuwa na wabunge wengi bila kuzingatia ufanisi na usawa kati ya wanawake na wanaume na makundi maalum wakiwepo walemavu.
Wamesema kwa sasa ambapo kuna wabunge zaidi ya 300, fedha nyingi za taifa zinapotea kwa ajili ya kuwalipa wabunge ambapo baadhi yao hawana ufanisi wowote katika kuendeleza ustawi wa jamii. "Tunataka Bunge la Jamhuri lenye watu wasiozidi 150, nusu wakiwa ni wanawake na nusu wanaume waliochaguliwa na wananchi kutoka kwenye wilaya Tanzania Bara na Visiwani," alipendekeza Peter Nalopori, kutoka Mkoa wa Kagera na kuungwa mkono na washiriki. Kadhalika washiriki wengine 39 waliozungumza na kuungwa mkono na wenzao walisema Katiba Mpya inapaswa izuie mbunge kupewa uwaziri na kwamba idadi ya wizara iwekwe kwenye katiba ili fedha za umma zielekezwe zaidi kwenye shughuli za maendeleo ya wananchi badala ya kuhudumia idadi kubwa ya mawaziri.
Wametaka pia Katiba Mpya iweke ukomo wa muda wa mtu kuwa mbunge kuwa ni vipindi viwili vya miaka mitano na kwamba mtu akishafikia umri wa miaka 70 katiba mpya ikataze kuwa asipewe kazi hiyo ya utumishi wa umma badala yake aachwe apunzike na kubaki kuwa mashauri wa taifa.
Kuhusu Spika, wametaka Katiba Mpya ibadilishe utaratibu wa kumpata Spika wa bunge ili asiwe mbunge na mwanachama wa chama chochote cha siasa.
Kuhusu uongozi wa wilaya na mikoa, wananchi hao wamependekeza kuwa Katiba Mpya iwe na kipengeke kinachowapa wananchi mamlaka ya kuwachagua wakuu wao wa wilaya na mikoa.
Katika ngazi za vijiji wamependekeza kuwa viongozi wake wawe ni wale wenye sifa ikiwa ni pamoja na elimu na kwamba katiba mpya iweke bayana kuwa mtu asiye na elimu ya sekondari hana sifa ya kuwa hata mjumbe wa nyumba kumi.
Ili kuimarisha haki na usawa kwa wananchi wote kwenye elimu, wamependekeza kuwa Katiba Mpya iweke wazi kuwa kila mwananchi atapata elimu hadi chuo kikuu. "Tuna rasilimali nyingi za nchi zinazotumika vibaya, zikielekezwa kwenye elimu kila mtoto wa taifa hili anaweza kusoma bure hadi chuo kikuu", alisema Andres Njau.
Kuhusu madaraka ya Rais, walipendekeza kuwa Katiba Mpya impunguzie Rais madaraka ikiwa ni pamoja na yale ya kuteua majaji na viongozi wa Tume ya Uchaguzi badala yake viwekwe vyombo huru ambavyo vitapewa madaraka ya kuteua watu hao kwa kuzingatia vigezo .
Kuhusu haki za kijamii na kiuchumi wamependekeza vipendele maalum viwekwe kwenye katiba mpya vinavyoahinisha haki za wananchi katika masuala ya afya, ajira, usalama na haki lugha ya alama kwa walemavu wasioona kutambulika kitaifa na kwamba katiba iweke kipengele ambapo kitaunda chombo cha kufuatilia utekelezaji wa katiba mpya. Wananchi hao walitoa mapendekezo hayo baada ya watoa mada za uchokozi Magdalena Mkolere na na Annmarie Mavenjina kutoka FemAct kueleza jinsi ambavyo katiba na sheria za sasa hapa nchi zisivyokidhi haki za kiuchumi na kijamii.
IPPMedia