Sky Eclat
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 57,595
- 215,272
SALAAM KUTOKA LAMADI KWENDA CHATO ALIKOPUMZIKA MGOMBEA WA CCM NDG. MAGUFULI.
Ndg, mgombea na Mh. Rais salaam sana. Hivi majuzi umekuwa kwenye ziara ya mikutano yako ya kampeni kwa mikoa ya kanda ya ziwa. Watu wamekusanyika kwa hiyari yao na wengine kwa kushawishiwa ili wakusikilize.
Mh. Mgombea umenukuliwa ulipokuwa Bunda na hata ulipofika masanza Busega ukisema wanainchi wasifanye ushabiki katika kuchagua, wasije wakawa kama Bunda, ambayo ilichagua upinzani na matokeo yake inazidiwa mpaka na Lamadi kamji kadogo ila kana taa za barabarani.
Ndg. Mgombea na Mh. Rais, kauli hii sisi wana Lamadi tumeipokea kwa masikitiko makubwa sana, . kwanza tumeiona ni kauli ya kichonganishi kati ya bunda na Lamadi, lkn vile vile ni kauli ya kibaguzi. Lakini tunashangaa kwamba wasaidizi wako hawakukuambia vizuri kwamba hizi taa za Lamadi zimefungwa wakati Lamadi ikiwa chini ya upinzani kbla ya diwani kuunga mkono juhudi.
Lakini pia watu wa Lamadi tunajihoji, kama hoja ya maendeleo ni CCM kuwa watawala, kwa nn hizo taa hazikufungwa
Gamboshi ambako tangu Mungu aumbe dunia mtawala ni CCM?
Lakini kitu cha pekee na cha kushangaza katika mikutano yako, unahubiri ubaguzi wazi wazi, kwamba mkichagua wa vyama vingine sitaleta maendeleo na wakati huo huo unahubiri maendeleo hayana chama!
Ndugu Mgombea na Mh. Rais, tunakuomba sana, ktk hotuba zako punguza kauli za ubaguzi, eleza Sera na usiwalazimishe watu kuchagua kiongozi unayemtaka wewe.
Asalam allaikum.
Ndg, mgombea na Mh. Rais salaam sana. Hivi majuzi umekuwa kwenye ziara ya mikutano yako ya kampeni kwa mikoa ya kanda ya ziwa. Watu wamekusanyika kwa hiyari yao na wengine kwa kushawishiwa ili wakusikilize.
Mh. Mgombea umenukuliwa ulipokuwa Bunda na hata ulipofika masanza Busega ukisema wanainchi wasifanye ushabiki katika kuchagua, wasije wakawa kama Bunda, ambayo ilichagua upinzani na matokeo yake inazidiwa mpaka na Lamadi kamji kadogo ila kana taa za barabarani.
Ndg. Mgombea na Mh. Rais, kauli hii sisi wana Lamadi tumeipokea kwa masikitiko makubwa sana, . kwanza tumeiona ni kauli ya kichonganishi kati ya bunda na Lamadi, lkn vile vile ni kauli ya kibaguzi. Lakini tunashangaa kwamba wasaidizi wako hawakukuambia vizuri kwamba hizi taa za Lamadi zimefungwa wakati Lamadi ikiwa chini ya upinzani kbla ya diwani kuunga mkono juhudi.
Lakini pia watu wa Lamadi tunajihoji, kama hoja ya maendeleo ni CCM kuwa watawala, kwa nn hizo taa hazikufungwa
Gamboshi ambako tangu Mungu aumbe dunia mtawala ni CCM?
Lakini kitu cha pekee na cha kushangaza katika mikutano yako, unahubiri ubaguzi wazi wazi, kwamba mkichagua wa vyama vingine sitaleta maendeleo na wakati huo huo unahubiri maendeleo hayana chama!
Ndugu Mgombea na Mh. Rais, tunakuomba sana, ktk hotuba zako punguza kauli za ubaguzi, eleza Sera na usiwalazimishe watu kuchagua kiongozi unayemtaka wewe.
Asalam allaikum.