supercharger GT
JF-Expert Member
- Sep 25, 2016
- 1,007
- 1,944
Wanakijiji wa kijiji kilicho ndani ya wilaya ya Igunga na kupakana na mkoa wa Singida wameamua kufunga barabara kwa kuweka mawe barabarani na kuzuia magari yote yanayotoka mkoani Tabora au kuingia mkoani Tabora wakishinikiza kuonana na Mkuu wa Wilaya au Mkuu wa mkoa huku wakiwa na silaha za jadi ambayo ni mikuki na mishale!
Barabara hiyo imefungwa tangu saa mbili asubuhi mpaka sasa hivi. Juhudi za baadhi ya askari na watu mbalimbali kuwatuliza waruhusu magari hazijafinikiwa mpaka sasa!
Wanakijiji wenyewe wanadai Sababu ya wao kufanya hivyo ni kutokana na uonevu waliofanyiwa wenzao baadhi kwa kubomolewa nyumba zao na kuibiwa mifugo yao na watu wanaodai ni watu wenye nguvu serikalini
Sent using Jamii Forums mobile app
Barabara hiyo imefungwa tangu saa mbili asubuhi mpaka sasa hivi. Juhudi za baadhi ya askari na watu mbalimbali kuwatuliza waruhusu magari hazijafinikiwa mpaka sasa!
Wanakijiji wenyewe wanadai Sababu ya wao kufanya hivyo ni kutokana na uonevu waliofanyiwa wenzao baadhi kwa kubomolewa nyumba zao na kuibiwa mifugo yao na watu wanaodai ni watu wenye nguvu serikalini
Sent using Jamii Forums mobile app