Wanajeshi 3 wa Uturuki wameuliwa kwa bahati mbaya katika shambulio la anga lililofanywa na Urusi

mcomunisti halisi

Senior Member
Jan 17, 2017
103
325
Mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Urusi yamewaua kwa bahati mbaya wanajeshi 3 wa Uturuki na kuwajeruhi wengine 11 kaskazini mwa Syria,Waziri wa ulinzi wa Urusi amethibitisha.

Ndege ya kivita ya Urusi ilipiga moja ya jengo ambayo ilikuwa inakaliwa na wanajeshi wa Uturuki.

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonyesha masikitiko yake kwa kutuma rambirambi kwa kumpigia simu Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan.-''katibu wa Kremlin Dmitry Peskov aliuambia mtandao wa Novosti
 

Attachments

  • attorney.jpg
    attorney.jpg
    154.6 KB · Views: 37
Balazo wa Urusi aliuliwa Uturuki kwa bahati mbaya then leo warusi wameua wanajeshi wa Uturuki kwa bahati mbaya.

Hapa pagumu
 
sizani kama ni bahati mbaya...hivi recent uturuki ilitungua ndege ya Urusi na mgogoro ukawa mkubwa. maybe wameamua kulipiza kisasi kimyakimya....
 
haya mambo yapo bt marekan alipostrike wanajesh wa syria kwa bahati mbaya urusi waligoma kukubali wakisema ni makusudi
 
Yeah kama yule rubani na balozi wa Urusi walivyo uawa kwa bahati mbaya.
 
Kuna bahati mbaya kwa maana ya ajali na kuna bahati mbaya ya makusudi. Kwa kawaida kwenye operation za kijeshi lazima kuna line of command na mawasiliano pale kunapotaka kutekelezwa shambilizi hasa la anga. sasa la makusudi huwa kunatolewa onyo kwamba usifanye usifanye usifanye badala yake unafanya kisha unaomba samahani - hiyo sio friendly fire
 
Mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Urusi yamewaua kwa bahati mbaya wanajeshi 3 wa Uturuki na kuwajeruhi wengine 11 kaskazini mwa Syria,Waziri wa ulinzi wa Urusi amethibitisha.

Ndege ya kivita ya Urusi ilipiga moja ya jengo ambayo ilikuwa inakaliwa na wanajeshi wa Uturuki.

Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonyesha masikitiko yake kwa kutuma rambirambi kwa kumpigia simu Rais wa Uturuki Tayyip Erdogan.-''katibu wa Kremlin Dmitry Peskov aliuambia mtandao wa Novosti
Viladmir putin ni mnafiki
 
sizani kama ni bahati mbaya...hivi recent uturuki ilitungua ndege ya Urusi na mgogoro ukawa mkubwa. maybe wameamua kulipiza kisasi kimyakimya....
Itakua ni bahat mbaya kweli... Mbn juzjuz jesh la Nigeria lilistrike wakimbiz wakidhan ni Boko haram
 
Jeshi la Urusi limesema Uturuki ndo waliwapa hizo coordinates za IS wapo eneo Fulani na URusi wakatumia hizohizo kupiga kumbe Uturuki walikosea ndo madhara yake
 
Back
Top Bottom