Wananchi wafurika Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi Wilaya ya Chato kumuona Nyoka wa ajabu

Dr. Wansegamila

JF-Expert Member
Feb 3, 2012
2,856
7,846
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Geita wamepiga kambi katika pori llililopo Kitongoji cha Iseni Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi Wilaya ya Chato Mkoani humo baada ya kudaiwa kuwepo kwa nyoka aina ya chatu mwenye maajabu huku wengine wakionekana kuchota Baraka kutoka kwa nyoka huyo kwa kufanya matambiko.


















======

UPDATES;

Chatu Aliyeonekana Chato Achukuliwa

September 11, 2019

NYOKA mkubwa aina ya chatu ambaye hivi karibuni alizua gumzo baada ya kuonekana Kitongoji cha Iseni, Kijiji cha Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi wilayani Chato Mkoani Geita amechukuliwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (Tawa) na kumpeleka pori la akiba la Kigosi Mulowosi, lililopo wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
1568374243165.png

Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Richard Bagolele amesema nyoka huyo anapelekwa pori la akiba la Kigosi kwa ajili ya kuhifadhiwa.

Nyoka huyo aliyeanza kuonekana siku saba zilizopita aligeuka kivutio kwa wananchi waliodai kuwa ni baraka, wengi kushinda porini wakimtazama huku wakiwa na mbuzi, maji na unga na vyakula wakiamini endapo nyoka atakula watapata baraka ya mvua, kuongezeka kwa mavuno na kuondoa mikosi kijijini hapo hivyo kuwaletea mafanikio.
1568374272447.png

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel amewataka wanakijiji wa kijiji cha Makurugusi waliokuwa wamepiga kambi porini wakisubiri maajabu ya nyoka huyo, wafanye kazi kwa bidii na kuachana na imani potofu za kupata baraka kwa matambiko na kuabudu nyoka na vitu vingine.

Na Edwin Lindege
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Geita wamepiga kambi katika poli llililopo Kitongoji cha Iseni Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi Wilaya ya Chato Mkoani humo baada ya kudaiwa kuwepo kwa nyoka aina ya chatu mwenye maajabu huku wengine wakionekana kuchota Baraka kutoka kwa nyoka huyo kwa kufanya matambiko.




Duh yaani tuna kazi kubwa kufikia ustarabu!
 
Watu wa kanda hiyo wana imani za kijinga sana, mpaka wasomi hawana tofauti na wasiosoma
Katiba imetoa uhuru wa kuabudu chochotee.Waziri lugora hao wanaosali hapo hiyo dini umeisajili ?maana wewe siku hizi umegeuka msajili wa dini na miungu wakati serikali haina dini.Yule nabii uliyemkamata kisa kanisa lake anaposalia halijasajiliwa mwachie.Kazi ya wizara Ni kusajili NGO Sio dini.Ziko NGo zenye Mashule ,mahospitali nk hizo ndizo usajili Sio dini.Ona Sasa hao wanaabudu nyoka wao nenda kawakamate kwa kuabudu bila kusajiliwa wizara ya Mambo ya ndani.Haya hao waabuduo wa chato kawakamate Kama ulivyokamata nabii wetu kuwa anasalisha bila kanisa lake kusajiliwa.Nilikuambia kukamata nabii SI kitu Cha mchezo .Kawakamate na hao.Huyo mzee padri wao mkamate Kama ulivyomkamata nabii wetu
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Geita wamepiga kambi katika pori llililopo Kitongoji cha Iseni Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi Wilaya ya Chato Mkoani humo baada ya kudaiwa kuwepo kwa nyoka aina ya chatu mwenye maajabu huku wengine wakionekana kuchota Baraka kutoka kwa nyoka huyo kwa kufanya matambiko.
View attachment 1203478
Wajinga ndiyo waliwao.
 
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wananchi kutoka maeneo mbalimbali ndani na nje ya Mkoa wa Geita wamepiga kambi katika pori llililopo Kitongoji cha Iseni Kijiji cha Kasala Kata ya Makurugusi Wilaya ya Chato Mkoani humo baada ya kudaiwa kuwepo kwa nyoka aina ya chatu mwenye maajabu huku wengine wakionekana kuchota Baraka kutoka kwa nyoka huyo kwa kufanya matambiko.
View attachment 1203478


Aisee kuna watu wana lafudhi mbaya
 
Back
Top Bottom