Wananchi Mtwara Mjini wafanya maandamano makubwa kupinga gesi kusafirishwa kwenda Dar!

Good move kama wameruhusiwa...but waangalie wasivunje tu sheria!

Maandamano yana kibali kaka hembu angalia machangu wanavyofuatilia....

2ih34wl.jpg
 
Nabwada uwe mkweli; hivi gesi ikisafirishwa hadi DSM, nyie watu wa Mtwara mtashindwa kuendelea na shughuli zenu za uzalishaji mali. Mie nafikiri mnatumia pasipo wenyewe kujitambua.
Manufaa ya kuwepo kwa gesi yameshafika Mtwara kama vile kuwepo kwa shughuli nyingi za kuingiza kipato tofauti na kabla ya gesi kama vile radio fm ziko nyingi, nyumba za kulala wageni zina soko, biashara kwa ujumla zinalipa siku hizi.
Muelewe gesi inayopangwa kupelekwa DSM ni ziada.
Kiwanda cha cementi kinachojengwa Mtwara hakitaweza kumaliza matumizi ya gesi iliyoko Mtwara hivyo haitakuwa rahisi kurudisha gharama za uzalishaji
"Alijuwaye joto la jiwe ni Mjusi".

Watu wa Mtwara wanaelewa maslahi yao. Labda utumike udikteta kuwanyamazisha. Na ukitumika udikteta litakuwa kosa kubwa sana kisiasa.
 
Huu ni ubinafsi wa hari ya juu.Cha kujiuliza hiyo gesi yote wanataka itumike mtwara pekee?je wataimaliza yote kwa matumizi ya mtwara tu?Je tutapaje fedha za kigeni kama itatumika mtwara tu?
 
Huu ni ubinafsi wa hari ya juu.Cha kujiuliza hiyo gesi yote wanataka itumike mtwara pekee?je wataimaliza yote kwa matumizi ya mtwara tu?Je tutapaje fedha za kigeni kama itatumika mtwara tu?

Ficha ujinga wako....
 
Shida imeanzia kwenye kuelimisha wananchi nini kinafanyika na wao wanafaidikaje.

Kwa mfano mitambo ya kufua umeme wa gesi imejengwa Dar, kwa nini isingejengwa Mtwara?

Hii inakuwa political issue mkuu. Kama watu hawaelewi waelimishwe na si kulaumiwa. Watu wa Mtwara wanaona wamebaguliwa katika maendeleo ya nchi. Wanataka waone hatua za wao kushiriki maendeleo hayo.

Mwnaukweli hii umenena, lakini maoni yangu ni kuwa wanaoleta haya si wananchi na wala si kukosa elimu. Wanaoleta haya ni watu wenye elimu na wanafanya kwa manufaa binafsi. Je Mtwara hakuna mtambo wa kufua umeme kwa gesi? Kwanza mimi binafsi nafikiri matumizi gesi kwa kuiunguza na kuzalisha umeme tu haitatusaidia kimaendeleo. Tunahitaji kufanya zaidi ya hapo kuona kuwa gesi yetu inalifaidia taifa. Tusiwaaminishe wananchi kuwa matumizi ya gesi ni kuzalisha umeme tu na kuwa gesi itamaliza kabisa tatizo letu la umeme!
 
Sisi watanzania ni watu wa ajabu sana!Leo watalalama,wataandandamana na kutoa kila aina ya hisia zao kupitia mabango ila cha ajabu ukija uchaguzi wanachagua watu wale wale tena kwa kura nyingi tu.Sasa sijui tumelogwa au ni uwendawazimu!Majibu sipati.
 
Ndugu zangu wa Mtwara nyie ni watu makini, msiponzwe na CHADEMA, maandamano si njia bora ya kudai haki zenu, tumieni wawakilishi wenu kuanzia madiwani hadi wabunge watafanyia kazi kupitia serikali yetu sikivu

MAFILILI yaani wewe kila maandamano ni ya CHADEMA, hapo sasa kwenye picha nimeona bendera inayofanana na ya CHADEMA ya ADC! Hao ndo wenye hayo maandamano siyo CHADEMA.
 
Last edited by a moderator:
Urusi ndiyo nchi inayoongoza kwa uzalishaji wa gesi duniani na wamejenga bomba la kusafirishia gesi hiyo hadi Bahari Nyeusi (Black Sea) ili waweze kuisafirisha kwenda Ulaya ambako ndiko kuliko na soko!

Itakuwa ajabu kwa gesi ya Mtwara kubaki huko ambako hakuna watumiaji wala soko!

Nadhani kuna upotoshaji mkubwa umefanywa, jitihada zifanyike kutoa elimu sahihi kuhusu gesi na hasa matumizi yake!

Ni kweli kuwa mitambo ya kuzalisha umeme na viwanda vya mbolea vitakavyotumia mali ghafi ya gesi vijengwe Mtwara na Lindi lakini pia bomba la kusafirisha gesi hadi Dar es Salaam, Tanga, Morogoro nk kwa matumizi ya nyumbani na kuendesha magari nk linapaswa kujengwa!

Hapo kwenye red....kitu hicho hiyo serikali yako ndio hawataki kukisikia.....kwani unadhani watu ni wajinga broda!!! Nooo
 
Naomba na ajitokeze mtu na
aeleze faida ya Gesi ya Mtwara kubaki Mtwara...

Pia aeleze hasara za gesi ile kupelekwa katika miji mingine kama
Darisalama....Kwa watu wa Darisalama, kwa watu wa Mtwara na Kwa
Watanzania wote....

anza wewe kwanza kufikiri halafu sisi,lakini kumbuka mtaji wa wanamtwara ni rasilimali ziliaopo mtwara.makamanda komaeni tuko pamoja.
 
nipo hapa pande za bima watu ni wengi mno, foleni ni kubwa sijawahi ona, waandamanaji/wapigananji..wanazunguka barabara kuu huku jeshi la posilisi likiwa nyuma yao lengo kubwa ni kupinga utoaji wa gas ielekee daslam...nyimbo nyiingi wanazoimba ni kwamba hawamtaki hasa ghasia wala mkuchika na gas isiwafate bali wao waifate ilipo....

nb: Kwa hali hii naona watu wa mtwara tumeanza/wameanza kujitambua!! Impact yake gas ikihamishwa itakuwa kubwa kuliko maelezo...we still keep in watching...gas kwanza, vyama baadae!!
More photos to come soon!!stay tuned!!
photoz: Update
wccs2g.jpg
33otb8g.jpg
2vcxjcj.jpg
2zjddhk.jpg
dp7lab.jpg




si walishaona ya kwamba southside ni koloni lao??

Sasa tunawaletea kauzibe ambacho hamkupata kukiwazia hata siku moja
lazima akili iwakae sawa
 
Hizi NGOs na vyama vinavyoshabikia maandamano ya watu wachache wa Mtwara watueleze yafuatayo:-

1. Uzalishaji wa gesi unaofanyika Mtwara
2. Watumiaji wa gesi mkoani Mtwara

Wananchi wasikubali kutumiwa na watu wanaotaka kupata maslahi yao kupitia maandamano

Ya ngoso mwachie ngoso,povu la nini
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom