Wanajeshi wadaiwa kutembeza kipigo kwa raia, 10 taabani

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,419
21,253
Wanajeshi wadaiwa kutembeza kipigo kwa raia, 10 taabani


Na Mwandishi Wetu,Tanga

BAADHI ya askari wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Kambi ya Maramba mkoani Tanga wanadaiwa kutembeza kipigo kwa wakazi wa eneo hilo ambapo watu 10 wamejeruhiwa vibaya na kulazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Tanga, Bombo.

Wanajeshi hao zaidi ya 20 wakiwa wamevalia sare za kazi, wanadaiwa kuwavamia wananchi hao wa Mramba na kuwapiga kwa kutumia marungu na magongo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Bw.Simon Sirro aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 25 mwaka huu saa 5 usiku huko Maramba wilayani Mkinga.

Kamanda Sirro, alisema wanajeshi hao pia wanadaiwa kuharibu mali za wananchi hao ikiwa ni pamoja na kuvunja vioo vya magari mawili, moja ni Toyota Hiace lenye namba za usajili T 130AHZ na lori lenye namba namba T871ASM .

Kamanda Sirro alisema chanzo cha vurugu hizo ni ugomvi uliotokea Agosti 24 mwaka huu ya saa 7 usiku eneo la Maramba 'B' kwenye ukumbi wa disko ambapo askari wa JKT aliyefahamika kwa jina la Bw. Godfrey Mwita (23)alijeruhiwa kwa kupigwa jiwe kichwani na mfanyabiashara Bw. Peter Gabriel (18), mkazi wa Maramba.

Alisema chimbuko la ugomvi huo ni mwanamke waliyemkuta hapo ukumbi. Baada ya kutokea vurugu hizo, Bw. Peter alikamatwa, kufungwa pingu na kupelekwa kwa mlinzi wa amani wa eneo hilo ambapo baada ya muda mfupi aliachiwa huru.

Ilildaiwa kuwa kitendo cha kuachiwa mfanyabiashara huyo kiliibua hasira kwa askari hao na kuamua kulipiza kisasi kwa wakazi wote wa eneo hilo.

Kamanda Sirro aliwataja waliojeruhiwa katika tukio hilo kuwa ni Bw. Ali Husein (50), Bw. Dustan Maghembe (37), Bi.Tabu Mustafa (56), Bw. Juma Athman (38) na Bw.Wales Mbwana (59).

Wengine Bw. Baltazar Christopher (45), Bi. Mwanaisha Adam (28), Bi. Saumu Dua (19),Bw. Charles Mbaga(26) Bw. Musa Mohamed (21).

Kamanda Sirro alisema hadi sasa Polisi hawajafanikiwa kumkamata mtuhumiwa yeyote kuhusiana na tukio hilo na Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasi (FFU) wamepelekwa eneo hilo kudhibiti vurugu hizo.
 
Nilipoona hayo majina harakaharaka nikadhani kuwa ni askari waliofanya fujo na kukamatwa, kumbe ni ya waliojeruhiwa. Inasikitisha kuwa watuhumiwa hawajakamatwa mpaka sasa hivi
 
WANAJESHI SI KAMA POLISI AU TRAFFICK.......!
WANA NIDHAMU, WAPOLE NA PIA SI WAONEAJI KAMA POLISI , MAHAKIMU, TRA, TANESCO, AUX.POLICE N.K...!
DAIMA NI VIGUMU KUSIKIA WAKIONEA MTU YEYOTE.......!
WAKICHOKOZWA hapo ndo utawajua wao ni askari ama la....!
mara nyingi wao si WAANZISHA vurumai, bali kanuni watumiayo ni AKUANZAYE MMALIZE....!
NI wamoja katika matatizo na shida zao mbalimbali, na pindi mwenzao anapofanyiwa uhalifu ni kama umetukana GESHI zima....!
kwa ile mitaa ambayo wanalea watoto wao ambao ni vibaka na wakwapuaji, na watoto hao pindi wafikishwapo polisi hutolewa kwa hongo. wakimpora MJESHI hapo ndo huchanganywa waliomo na wasiokuwamo.....! (KWA NINI MITAANI TUNALEA VIBAKA?)
 
Hawa ni walinzi wa nchi na mipaka yake, wananchi hulindwa na polisi. Hivyo kwa ndani mwanajeshi ni sawa na mwananchi kwani pia hulindwa na askari polisi. Akiudhiwa anapaswa kushirikiana na jeshi la polisi na sio kuchukua hatua miguuni.
 
WANAJESHI SI KAMA POLISI AU TRAFFICK.......!
WANA NIDHAMU, WAPOLE NA PIA SI WAONEAJI KAMA POLISI , MAHAKIMU, TRA, TANESCO, AUX.POLICE N.K...!
DAIMA NI VIGUMU KUSIKIA WAKIONEA MTU YEYOTE.......!
WAKICHOKOZWA hapo ndo utawajua wao ni askari ama la....!
mara nyingi wao si WAANZISHA vurumai, bali kanuni watumiayo ni AKUANZAYE MMALIZE....!
NI wamoja katika matatizo na shida zao mbalimbali, na pindi mwenzao anapofanyiwa uhalifu ni kama umetukana GESHI zima....!
kwa ile mitaa ambayo wanalea watoto wao ambao ni vibaka na wakwapuaji, na watoto hao pindi wafikishwapo polisi hutolewa kwa hongo. wakimpora MJESHI hapo ndo huchanganywa waliomo na wasiokuwamo.....! (KWA NINI MITAANI TUNALEA VIBAKA?)

...subiri siku yakukute na upewe kipigo bila sababu wewe na mkeo na watoto bila sababu then uje uwatete hapa....hawa inabidi wafuate sheria na hii tabia ipo sana ya wanajeshi kuleta ubabe kwa raia,jeshi linafuga majambazi kwa kuachia tabia kama hizi.
 
KOBA & OTHERS,
Tayari yamenikuta pale Manzese walipofunga mtaa baada ya kibaka mmoja wa maeneo hayo (HASANI BOLI) kumpora mmoja wao
Do you know what happened?
 
Hii sio dalili nzuri ,visa kama hivi vimeanza kushamiri hapa Tz ,sasa fikiria wakazi wa eneo husika huwa na jamaa au ndugu wanaofanya kazi au ni wajeshi wa kambi hizo,sasa ikiwa katika vurumai hizo wajeshi waliokwenda kujichukulia hatua au sheria mikononi mwao ,wamempiga na kumuumiza au kumuua mzazi wa kijana ambae nae ni muajiriwa katika jeshi au kikosi hicho na kwa bahati mbaya au nzuri hakushiriki au pengine yeye amehamishiwa kikazi mkoa mwengine au kambi nyengine ,akisikia kumetokea vulumai lililofanywa na wajeshi kutoka kambi fulani na wamejeluhi raia kibao katika raia waliokufa mmoja ni baba yake au mama yake ,unafikiri itakuwaje hapo ?
 
WANAJESHI SI KAMA POLISI AU TRAFFICK.......!
WANA NIDHAMU, WAPOLE NA PIA SI WAONEAJI KAMA POLISI , MAHAKIMU, TRA, TANESCO, AUX.POLICE N.K...!
DAIMA NI VIGUMU KUSIKIA WAKIONEA MTU YEYOTE.......!
WAKICHOKOZWA hapo ndo utawajua wao ni askari ama la....!
mara nyingi wao si WAANZISHA vurumai, bali kanuni watumiayo ni AKUANZAYE MMALIZE....!
NI wamoja katika matatizo na shida zao mbalimbali, na pindi mwenzao anapofanyiwa uhalifu ni kama umetukana GESHI zima....!
kwa ile mitaa ambayo wanalea watoto wao ambao ni vibaka na wakwapuaji, na watoto hao pindi wafikishwapo polisi hutolewa kwa hongo. wakimpora MJESHI hapo ndo huchanganywa waliomo na wasiokuwamo.....! (KWA NINI MITAANI TUNALEA VIBAKA?)

Mtu akifanya mabaya nawewe unalipiza kwa mabaya?

Sasa hapa anajulikana ni nani mwenye busara?

Waliyofanya wanajeshi na wao kutokana na sheria za nchi nao ni wahalifu, tena uhalifu wenyewe kwa ajili ya mwanamke tu?

Pumbaaaaavu
 
Pdidy,
Siku chache zilizopita tulivyokuwa tunachangia swala la wanajeshi wetu kulipa au kutokulipa nauli za dala dala,niliandika kuwa hawa huwa wanapata mishahara halafu wanaingia baa na kuanza kuwapiga raia. Haijapita wiki moja na tukio hilo likatokea. Wanajeshi hawafai kukaa uraiani, wanajeshi wana maeneo makubwa yaliokuwa wazi, tena mazuri sana katika kila Mkoa. Serikali iwajengee makao yao jeshini wakae pamoja mbali na raia na swala la wao kupanda dala dala halitakuwepo kwa vile watakuwa na mabasi yao wenyewe. Inaonyesha jinsi baadhi ya wanajeshi wetu walivyokuwa hawana nidhamu. Mambo ya kupigania msichana kwenye kumbi za starehe yalishapitwa na wakati na ya kishamba, wapiganie huko, huko kambini kwao.
 
umoja wao ni kama kunguru kasoro kunguru hashambulii ... walishawahi kutembeza mkongoto kule kigamboni miaka ya nyuma ... sidhani kama polisi anaweza kupata na hata kuweza kuwadhibiti hao wakicharukwa
 
umoja wao ni kama kunguru kasoro kunguru hashambulii ... walishawahi kutembeza mkongoto kule kigamboni miaka ya nyuma ... sidhani kama polisi anaweza kupata na hata kuweza kuwadhibiti hao wakicharukwa
Lakini jiulize hivi na wao hawaogopi kufwa ? Maana kama wakishapuliza bhangi zao na kujiona wao ndio wenye haki na nguvu vilevile wakumbuke wananchi nao wanweza kuamua kuzivuta hizo bhangi na wao kujiona ni wanajeshi bora kuliko wao ,ogopa hilo lisije kutokea.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom