Wananchi wamkataa Waziri Karamagi

Keil

JF-Expert Member
Jul 2, 2007
2,214
803
Wananchi wamkataa Waziri Karamagi

* Wasema hajatekeleza ahadi zake kwao


Na Stella Ibengwe, Geita

WANANCHI wa wilaya ya Geita mkoani Mwanza, wamemkataa Waziri wa Nishati na Madini Bw. Nazir Karamagi, kwa madai kuwa yeye ndiye chanzo cha migogoro kati ya wawekezaji na wananchi wa maeneo ya migodi.

Hatua hiyo ya wananchi inafuatia ahadi za Waziri kutotekelezwa kwa muda mrefu na kuwafanya wananchi kuendelea kudhulumiwa haki zao bila kupata muafaka kutoka serikalini, kupitia wizara hiyo.

Wakizungumza jana wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika viwanja vya Kalangalala wilayani humo, wananchi hao waliitaka Kamati ya Kuchunguza Mikataba ya Madini na kupitia sheria za madini chini ya uenyekiti wa Jaji Mark Bomani, kumfikishia taarifa Rais kuwa hawamtaki Waziri Karamagi.

Waliiambia Kamati hiyo kuwa iwapo Rais hatalifanyia kazi suala hilo, kuna matatizo makubwa ambayo yanaweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na wananchi kujichukulia sheria mkononi kutokana na kuchoshwa na ahadi zisizofanyiwa kazi huku wakiendelea kuumia.

“Hatumtaki Waziri wa Nishati na Madini Karamagi, alishafika hapa Geita na akaambiwa matatizo yetu akaahidi kuyafanyia kazi, lakini mpaka leo hakuna alichotekeleza, unatarajia tuendelee kuwa na kiongozi wa aina hiyo, hatufai sisi kwani hajali matatizo yetu, tunaiagiza Kamati hii imfikishie taarifa Rais kuwa hatumtaki Waziri huyo,” alisema mmoja wa wananchi hao, Bw. Lameck Petro, kwa niaba ya wananchi hao.

Waliitaka Serikali kujali maoni ya wabunge yanayotolewa wakati wa vikao vya Bunge kwani wao ndio wawakilishi wa wananchi na waliwachagua kwa kuwa na imani nao kwamba wanaweza kutetea haki zao katika majimbo wanayotoka.

Aidha, wananchi hao walisema ni aibu kwa nchi kama Tanzania, kwenda kuomba msaada Ulaya, wakati wana utajiri mkubwa wa madini wanaowapa Wazungu kuchimba na kuwaachia mashimo "watoto na wajukuu wetu ambao watakuja kutuuliza haya mashimo ni ya nini sijui tutawajibu nini?".

Walisema viongozi wa Sekta ya Madini hawako makini na ndicho chanzo cha chimbuko la matatizo yote ya migodini na kudai kuwa ukweli wa mbunge wa Kigoma Kaskazini, Bw. Zitto Kabwe, umesababisha kuundwa kwa kamati hiyo huku wakihoji kati ya Serikali na Zitto nani ni mkweli.

Akipokea malalamiko, mapendekezo, maoni na ushauri kutoka kwa wananchi hao, Jaji Bomani alisema pengine matatizo hayo yalikuwa hayamfikii Rais ambapo aliahidi kuyafikisha na kuwahakikishia kuwa yatafanyiwa kazi huku akiwaambia Kamati haikuja kutembea bali kufanya kazi.

Source: Majira
 
Hooray! Watanzania hatimaye waamka katika usingizi mzito. Hakuna wa kutuchezea tena na usanii usiokwisha, ufisadi, uroho wa utajiri kwa kutumia nyadhifa tulizowakabidhi na kusaini mikataba feki isiyotunufaisha.

Mtu angeniambia kwamba kuna siku utasikia Watanzania wanatamka kwamba hawamtaki Waziri kwa sababu yeye ndiye chanzo cha matatizo yanayowakabili, ningebishana naye mpaka asubuhi...:) lakini sasa Watanzania kweli wamechoka. Nimesikia raha sana kusoma hii article maana sasa najua kwamba ukombozi wa kweli wa Watanzania uko njiani.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Mtu angeniambia kwamba kuna siku utasikia Watanzania wanatamka kwamba hawamtaki Waziri kwa sababu yeye ndiye chanzo cha matatizo yanayowakabili, ningebishana naye mpaka asubuhi...:) lakini sasa Watanzania kweli wamechoka. Nimesikia raha sana kusoma hii article maana sasa najua kwamba ukombozi wa kweli wa Watanzania uko njiani.
Bubu, haya ni matokeo ya tabu na shida, natamani maisha yaendelee kuwa magumu zaidi na zaidi (Shida ndio shule pekee kwa Watz).

Hili ni fundisho kuwa Tanzania ingekuwa nzuri sana kama tusingetegemea kabisa misaada ya hao wafadhili maana ndio tungetia akili.
 
Bado watanzania wamezoea shida hao wanaopiga kelele Karamagi akiwapa elfu hamsini hamisini kila mmoja akagombea ubunge kwenye jimbo hilo hujue atapata tu.
 
Bubu, haya ni matokeo ya tabu na shida, natamani maisha yaendelee kuwa magumu zaidi na zaidi (Shida ndio shule pekee kwa Watz).

Hili ni fundisho kuwa Tanzania ingekuwa nzuri sana kama tusingetegemea kabisa misaada ya hao wafadhili maana ndio tungetia akili.



Not to be easily confused with sadism, this is an ironic, counter intuitive and unorthodox observation that has more sense than common sense.
 
Hali hii imetokana na ahadi nyingi ambazo ziliwafanya wananchi wawe na matumaini ya kuwa na maisha bora lakini ghafla hali inabadilika na kuwa ngumu zaidi na viongozi wetu wanashindwa kusoma alama za nyakati na kuendelea kudhani wananchi bado wamelala.
Mfano mzuri ni issue ya Bot wakati serekali inaambiwa mabilioni yanachotwa eti wanaendeleza ubishi kwamba hakuna kitu kibaya kinaendelea pale bot na sasa ukweli omejionyesha sasa wamenywea kimya na hasa wabunge wetu ambao wanaendekeza itikadi za kisiasa na kusahau kilichowapeleka bungeni.
 
Pamoja na kuwa mfisadi nadhani huyu jamaa ana damu ya kunguni pia.

Maana kila anapopitia ni lazima lawama ziwepo. Hata huko TICTS ni lawama tuu!
 
Bado watanzania wamezoea shida hao wanaopiga kelele Karamagi akiwapa elfu hamsini hamisini kila mmoja akagombea ubunge kwenye jimbo hilo hujue atapata tu.

I am afraid i agree with above observation. Just think how stupi we are, people have stolen stollen bilions of our money so as we can vote for them( and that is what we did), and today we are pretending to say otherwise. I will not be suprised kuwa serikali ya sasa baadaye itashinda tena, pamoja na madudu yaliyoibuliwa sasa, sitashangaa vilevile kuona kuwa hakuna kati ya hao wanaouhusika wakichukuliwa hatua kali!
 
Pamoja na kuwa mfisadi nadhani huyu jamaa ana damu ya kunguni pia.

Maana kila anapopitia ni lazima lawama ziwepo. Hata huko TICTS ni lawama tuu!

Mheshimiwa Mfwatiliaji,
Hiyo siyo "Damu ya Kunguni" aliyo nayo jamaa, hapana!
Hiyo ndiyo hatima na matokeo halisi ya ubabaishaji alio nao waziri wetu huyu katika utendaji kazi wake, ndio maana kila mahali anajikuta anapwaya. Kila atakachogusa anajikuta kakosolewa na kulaumiwa. Angekuwa katulia na kufanya mambo yake kwa mujibu wa taratibu zinazotakikana nadhani asingekutana na haya yanayomkuta. Aache kupita njia za mkato. "Short cut is always a wrong cut"
 
Back
Top Bottom