Hatimaye Taifa limeamka na elimu ya demokrasia inayosambazwa na Chadema imeenea nchi nzima.
Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa ulipita wananchi wa Mto wa Mbu huko Monduli Arusha walipiga kura na kumchagua kwa wingi wa kura mgombea wa Chadema lakini katika hali ya kushangaza inadaiwa kwa maelekezo ya mbunge wa Jimbo hilo Edward Lowassa msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa CCM ndiye mshindi.
Leo kulikuwa na mkutano wa wakazi wa Mto wa Mbu kumtambulisha Mwenyekiti huyo wa CCM hata hivyo ilitokea vurugu kubwa sana na wananchi walimtimua Mwenyekiti huyo kama kibaka na kuapa kwamba hatowaongoza.
Mara baada ya kumtimua kama kibaka mteule huyo wa Lowassa umati huo ulimbeba juujuu mteule wao wa Chadema na kumpeleka kiti cha mbele.Kulikuwa na polisi wengi lakini waliogopa nguvu ya Umma.
Umati huo ulikuwa ukiimba Fukuza vibaka,Fukiza wezi.
Katika uchaguzi wa Serikali za mitaa ulipita wananchi wa Mto wa Mbu huko Monduli Arusha walipiga kura na kumchagua kwa wingi wa kura mgombea wa Chadema lakini katika hali ya kushangaza inadaiwa kwa maelekezo ya mbunge wa Jimbo hilo Edward Lowassa msimamizi wa uchaguzi alimtangaza mgombea wa CCM ndiye mshindi.
Leo kulikuwa na mkutano wa wakazi wa Mto wa Mbu kumtambulisha Mwenyekiti huyo wa CCM hata hivyo ilitokea vurugu kubwa sana na wananchi walimtimua Mwenyekiti huyo kama kibaka na kuapa kwamba hatowaongoza.
Mara baada ya kumtimua kama kibaka mteule huyo wa Lowassa umati huo ulimbeba juujuu mteule wao wa Chadema na kumpeleka kiti cha mbele.Kulikuwa na polisi wengi lakini waliogopa nguvu ya Umma.
Umati huo ulikuwa ukiimba Fukuza vibaka,Fukiza wezi.
Kingine nilichokiona na weledi na utulivu wa askari wa polisi waliokuwa pale. They were very organized and coordinated kwamba kazi yao ilikuwa ni kuhakikisha usalama na si kuingilia mchakato.
Pamoja na zile kelele na heka heka zote, hawakutawanya watu kwa mabomu wala virungu, na wala hawakuziita fujo. Walikaa imara wakiangalia kinachoendelea kama kina madhara kwa yeyote ama la. Hata wakati yule Mpendwa wa wanakijiji anakalishwa kwenye kiti na kurekebishiwa mavazi yake pale mbele, nilimwona askari mmoja, akiwa na silaha yake amesimama karibu kabisa na kile kiti, akiangalia kwa umakini kilichokuwa kikiendelea na baada ya yule kuketishwa, askari yule alionyesha sura ya tabasamu lakini yenye umakini mkubwa.
Tunahitaji askari wenye ufahamu wa kazi yao na wenye uwezo wa kutofautisha kati ya fujo na heka heka za michakato. Angekuwa kamanda usu, ungesikia mabomu ya machozi, virungu na risasi na damu kwa kisingiziokwamba wananchi wamefanya vurugu.
Niliona kitu kizuri sana hiki. Kwamba polisi wajifunze kulinda amani na kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, siyo wao kuingilia michakato na kusababisha fujo.