Elections 2010 .......wananchi tuliona; ubunge si saizi yake!!

Omutwale

JF-Expert Member
Feb 4, 2008
1,429
1,045
Nimetoka maeneo ya St. Peter Church. Karibu kabisa na milango MIKUU ya jengo la UMBO la NDEGE. Unyayo wangu umegusa korido kadhaa za JENGO hili. Macho na Masikio yangu vimeona na kusikia yanayoendelea.

MACHO yameona pilikapilika nyingi na MASIKIO yamesikia mabishano MENGI na mijadala mbalimbali. Ni vigumu kufikisha HALI na HISIA za kile macho ilichoona (pilikapilika nyingi)

LAKINI naweza kuelezea NILICHOSIKIA: YULE anamshauri amteuwe MEMBE kuwa Waziri Mkuu eti Pinda siyo PERFORMER na MWINGINE anapendekeza MAGHUFULI kwani huyu si MTU WA MAKUNDI, ANAKUBALIKA KWA WANANCHI NA NI MTENDAJI. Na mwingine anapendekezo, Membe siyo kundi letu (obvious huyu ni shabiki wa EL Camp).

Na Je, vipi kuhusu kutuliza HALI YA NCHI?

WANAMSHAURI ampe MSHINDI wa URAIS nafasi ya KITI cha UBUNGE wa Kuteuliwa mapema tu BAADA ya kula KIAPO.

Baada ya hapo FIKRA zinanijia na napata kukumbuka.


  • HIVI huyu anayependekezwa KUSANDAKALIWA (imetoolewa toka SANDAKALAWE) UBUNGE si angeliupata tu hata kwa kugombea JIMBO LOLOTE TANZANIA BARA?!

  • Na ISITOSHE si alikwishachukua na kurejesha fomu ya UBUNGE lakini WANANCHI wakamwambia hapana TUNAKUHITAJI katika NGAZI YA URAIS?
Mwana JF,
Usichangie HAPA. Mimi TU, KUKUHABARISHA HAYO!
 
Back
Top Bottom