Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 8,793
- 12,238
Kuna wananchi wenzetu wa asili ya mkoa wa Kigoma wametaharuki baada ya watu kuhoji uraia wa Dr. Mpango na kuona kama wanabaguliwa.
Hapana, ni jambo la kawaida kwani kuna watu wengi kutoka nchi jirani wanahamia Kigoma. Jambo linalotakiwa ni kujibu hoja mnazoulizwa kwa usahihi na siyo kuanza kuona kama mnabaguliwa na kutengwa. Uraia wa mtu ye yote nchini ni suala la usalama wa nchi na rasilimali zake.
Watu wanaohoji uraia wa Dr Mpango wako sahihi na mwacheni ajibu hoja na siyo ninyi wengine wenyeji wa Kigoma kuanza kumjibia. Ni hoja zake binafsi na yeye ndiye mwenye majibu na siyo ninyi. Kitendo cha baadhi ya wenyeji wa Kigoma kuanza kulalamika na kujenga hoja ya kubaguliwa kikabila halikubaliki. Ukabila au ukanda ni mambo ambayo hayatakiwi na ni ya kuyapiga vita kwa nguvu zetu zote.
Dr Mpango ameteuliwa kuwa makamu wa Rais hivyo wananchi wenzake tunatakiwa kumfahamu vizuri mwenzetu huyu na si vinginevyo. Usalama wa Tanzania kwanza!
Hapana, ni jambo la kawaida kwani kuna watu wengi kutoka nchi jirani wanahamia Kigoma. Jambo linalotakiwa ni kujibu hoja mnazoulizwa kwa usahihi na siyo kuanza kuona kama mnabaguliwa na kutengwa. Uraia wa mtu ye yote nchini ni suala la usalama wa nchi na rasilimali zake.
Watu wanaohoji uraia wa Dr Mpango wako sahihi na mwacheni ajibu hoja na siyo ninyi wengine wenyeji wa Kigoma kuanza kumjibia. Ni hoja zake binafsi na yeye ndiye mwenye majibu na siyo ninyi. Kitendo cha baadhi ya wenyeji wa Kigoma kuanza kulalamika na kujenga hoja ya kubaguliwa kikabila halikubaliki. Ukabila au ukanda ni mambo ambayo hayatakiwi na ni ya kuyapiga vita kwa nguvu zetu zote.
Dr Mpango ameteuliwa kuwa makamu wa Rais hivyo wananchi wenzake tunatakiwa kumfahamu vizuri mwenzetu huyu na si vinginevyo. Usalama wa Tanzania kwanza!