Wanakijiji wenzangu, nini kilisababisha Mwenyekiti wa Kijiji chetu kukatisha ziara yake ghafla?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,991
144,327
Tukiwa safarini katika basi dogo kutoka sehemu moja ya kijiji chetu kwenda sehemu nyingine,tulifika mahali tukapaki gari ile tupate msosi na pia tuweze kuchimba dawa kabla ya kuendelea na safari.

Wakati baadhi ya wenzetu wakiendelea kupata msosi,sisi tulikaa kakikundi na tukawa tunapiga story za hapa na pale.Tukiwa katikati ya mazungumzo hayo ya muda mfupi,jamaa mmoja aliekuwa anaperuzi simu yake ya mkononi,akagusia swala la mwenyekiti liliokuwa gumzo pale kijijini kwa siku kama mbili au tatu hivi na hapo mada ikabadilika na mjadala ukawa juu ya sintofahamu iliyokuwa imemkumba mwenyekiti wetu.

Kila mtu aliongea lake alilokuwa analijua ama kusikia kuhusu mwenyekiti, ila katika wote waliongea,kuna mwenzetu mmoja alisema kuwa yeye alikuwa katika enep la tukio na walikuwa sehemu wakimsubiri mwenyekiti apite na msafara wake ila cha ajabu msafara wa mwenyekiti haukupita na badala yake alipita mawinguni na kwamba hawakuambiwa hata kilichotokea.

Mimi sikutaka kumuamini sana mwanakijiji yule ila tulipofika safari yetu na mimi kuingia mtaani,nikakuta story ni ile ile katika maeneo mengine ya kijiji na hata katika mitandao habari ikawa ni ile ile.

Sasa kwa wale wadau wanaotoka katika kijiji hiki (kijiji X) na wanaoofahamu hii issue,mnaweza kutueleza ni nini kilimpata mwenyekiti wetu kama habari ile ilikuwa na ukweli kiasi kwamba ilibidi apitishwe mawinguni faster faster kama inavyodaiwa na hawa wanakijiji wenzetu?

Je,walihofia ile mvua na kuhisi njia ya barabara isingefaa kama baadhi ya wanakijiji walivyodhani au kulikuwa na sababu nyingine ambayo haikuwekwa wazi?
 
Japokuwa umeongea kwa mafumbo. Jibu ni RAHISI sana.
Barabara ama mode of transport/Usafiri anaotumia kwenda mahali fulani SI LAZIMA atumie njia HIYO HIYO,ama HUO HUO!.

Hivyo hali HUBADILIKA kulingana na Mazingira Washauri wa masuala husika.
Kwa hivyo mkuu hapa hamna cha nini kilitokea bali ndo wanavyofanyaga.. Unaweza ukawajulisha wale mliokuwa nao kuwa KUMBE inakuwaga ni KAWAIDA tu na si MJADALA!
 
Tatizo walinzi wake wanaomwachiaga simu atakuwa alistuka alipoona meseji inayosema USISAHAU MH MWENYEKITI Jumapili hii tunapiga kura za maoni kuchagua Mwenyekiti wetu Mpya ! Jamaa akakurupuka kurudi nyumbani baada ya kugundua kumbe ulikuwa uchaguzi ngazi ya kitongoji akarudi nyumbani na kuanza kujibroadicastfy waiteni tbfisiemu nataka kuapisha wale wote niliowateuwa na kuwakaimisha vyeo
 
Japokuwa umeongea kwa mafumbo. Jibu ni RAHISI sana.
Barabara ama mode of transport/Usafiri anaotumia kwenda mahali fulani SI LAZIMA atumie njia HIYO HIYO,ama HUO HUO!.

Hivyo hali HUBADILIKA kulingana na Mazingira Washauri wa masuala husika.
Kwa hivyo mkuu hapa hamna cha nini kilitokea bali ndo wanavyofanyaga.. Unaweza ukawajulisha wale mliokuwa nao kuwa KUMBE inakuwaga ni KAWAIDA tu na si MJADALA!

Tofautisha kubadilisha njia ya usafiri na kukatisha ziara. Kama natoka Kijiji A kwenda Kijiji B kwa pikipiki, nikiamua kubadili njia ya usafiri naweza kutumia bajaji, gari binafsi au hata kutembea kwa miguu lakini ntatoka Kijiji A kwenda Kijiji B, hapa kilichotokea ni kukatisha ziara, baadala ya kutoka Kijiji A hawenda kabisa Kijiji B.

Hapo ilikua tunawekana sawa kwanza kwenye maelezo yako. Turudi kwenye hoja sasa.

Salary Slip , ifike mahali tujadili mambo yenye tija. Urais ni taasisi, ni mhimili mkuu uliojichimbia ndani kabisa ( Pascal Mayalla atanisaidia hapo).

Ni vizuri mambo mengine tukawa na subra wanaotakiwa na wenye mamlaka wakatujuza endapo kuna ulazima wa kufanya hivyo.

Vinginevyo ni kuendelea kujivunjia heshima kwa tetesi zisizo na msingi.
 
Safari hii mmeharibu kabisa wachawi nyie
Mmebakia kuulizana nini kilitokea pia hamjui
Unasemaje wewe Nabii Tito?
tapatalk_1571921669725.jpeg
 
Bado mimi naona watu aina ya mleta mada ni wapumbavu sana.

Sioni mkifanya juhudi yeyote ili mpate kura kwenye uchaguzi uliombele yetu lakini uko hapa mmekomaa na afya ya rais ambae tu namuona Ikulu kila siku akipiga kazi. Hakika aliye waita manyumbu na Malofa hakukosea
 
Tukiwa safarini katika basi dogo kutoka sehemu moja ya kijiji chetu kwenda sehemu nyingine,tulifika mahali tukapaki gari ile tupate msosi na pia tuweze kuchimba dawa kabla ya kuendelea na safari.

Wakati baadhi ya wenzetu wakiendelea kupata msosi,sisi tulikaa kakikundi na tukawa tunapiga story za hapa na pale.Tukiwa katikati ya mazungumzo hayo ya muda mfupi,jamaa mmoja aliekuwa anaperuzi simu yake ya mkononi,akagusia swala la mwenyekiti liliokuwa gumzo pale kijijini kwa siku kama mbili au tatu hivi na hapo mada ikabadilika na mjadala ukawa juu ya sintofahamu iliyokuwa imemkumba mwenyekiti wetu.

Kila mtu aliongea lake alilokuwa analijua ama kusikia kuhusu mwenyekiti, ila katika wote waliongea,kuna mwenzetu mmoja alisema kuwa yeye alikuwa katika enep la tukio na walikuwa sehemu wakimsubiri mwenyekiti apite na msafara wake ila cha ajabu msafara wa mwenyekiti haukupita na badala yake alipita mawinguni na kwamba hawakuambiwa hata kilichotokea.

Mimi sikutaka kumuamini sana mwanakijiji yule ila tulipofika safari yetu na mimi kuingia mtaani,nikakuta story ni ile ile katika maeneo mengine ya kijiji na hata katika mitandao habari ikawa ni ile ile.

Sasa kwa wale wadau wanaotoka katika kijiji hiki(kijiji X) na wanaoofahamu hii issue,mnaweza kutueleza ni nini kilimpata mwenyekiti wetu kama habari ile ilikuwa na ukweli kiasi kwamba ilibidi apitishwe mawinguni faster faster kama inavyodaiwa na hawa wanakijiji wenzetu?

Je,walihofia ile mvua na kuhisi njia ya barabara isingefaa kama baadhi ya wanakijiji walivyodhani au kulikuwa na sababu nyingine ambayo haikuwekwa wazi?
Mbinu yenu ya kishetani iligunduliwa ndiyo maana fasta akapitishwa mawinguni mkabaki hoi bin tabani.....!!
 
Bado mimi naona watu aina ya mleta mada ni wapumbavu sana.

Sioni mkifanya juhudi yeyote ili mpate kura kwenye uchaguzi uliombele yetu lakini uko hapa mmekomaa na afya ya rais ambae tu namuona Ikulu kila siku akipiga kazi. Hakika aliye waita manyumbu na Malofa hakukosea
Labda ikulu ya Gamboshi maana hajaonekana onekana kihivyo baada ya kukatisha ziara zake.
 
Back
Top Bottom