magode
JF-Expert Member
- Oct 2, 2014
- 2,201
- 3,322
Wanajamvi salaam,
Tangu taarifa ya katibu wa serikali wa marekani Mike Pompeo kuweka zuio la watanzania kushiriki bahati nasibu ya kuingia Marekani na kumzuia Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda kuingia Marekani, kumekuwa na mijadala mbalimbali hasa kuhusu zuio la Makonda na tuhuma zake ambazo Pompeo amedai wana ushahidi usio na shaka!
Kama ambavyo sisi wananchi tunapata shida,naamini hata Mkuu wa Nchi huenda anapitia kipindi kigumu sana kutokana na Makonda.
Nawaza huenda Rais ana wakati mgumu zaidi hasa kutokana na taswira ya sasa kati ya Rais na Makonda. Rais kwa sasa huwezi kumsikia akimsifia Makonda kama mwanzo, lakini ilitokea Rais alimpita Makonda bila kumpa mkono wakati makonda alijiandaa kwa tukio hilo.
Lugha ya mwili ya viongozi hawa wawili, ipo wazi kuwa kwa sasa hawana uhusiano unaofaa.
Lakini unajiuliza ugumu wa Makonda kuwajibishwa unatoka wapi!? Hapa ndo nadhani Rais anawaza zaidi kutokana na tuhuma za Makonda na jinsi ya kumuwajibisha.
Ugumu unatokana na jinsi Rais alivyomkumbatia makonda kule nyuma, au pengine Makonda na kiburi chake pengine alikuwa anatumwa.
Hofu ya Mteule wa Makonda, akimtumbua atampeleka wapi ili aendelee kubaki na siri kama alikuwa anatumwa.
Sote tunajua elimu ndogo aliyonayo Makonda, ukimuondoa kwenye ukuu wa mkoa ambayo ndiyo nafasi isiyohitaji elimu wala akili nyingi utampeleka wapi Makonda na akaweza kujizuia kubaki na siri?
Lugha ya mwili na matendo ya Makonda huenda huyu kijana ana siri nzito sana na ukimgusa nchi inatikisika.
Rais ameshaonyesha ishara za wazi za kumchukia Makonda ukilinganisha na siku za nyuma.
Kwa jinsi alivyo Makonda, kama alitumiwa ni vigumu sana kumfanya awe raia na akabaki na siri lazima atasema tu.
Hapa labda Wamarekani waje kumchukua wenyewe lakini kwa hapa nchini, huenda Makonda ana siri nzito na hagusiki. Na Rais hata akimchukia vipi, bado atajilaumu kwa kumkingia kifua huko nyuma.
Nawasilisha.
Tangu taarifa ya katibu wa serikali wa marekani Mike Pompeo kuweka zuio la watanzania kushiriki bahati nasibu ya kuingia Marekani na kumzuia Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda kuingia Marekani, kumekuwa na mijadala mbalimbali hasa kuhusu zuio la Makonda na tuhuma zake ambazo Pompeo amedai wana ushahidi usio na shaka!
Kama ambavyo sisi wananchi tunapata shida,naamini hata Mkuu wa Nchi huenda anapitia kipindi kigumu sana kutokana na Makonda.
Nawaza huenda Rais ana wakati mgumu zaidi hasa kutokana na taswira ya sasa kati ya Rais na Makonda. Rais kwa sasa huwezi kumsikia akimsifia Makonda kama mwanzo, lakini ilitokea Rais alimpita Makonda bila kumpa mkono wakati makonda alijiandaa kwa tukio hilo.
Lugha ya mwili ya viongozi hawa wawili, ipo wazi kuwa kwa sasa hawana uhusiano unaofaa.
Lakini unajiuliza ugumu wa Makonda kuwajibishwa unatoka wapi!? Hapa ndo nadhani Rais anawaza zaidi kutokana na tuhuma za Makonda na jinsi ya kumuwajibisha.
Ugumu unatokana na jinsi Rais alivyomkumbatia makonda kule nyuma, au pengine Makonda na kiburi chake pengine alikuwa anatumwa.
Hofu ya Mteule wa Makonda, akimtumbua atampeleka wapi ili aendelee kubaki na siri kama alikuwa anatumwa.
Sote tunajua elimu ndogo aliyonayo Makonda, ukimuondoa kwenye ukuu wa mkoa ambayo ndiyo nafasi isiyohitaji elimu wala akili nyingi utampeleka wapi Makonda na akaweza kujizuia kubaki na siri?
Lugha ya mwili na matendo ya Makonda huenda huyu kijana ana siri nzito sana na ukimgusa nchi inatikisika.
Rais ameshaonyesha ishara za wazi za kumchukia Makonda ukilinganisha na siku za nyuma.
Kwa jinsi alivyo Makonda, kama alitumiwa ni vigumu sana kumfanya awe raia na akabaki na siri lazima atasema tu.
Hapa labda Wamarekani waje kumchukua wenyewe lakini kwa hapa nchini, huenda Makonda ana siri nzito na hagusiki. Na Rais hata akimchukia vipi, bado atajilaumu kwa kumkingia kifua huko nyuma.
Nawasilisha.