Wananchi waelewe kujengewa miundombinu sio hisani bali ni wajibu wa Serikali yoyote iliyoko madarakani

Areus

JF-Expert Member
Jul 27, 2016
324
403
Kama kichwa cha habari kinavyojieleza hapo juu. Wananchi waelewe kuwa kujengewa miundombinu,kupewa huduma za jamii sio hisani ya serikali ila Ni wajibu wa serikali yoyote ile duniani. Hilo tuliweke sawa.

Pesa zote zinazopelekwa kwenye shughuli za miradi ya Maendeleo ni kodi za wananchi wenyewe wala hazitoki mfukoni mwa mzalendo yeyote. Kwahyo serikali yoyote haina haki ya kuwabagua watu kwa misingi ya vyama vyao kwamba sehemu fulani kuna wananchi wa upinzani na hawezi kupelekewa maendeleo.zana hii ni mbovu na sio nzuri kutumia kwenye kampeni. Ni harufu mbaya ya kuligawa Taifa.

Kwahyo ni vema wanasiasa wakaeleza watawafanyia nini wanachi ila sio kuwatisha.

MAENDELEO HAYANA VYAMA
 
Jiwe kutwa kuwatisha watu, et mkichagua upinzani mm sileti maendeleo hapa! Kauli za kibaguzi kabisa yani!
 
Chama kinasena sera yetu hatutaki maendeleo ya vitu kama Chadema ukiwachagua wakati unajua hawataleta utakuwa huna akili.

Sera ni mkataba kati ya chama na mpiga kura ukimpa kura usimuulize barabara ziko wapi miradi ya maji iko wapi nk ndio maana mpiga kura asikilize kwa makini sera afanye maamuzi sahihi siku ya kupiga kura.
 
Back
Top Bottom