Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Idd Azan amethibitisha namna CCM imajaa wabunge vihiyo.
Majira, Gazeti Huru la Kila Siku, inaripoti kuwa katika maeneo fulani Jijini Dar Es Salaam Mbunge wa Kinindoni, Idd Azan alikutana na genge la wafuasi wa CUF wakimsindikiza Diwani wa Kata yao.
Wakiwa kwenye msafara huo kwa kutumia TZ11 zao, walikutana na Idd Azan, wakapaza sauti kuomba maji. Kwa ujuha, ama ukihiyo, ama pupa, ama sifa, mzee mzima aliingia mfukoni akachomoa Tshs. 50,000 ili vijana wa CUF wanunue maji ya kunywa.
Kumbe jamaa walikuwa wanataka miundombinu ya maji, na si fedha.
Wakachomoa.
Wakamrudishia mpunga wake.
Ikawa aibu funga-mwaka kwa Idd Azan.
Source: Majira
Majira, Gazeti Huru la Kila Siku, inaripoti kuwa katika maeneo fulani Jijini Dar Es Salaam Mbunge wa Kinindoni, Idd Azan alikutana na genge la wafuasi wa CUF wakimsindikiza Diwani wa Kata yao.
Wakiwa kwenye msafara huo kwa kutumia TZ11 zao, walikutana na Idd Azan, wakapaza sauti kuomba maji. Kwa ujuha, ama ukihiyo, ama pupa, ama sifa, mzee mzima aliingia mfukoni akachomoa Tshs. 50,000 ili vijana wa CUF wanunue maji ya kunywa.
Kumbe jamaa walikuwa wanataka miundombinu ya maji, na si fedha.
Wakachomoa.
Wakamrudishia mpunga wake.
Ikawa aibu funga-mwaka kwa Idd Azan.
Source: Majira