Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,471
- 23,743
Nilikuwa naongea na rafiki yangu hapa south africa. akawa ananiambia kuwa anatamani sana kama Rais Samia angekuwa Rais wao. Huyu jamaa yangu ni mfanya biashara mkubwa sana hapa Pretoria South Africa. Ni jamaaa wa nne namsikia akisema maneno hayo. Maana last week nilikuwa Zambia nako nilimsikia jamaa mmoja ni Muuzaji wa Mafuta (Mfanyabiashara 0 naye alitamani kama wangekuwa na Rais kama Samia ambaye ameleta mapinduzi Makubwa katika Uchumi ndani ya muda mfupi sana.
Haraka ikaunganisha na lile tamko kuwa kuna maombi ya nchi kama tatu hivi yakitaka Rais Samia awe Rais wao. hapo nikashukuru Mungu kuwa sisi Tanzania tumebarikiwa sana. na inawezekana tusione jambo hili kwa wepesi ila kweli nawaambia nabii hakubaliki kwao. Toka awe madarakani tumeona mapinduzi makubwa sana katika biashara. Nchi sasa imefunguliwa watu wanaingia na kutoka. Zamani hali ilikuwa ngumu na kupelekea hata watu kuanza kuiba yale masega ya kwenye magari kuyatumia. Sasa hayo mambo yameisha hawaibi tena sababu hamna sababu zao zile za kipuuzi ze kuiba wakayavute kama madawa ya kulevya.
Mpaka tukifika mwaka 2025 niamini mimi nachokwambia kuna watu watakuwa wanakuja kumwazima akaongoze nchi zao hata kwa wiki kadhaa tu. Kenya nao naona wanapiga jalamba katika harakati hizi za kumtaka Rais Samia awe wao.
Jamaa hawachelewi kusema ni Rais wao kwa jinsi ambavyo siku zote hupenda vitu vizuri viwe vyao.
Haraka ikaunganisha na lile tamko kuwa kuna maombi ya nchi kama tatu hivi yakitaka Rais Samia awe Rais wao. hapo nikashukuru Mungu kuwa sisi Tanzania tumebarikiwa sana. na inawezekana tusione jambo hili kwa wepesi ila kweli nawaambia nabii hakubaliki kwao. Toka awe madarakani tumeona mapinduzi makubwa sana katika biashara. Nchi sasa imefunguliwa watu wanaingia na kutoka. Zamani hali ilikuwa ngumu na kupelekea hata watu kuanza kuiba yale masega ya kwenye magari kuyatumia. Sasa hayo mambo yameisha hawaibi tena sababu hamna sababu zao zile za kipuuzi ze kuiba wakayavute kama madawa ya kulevya.
Mpaka tukifika mwaka 2025 niamini mimi nachokwambia kuna watu watakuwa wanakuja kumwazima akaongoze nchi zao hata kwa wiki kadhaa tu. Kenya nao naona wanapiga jalamba katika harakati hizi za kumtaka Rais Samia awe wao.
Jamaa hawachelewi kusema ni Rais wao kwa jinsi ambavyo siku zote hupenda vitu vizuri viwe vyao.