WanaJF tungekuwa wakweli

Ndio kusema wewe huuishi uhalisia wa Maisha yako unapokuwa JF?
Habari wapendwa!
Nimekaa nikatafakari kwa kutumia akili ya kawaida tu ( common sense), nikafikiri ambavyo ingekuwa vyema kama tungeishi maisha halisi humu,

Tungekuwa na uwezo wa kusaidiana kwa kupeana fursa na mipango mizuri ya kutuwezesha sisi kufanikisha mambo yetu kupitia network ambayo tungeitengeneza kupitia jamiiforums,

Mfano, kama mimi ni mkulima wa mahindi ningelikuwa na uwezekano wa kupata soko kwa watu wenye mashine za kukoboa au kupack nafaka na unga, wenye kampuni za ulinzi wangepata maeneo ya kutoa huduma hizo, wenye kampuni za udalali pia vivyo hivyo.

Tungekuwa na mahusiano yenye tija( mutual benefit) baina yetu wana jf, tungetengeneza jamii yenye kusaidiana kulingana na nafasi ya kila mmoja wetu.

Tatizo tunaishi fake life kiasi kwamba baadhi ya watu humu wameji brand hadhi fulani ambazo huenda hawana!

Kwa sisi wafugaji wa ng'ombe tungepata soko la maziwa na nyama hasa kwa walioko mijini hata kwa makubaliano maalumu ili wote tunufaike.

NB: Hii ingewezekana iwapo tungefahamiana physically, na kujiridhisha pasi na shaka kuwa wahusika mpo kwenye uhalisia ili kuepuka utapeli.

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi nakula kwa wazazi wangu hata vocha ya kuingia hapa nimeiba ,,Leo nimetumwa nyama kilo tatu nikaleta 2.5 nika-save 3000/= ndo nmenunua vocha .Yaani kiufupi bado Mimi ni Mfugo kwa wazazi wangu .

Huo ndo Ukweli wangu karibu sasa tufanye biashara ya kuuziana mahindi ,karanga na maziwa kutoka huko kijiji kwako
 
Ni wazo zuri,nadhani kwa anayejisikia kuweka 'real ID' akatazwi,ila chamuhimu ni kujua unapata faida/hasara gani kwa kutumia hiyo ID.
 
Mimi nakula kwa wazazi wangu hata vocha ya kuingia hapa nimeiba ,,Leo nimetumwa nyama kilo tatu nikaleta 2.5 nika-save 3000/= ndo nmenunua vocha .Yaani kiufupi bado Mimi ni Mfugo kwa wazazi wangu .

Huo ndo Ukweli wangu karibu sasa tufanye biashara ya kuuziana mahindi ,karanga na maziwa kutoka huko kijiji kwako
That's why you sound pupy!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom