Wananchi wa usa river walishwa sumu kutoka kampuni ya maua ya kiliflora

kombah

Member
Nov 1, 2010
52
38
Wananchi wa Usa river juzi walipata wakati mgumu baada ya mabomba yote ya maji kutoa maji yenye rangi ya maziwa.Wenyeviti wa vitongoji waliona hali hiyo wakachukua hatua haraka ya kwenda kwenye chanzo cha maji na wakakuta mafundi bomba wa Kiliflora ndio waliounganisha bomba la mbolea ya maua kwenda kwenye bomba la maji masafi ambayo hutumiwa na watu wengi Usa River.Katibu wa mbunge,Ndugu Totian Ndonde,Mwenyekiti wa mji mdogo Kamanda Malisa,pamoja na wenyeviti wa vitongoji wote kwa pamoja walifuatilia jambo hili kwa kina mpaka kwenye shamba la maua na kukuta uzembe uliofanyanywa na mafundi ndio uamuzi waliofuatwa kuchukua maji kuyapeleka kwa mkemia wa mkoa na kukuta kuna kemikali ambazo zinaweza kumdhulu binadamu.Viongozi hao waliitisha mkutano wa wananchi wakiwemo viongozi wa Kiliflora,bwana afya wilaya,mkurugenzi na Afisa maji wilaya.Viongozi wa maua wameomba radhi kwa wananchi wa usa river walisema kwamba jambo hilo halitatokea tena . Wananchi wametoa tamko kuwa watachangishana pesa ili wapate wakili ambae ataweza kuwasaidia ili walipwe fidia kwa kunyweshwa maji yenye kemikali pia wameomba uongozi kumlazimisha mmiliki wa kiliflora kuondoa mfumo wa maji unaopita ndani ya shamba hilo na kulitoa nje ya eneo la shamba ili kusitokee jambo kama hilo vile vile wale wote waliusika na kuunganisha bomba la mbolea katika njia ya maji masafi wachukulwe hatua za haraka.
 
Jk amesema atajenga hospital kubwa kuliko muhimbili, relax, mkianza kuugua ccm is there for you
 
Arumeru mna kazi. Flourine hamjaitoa kwenye maji bado mnawekewa tena sumu ya maji ya maua. Tusubiri utetezi wa
Toto janja (Mh. Nasari).
 
Back
Top Bottom