Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Kuna madai ambayo tulianza kuyasikia siku ya J'pili wakati waupigaji kura kuwa watu walikuwa wanakataliwa kupiga kura kwa sababu mbalimbali. Na baadaye madai haya yametolewa na pande zote mbili hasimu (Katibu Mkuu Mukama kwa upande wa CCM, na Mwenyekiti Mbowe kwa upande wa CDM).
Natumaini wote hawa wana ushahidi wa madai haya; binafsi ningependa kujua tu je vyama hivi vilifanya utaratibu wa kufuatilia na kujua wale waliokataliwa kupiga kura ni kina nani na sababu za kukataliwa ni zipi na kwa kufanya hivyo kuweza kujua kwa kiasi fulani idadi ya watu waliokataliwa kupiga kura kwenye jimbo hilo.
Kuna mtu ana namba isije kuwa ni idadi ambayo ni negligible - isingeweza kubadilisha matokeo. Kwa mfano (kama ni watu 100 kwenye jimbo zima hata kama wote wangeruhusiwa kupiga kura na wote wangeipigia CDM bado matokeo yasingebadilika).
Sidhani kama kwenda baada ya uchaguzi kuuliza watu kama walikataliwa yaweza kuwa njia sahihi ya kujua kilichotokea siku ya uchaguzi. Ni matumaini yangu CDM walifanya utaratibu wa kuorodhesha watu waliokataliwa kupiga kura kwenye vituo mbalimbali siku ya Jumapili mbili ya Oktoba.
Natumaini wote hawa wana ushahidi wa madai haya; binafsi ningependa kujua tu je vyama hivi vilifanya utaratibu wa kufuatilia na kujua wale waliokataliwa kupiga kura ni kina nani na sababu za kukataliwa ni zipi na kwa kufanya hivyo kuweza kujua kwa kiasi fulani idadi ya watu waliokataliwa kupiga kura kwenye jimbo hilo.
Kuna mtu ana namba isije kuwa ni idadi ambayo ni negligible - isingeweza kubadilisha matokeo. Kwa mfano (kama ni watu 100 kwenye jimbo zima hata kama wote wangeruhusiwa kupiga kura na wote wangeipigia CDM bado matokeo yasingebadilika).
Sidhani kama kwenda baada ya uchaguzi kuuliza watu kama walikataliwa yaweza kuwa njia sahihi ya kujua kilichotokea siku ya uchaguzi. Ni matumaini yangu CDM walifanya utaratibu wa kuorodhesha watu waliokataliwa kupiga kura kwenye vituo mbalimbali siku ya Jumapili mbili ya Oktoba.