WanaJF: Dowans - Unafiki; Maneno Mengi zaidi ya Vitendo!!

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Mjadala wa Dowans umezidi kuendelea. Wazungumzaji wamekuwa wengi. Kila mtu anatoa mawazo yake. Kila mtu anatoa msimamo wake. Mtanzania wa kawaida haelewi nini cha kufanya. Mjadala wa wasomi unamuhusu nini? Kinachomuhusu yeye ni ugumu wa maisha zidisha mara tano!!

Humu jamvini ni post baada ya post, Dowans! Dowans! Dowans! Mpaka watalipwa sisi tunapiga story tu! Mawazo yanayotolewa ya nini kifanyike yanaishia hewani!!

Watu wanataka kuandamana lakini hakuna tarehe inayopangwa, hakuna maandalizi yanayofanyika! Inakuwa kama tumepigwa butwaa.

Najiuliza, hivi mtu akibakwa mara kwa mara anaishia kulia tu bila kupiga kelele? Je anafika mahali anabaki kumwangalia mbakaji bila kuomba msaada? Eti akipiga kelele atakosa mtu wa kumuoa au akiolewa watu hawatamchangia!!

Huu ni upunguani. Humu jamvini tunaongeleshana, tunajibizana na kushauriana lakini hujui unamshauri nani, unajadili na nani na matokeo yake ni yapi. Hapo ndipo ugumu wa utekelezaji wa mapendekezo unapotokea!! Inakuwa ni kupiga story tu!!

Unafiki unachomoza, uoga unadhihirika!

Nafikia mahali naanza kuvisualize posts zitakazo andikwa siku Dowans wanalipwa! Lakini itakuwa too late!! Tutakuwa tushabakwa tunabakia kulalamika na kumuachia Mungu amlaani aliyetubaka!!

Tukubaliane cha kufanya, tarehe ya kufanya, mahali pa kufanya na jinsi ya kufanya. Kama hatuwezi basi tuharakishe walipwe maisha yaendelee. Kama huwezi kuzuia kubakwa basi tembea na kinga mbakaji akija mpe atumie usipate maambukizo na mwambie amalize haja yake haraka wewe uwahi kufanya mambo mengine!!

Kwa kitakachopendekezwa nitashiriki. Kama ni kwa mkoa Arusha nitashiriki kikamilifu.

KUMBUKA.

1. Hatupingi sheria kwamba ukishtakiwa na ukashindwa kesi unatakiwa kulipa.

2. Hatupingi kwamba tumesaini treaty/convention iliyoanzisha ICC.

Tunapinga;

1. Mkataba feki kati ya Richmond na Tanesco kuidhinishwa na kutoa haki kwa Dowans hata kama tumechelewa kupinga.

2. Tunapinga uharaka wa kulipa deni hilo. Na pia matisho kwamba tutanyimwa misaada. Sasa kama ni misaada si watusaidie kulipa hilo deni? Si msaada pia? Au?

3. Tunapinga kauli mbalimbali kwamba Dowans lazima walipwe bila kujaribu kuweka pressure ili kujua ukweli wa kilichojiri mpaka tupo hapa tulipo.

Tunataka;

1. Aliyeisajili Richmond nchini bila kujiridhisha uhalali wake awajibishwe. Tumjue ni nani na hatua gani zimechukuliwa.

2. Tunataka aliyeshiriki mazungumzo na Richmond i.e vikao nk awajibishwe na atueleze aliifahamuje hiyo kampuni na alifanya due diligence search akagundua nini mpaka wakasaini mkataba.

3. walioshauri kuvunja mkataba na kupongezwa na PM watoe maelezo kwa nini walitushauri vibaya na ikiwezekana tuwafungulie mashtaka kwa professional negligence na kudai fidia.

4. Waliotuwakilisha huko ICC au hotelini watueleze wameshindwaje kesi hii. Ni uwezo mdogo au walifanya makusudi?

5. Dowans hatuna hela za kuwalipa sio kwamba hatutaki peke yake. Mdaiwa hafungwi jamani. Na sheria inakataza kushika mali za serikali sasa tusipolipa inakuwaje? Mbona Omar Bashir amegoma kwenda the Hague na bado anaendelea na maisha? Huu wema wetu utatuponza!

Tufike mahali tuamue na tutende! Hakuna cha kusubiri!
 
Kwenye mjadadala huu yalinadikwa yafuatayo:



1. 'Jamhuri Ya Ukombozi' yaundwa ndani ya Tanzania inahusisha Warundi na Watanzania

Originally Posted by bonvize https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...husisha-warundi-na-watanzania.html#post888411
Ni vizuri kuangalia jambo hili katika upeo mpana zaidi,kwa kuwa hata nchi ambazo hazina utulivu sasa kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe zilianzia kwenye vikundi kama hivi ambavyo vilikuwa na nia ya ukombozi kutokana na unyonyaji unaofanya na kikundi kidogo cha watu kilichopatiwa thamana ya nchi kwa hila na mbinu chafu (kwa mf CCM).
Kutokana na watu kukata tamaa halitakuwa jambo jipya kuona vikundi kama hivi vikiibuka kutoka pembe tofauti za nchi yetu kwa kuwa watu wamepoteza imani na watu waliopewa dhamana kwa hiyo wanaweza kukabidhi imani yao ha kwa wehu kama hao.

Ni kweli suala hili liangaliwe kwa upana wake. Niliwahi kuandika humu kuwa hivi sasa wadanganyika wanakosa kiongozi kama kinjeketile atakayewaambia risasi zitageuka maji, na watamfuata; kwa maana wamechoka na hali hii mbaya ya maisha. Sasa isije ikawa kuna mtu kishajitokeza; kwa hakika anaweza kupata wafuasi wengi katika muda mfupi sana, maana mtu ambaye hana uhakika wa kula hata mlo mmoja, na wakati huo huo anasikia mbunge analipwa zaidi ya 100,000 kwa kikao cha siku moja, anasikia watu wamekwiba fedha nyingi na bado hawachukuliwi hatua, na wakati huo huo yeye anaambiwa nchi ni maskini; akiambiwa njoo tuna silaha za kutufanya tupate milo mitatu kwa siku hakika atakubali kujiunga nao; kwake kuwa msituni akauawa huko ni sawa kwani hata bila ya kuwa msituni yupo anakufa taratibu na 'amani' yake.
Wakati tukitafuta namna ya kuwaangamiza watu hawa mara moja, tuwe tayari pia kushughulikia mafisadi ambao wanaweza kuwa sababu ya watu hawa kujiunga pamoja!


Mantiki ya hoja hiyo hapo juu, bado yana msingi
 
Kwenye mjadadala huu yalinadikwa yafuatayo:



1. 'Jamhuri Ya Ukombozi' yaundwa ndani ya Tanzania inahusisha Warundi na Watanzania

Originally Posted by bonvize https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...husisha-warundi-na-watanzania.html#post888411
Ni vizuri kuangalia jambo hili katika upeo mpana zaidi,kwa kuwa hata nchi ambazo hazina utulivu sasa kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe zilianzia kwenye vikundi kama hivi ambavyo vilikuwa na nia ya ukombozi kutokana na unyonyaji unaofanya na kikundi kidogo cha watu kilichopatiwa thamana ya nchi kwa hila na mbinu chafu (kwa mf CCM).
Kutokana na watu kukata tamaa halitakuwa jambo jipya kuona vikundi kama hivi vikiibuka kutoka pembe tofauti za nchi yetu kwa kuwa watu wamepoteza imani na watu waliopewa dhamana kwa hiyo wanaweza kukabidhi imani yao ha kwa wehu kama hao.

Ni kweli suala hili liangaliwe kwa upana wake. Niliwahi kuandika humu kuwa hivi sasa wadanganyika wanakosa kiongozi kama kinjeketile atakayewaambia risasi zitageuka maji, na watamfuata; kwa maana wamechoka na hali hii mbaya ya maisha. Sasa isije ikawa kuna mtu kishajitokeza; kwa hakika anaweza kupata wafuasi wengi katika muda mfupi sana, maana mtu ambaye hana uhakika wa kula hata mlo mmoja, na wakati huo huo anasikia mbunge analipwa zaidi ya 100,000 kwa kikao cha siku moja, anasikia watu wamekwiba fedha nyingi na bado hawachukuliwi hatua, na wakati huo huo yeye anaambiwa nchi ni maskini; akiambiwa njoo tuna silaha za kutufanya tupate milo mitatu kwa siku hakika atakubali kujiunga nao; kwake kuwa msituni akauawa huko ni sawa kwani hata bila ya kuwa msituni yupo anakufa taratibu na 'amani' yake.
Wakati tukitafuta namna ya kuwaangamiza watu hawa mara moja, tuwe tayari pia kushughulikia mafisadi ambao wanaweza kuwa sababu ya watu hawa kujiunga pamoja!


Mantiki ya hoja hiyo hapo juu, bado yana msingi

Ni kweli kabisa. Idadi ya watu wanaoamua kuokoka inaongezeka, kwa nini? Wananchi wameamua kufind answers za matatizo yao sehemu nyingine. Lakini na hao wanaoanzisha makanisa (sio wote) wengine ni njia ya kupata kipato! Wanawachangisha wananchi fedha na vito vya thamani ili na wao wapate kula.

Itafika mahali atatokea mtu atawapa tumaini jipya, msitu! Atawapa imani mpya, kisasi! Wengi watamfuata na hapo tutakuwa tumechelewa!
 
Ni kweli kabisa. Idadi ya watu wanaoamua kuokoka inaongezeka, kwa nini? Wananchi wameamua kufind answers za matatizo yao sehemu nyingine. Lakini na hao wanaoanzisha makanisa (sio wote) wengine ni njia ya kupata kipato! Wanawachangisha wananchi fedha na vito vya thamani ili na wao wapate kula.

Itafika mahali atatokea mtu atawapa tumaini jipya, msitu! Atawapa imani mpya, kisasi! Wengi watamfuata na hapo tutakuwa tumechelewa!
Kiongozi,
Hoja zako zinaongeza pressure kumwoyo!
Nimekaa mbele ya pc napigapiga meza sijui cha kufanya.
Lakini kilio hiki kipo all over Tanzania...Na kwa mfumo wetu wa utawala, mwakilishi wa wananchi ni Mbunge...Je mbunge huyu ni lazima awe ndani ya mjengo ndipo aweze kuongea kero za wananchi wake?...hakuna njia mbadala ya ku'petition hoja 'pressing' kama hizi ili kuzishughulikia?...Hivi hakuna Bubge la dharula?
Njia ya Maandamano ni kweli ingefanya kazi kwa sehemu zinginezo duniani..lakini njia hii haijaprove kutoa matunda kwa hapa nchini!...sipendi ukumbusha ya Arusha!
Mkuu alishatamka kwamba "sipendi kuona watu wanaenda kwenye maongezi wakiwa na plasta", kwa maana kwamba yeye anaona dawa ya maandamano yoyote ni kuyapiga mabomu!...
Vinginevyo kwa sasa tutaendelea tu kuandika sana hapa, lakini kama hatumove just an extra milimetre kujaribisha next level, basi tusitegemee badiliko!
Ni ukweli mbaya sana huu!
 
Sawa kabisa.

Vitendo bila kuchelewa!!! ndio siri, yamafanikioooo katika kazi!!!!!!!

Kama tunapinga malipo, tupinge kwa vitendo sasa, mijadala inatosha.
 
Mjadala wa Dowans umezidi kuendelea. Wazungumzaji wamekuwa wengi. Kila mtu anatoa mawazo yake. Kila mtu anatoa msimamo wake. Mtanzania wa kawaida haelewi nini cha kufanya. Mjadala wa wasomi unamuhusu nini? Kinachomuhusu yeye ni ugumu wa maisha zidisha mara tano!!

Humu jamvini ni post baada ya post, Dowans! Dowans! Dowans! Mpaka watalipwa sisi tunapiga story tu! Mawazo yanayotolewa ya nini kifanyike yanaishia hewani!!

Watu wanataka kuandamana lakini hakuna tarehe inayopangwa, hakuna tarehe iliyopangwa,hakuna maandalizi yaliyofanyika.Inakuwa kama tumepigwa butwaa.Tukubaliane cha kufanya, tarehe ya kufanya, mahali pa kufanya na jinsi ya kufanya. Kama hatuwezi basi tuharakishe walipwe maisha yaendelee.
Huu ni upunguani. Humu jamvini tunaongeleshana, tunajibizana na kushauriana lakini hujui unamshauri nani, unajadili na nani na matokeo yake ni yapi. Hapo ndipo ugumu wa utekelezaji wa mapendekezo unapotokea!! Inakuwa ni kupiga story tu!!

Unafiki unachomoza, uoga unadhihirika!!

Tufike mahali tuamue na tutende! Hakuna cha kusubiri!


Nakubaliana na wewe asilimia 100,tumekuwa watu wa maneno sana,tutende,tutakuwa tumetenda haki kwa kuwa na ufahamu wa haya yote.Tuwe viongozi, i guess many of us will be proud to be part of this movement against DOWANS and any other evil/corrupt decision made that costs us.....Thank you for this post! Mi niko tayari wewe je????:amen:
 
Kiongozi,
Hoja zako zinaongeza pressure kumwoyo!
Nimekaa mbele ya pc napigapiga meza sijui cha kufanya.
Lakini kilio hiki kipo all over Tanzania...Na kwa mfumo wetu wa utawala, mwakilishi wa wananchi ni Mbunge...Je mbunge huyu ni lazima awe ndani ya mjengo ndipo aweze kuongea kero za wananchi wake?...hakuna njia mbadala ya ku'petition hoja 'pressing' kama hizi ili kuzishughulikia?...Hivi hakuna Bubge la dharula?
Njia ya Maandamano ni kweli ingefanya kazi kwa sehemu zinginezo duniani..lakini njia hii haijaprove kutoa matunda kwa hapa nchini!...sipendi ukumbusha ya Arusha!
Mkuu alishatamka kwamba "sipendi kuona watu wanaenda kwenye maongezi wakiwa na plasta", kwa maana kwamba yeye anaona dawa ya maandamano yoyote ni kuyapiga mabomu!...
Vinginevyo kwa sasa tutaendelea tu kuandika sana hapa, lakini kama hatumove just an extra milimetre kujaribisha next level, basi tusitegemee badiliko!
Ni ukweli mbaya sana huu!

PakaJimmy, mimi nilikuwepo Arusha siku maandamano na siku ya mazishi. Kuna kijana mmoja hana zaidi ya miaka 21. Alikuwa amekaa chini ya jukwaa kuu huku Diwani mmoja wa CCM anaitwa Mawazo akiwa anaongea baada ya raia kumshikia bango amefuata nini kwenye mkutano tar 5. Yule kijana alikuwa haongei anamuangalia machozi yanamtoka kwa hasira!! Nikawa namuangalia, mara akasogea pembeni akanyanua jiwe!! Wakati Mawazo anashuka taratibu kijana akawa anajipenyeza kumkaribia ampige jiwe. Nikamshtua bouncer akamuwahi. Aliponyang'anywa jiwe dogo akaendelea na kilio huku akisema 'labda huyu k*** ahame Arusha'. Ilibidi Mawazo apakiwe kwenye gari ya Dr Slaa aokolewe!! Hiyo ni hasira! Je nikimpa huyo kijana SMG nikamuelekeza alipo waziri fulani inakuwaje?

Wapo vijana wengi ambao wamechoka. Ukiangalia umati wa NMC utaona imani mpya na tumaini jipya linavyojengeka. Kama CDM watatumia vibaya hasira na kuchoka kwa wananchi hakuna atakayekuwa salama.

Kila mwenye shida anamuona asiye na shida ndiye mbaya wake. Angalia hasira za wananchi Mbarali, mwekezaji ndie tatizo! Choma gari lake. Polisi wanaomtetea tatizo, tukabidhiwe tumwonyeshe!

Tunaenda wapi? Unadhani tuko mbali?

Hapo machame kuna wananchi wana hasira na mwekezaji eti ameloga mvua. Mvua hainyeshi kwa sababu ameanzisha shamba la maua! Utajiuliza Albert hii ni nini? Na mimi nitakuuliza hivyo hivyo!! Ila ni ishara ya hasira na njia ya kutafuta mbaya wao hata kama sie!

Kuandamana inaweza sababisha kipigo. Kipigo ni njia ya kutuogopesha. Lakini pia huwa kinaleta usugu na hasira zaidi. Watawala wakiamini kwamba tunaogopa hata tuandike vipi wanajua hakuna la zaidi tutakalofanya. At least maandamano yatafanyika mchana. Hayakuwa na silaha.

Wasiwasi wangu ni pale yatakapofanyika usiku baada ya kuandaliwa msituni! Yatakapokuwa na silaha kutoka kwa wasomali na burundi! Hapo itakuwa tabu. Fikiria hasira uliyonayo na umekaa mbele ya PC ulinganishe na hasira aliyenayo aliyelala kwenye wheel barrow sasa hivi hana mzigo wa kubeba! Halafu wewe na yeye mkutane!
 
Naomba sasa tukubaliane njia ya kuchukua, tuache maneno.
Mimi naamini maandamano ni njia ya kwanza - nayaamini kwani hakuna hata sehemu moja ambako maandamano ya muda mrefu hayakuzaa matunda yaliyokusudiwa. Ni kweli yanagharimu maisha kama ilivyotokea Arusha, lakini si watu wengi watakaopoteza maisha kama vile kuingia msituni.
Tumepoteza fursa ya Arusha; hayo ya Arusha yangeendelea kesho yake wangeua labda 20 au zaidi, na dsm mwanza na dodoma wangelipuka, maandamano yangeendelea na vifo vingeongezeka lakini wa dsm wangeelekea ikulu na wa dodoma kwa waziri mkuu, hakika ingefika mahali Pinda anaiacha ofisi (najua huyu angekuwa wa kwanza kuachia),halafu Jk huko ikulu angefika mahali nae akaachia maana waziri mkuu akishatoka maana yake baraza zima limetoka! nk na rais hawezi kutawala bila mawaziri na muda wa kuunda baraza jipya asingeupata au wapya ambao angewateua wasingekubali, wangeogopa nguvu ya umma!
Tuondoe woga, tuandamane hasa wale walioko kwenye kitovu cha nchi; msitarajie watu wakaandamana njombe au kasulu kilio chao kisikike kama aliyeandamana dsm, dodoma, arusha na Mwanza.
Tunisia walianzia kwenye mazishi ya kijana kijana aliyejichoma moto baada ya kudhulumiwa na askari wa halmashauri na malalamiko yake kufungiwa milango kila alipojaribu kuyapeleka, je sisi tunaanzia wapi? Wakianzisha CDM mnasema udini, ukabila nk, wakianzisha CUF mnasema udini nk mnasahau kuwa ugumu wa maisha hauchagui imani ya mtu.
Naomba yeyote atakayeanzisha tumuunge mkono
 
Wasomi ni kundi lenye nguvu sana katika jamii. Kwanza wanafanya utafiti pili wanaeleza suluhisho. Ndio maana zamani wasomi wa vyuo vikuu walikuwa wanaheshimika. Sasa hivi ukisikia mgomo chuo kikuu chochote ni kuhusu posho na mikopo yao. Hakuna atakayeanzisha mgomo chuo kikuu kupinga malipo ya Dowans kwa kuona kwamba wanakosa mikopo kwa malipo kama hayo kufanyika na matumizi mengine yasiyo ya lazima. Wanagomea kukosa mikopo lakini hawagomei sababu zinazosababisha mikopo na posho kukosekana!!

CDM wakianzisha CCM hawatashiriki, CUF watataka kuanzisha ya kwao nk

Napata tabu kujua njia ipi itumike. Kundi gani liongoze hii movement! Ngo's nazo zinaliangalia hili suala kwa kusita. Hakuna inayosimama kidedea kuingia front!

Bado miguu yetu imekuwa reluctant. Vyovyote itakavyokuwa ngoja niwasilishe hoja kwa uongozi wa CDM kusikia msimamo wa chama ingawaje nisingependa tushindwe kushiriki kutokana na itikadi! Hili ni la watanzania wote!
 
Alberto, unazidi kututia hasira na hoja zako. Hakuna Mtanzania mwenye akili timamu ambaye kwa kweli hili swala la Dowans halimpi shida. Ni wale tuu ambao Dowans imewanufaisha kwa namna moja au nyingine ndo wanalitetea. Kumekua na uozo ambao hahuhitaji hata kwenda shule ndo ujue uozo uliopo kwenye Dowans na mwenendo mzima wa kesi na uharaka wa kutaka kulipa deni. Unajiuliza ni kwa nini hawa watu wanaharaka hivi..kama wameshinda kesi si hela yao watapata?? Ila kwa vile hawajashinda ndo maana wanataka wapewe hela haraka.

Kama ulivyosema hakuna atakaefungwa hapa kwa Tanzania kushindwa kulipa hizo hela, na ni lazima tujiridhishe kwanza kabla ya kufanya hayo malipo. Hili swala lipo wazi... ni ufisadi umefanyika hapo na hatuna haki ya kulipa, tunachotakiwa sasa hivi ni kuruka na mmoja mmoja aliyehusika kwenye mchakato mzima, kuanzia Richmond hadi hao walioiwakilisha serikali kwenye kesi na serikali kushindwa. Hao wote ni wa kukamata na kuwajibisha. Kwani ndiyo wanaipeleka nchi kwenye shimo.

Tanzania imekua ni nchi isiyokua na tumaini tena, watu wake wamechoka kupita maelezo, ona maisha yalivyopanda, hata huduma zile za msingi zinapanda. Katika nchi yoyote, serikali inajivunia kwa kuweza kuzifanya huduma zote za jamii kuweza kumfikia mwananchi na kuzipata kwa uwezo wake na sio kumkomoa. Ona bei ya gesi, mafuta n.k hivi sisi wananchi kweli tutaacha kua na hasira? Imefikia sasa kila mtu anamuona mwenzie ndo mchawi na ndiyo anazidisha matatizo dhidi yake.

Ni wakati wa kila mmojawetu wa kusema no na kunyanyuka hapo alipo na kuchukua hatua. Kama ni maandamano yasiwe ye CDM au CUF au NGO's yawe ya nchi nzima, najua CCM hawatataka maandamano kwani ni kuumbuka. Mungu ibariki Tanzania
 
Mambo haya yoote, yana mwisho wake! na mwisho huo uko kariibu saaana! :smile-big:
 
Back
Top Bottom