kALEnga kidamali
JF-Expert Member
- Nov 19, 2015
- 542
- 733
Jimbo la Kalenga hakika limempata mkombozi, Jackson Kiswaga ni moja kati ya watu makini mno kuwahi tokea hapa jimboni kwetu, huyu ndugu Kiswaga alianza kushiriki moja kwa moja kwenye shughuli za maendeleo miaka mingi iliyopita, huyu kwetu wana Kalenga ndiye mzalendo wa kweli na hakuwahi kuisahau kalenga hata mara moja licha ya majukumu yake makubwa aliyokuwa nayo wakati huo tena akiwa mikoa ya mbali ila hakuiacha Kalenga. Aliwahi kuwa meneja wa kanda kwenye makampuni ya simu Tigo na Vodacom.
Kiukweli amejitoa sana kusaidia wananchi wa kalenga kama vile kusomesha watoto wasiojiweza na kuchangia miradi ya maendeleo jimboni, wana kalenga tumpeleke huyu KISWAGA bungeni akatung'arishie jimbo letu baada ya kuwa pweke kwa muda mrefu.
Kiukweli amejitoa sana kusaidia wananchi wa kalenga kama vile kusomesha watoto wasiojiweza na kuchangia miradi ya maendeleo jimboni, wana kalenga tumpeleke huyu KISWAGA bungeni akatung'arishie jimbo letu baada ya kuwa pweke kwa muda mrefu.