Wanajamii natangaza nia nataka jimbo la musoma mjini 2015

Kiherehere

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
1,806
621
wanajamii, msoma mjini ni jimbo langu la kuwa mbunge tokea nimezaliwa, na nimezaliwa katika familia ya kisiasa ambayo baba yangu mzazi ALIUWAWA kwa mbinu na ishu za kisiasa

NINAYO DHAMIRA YA KWELI KATIKA KULETA MABADILIKO KATIKA JIMBO HILI.

Sasa ninaomba ushirikiano wenu nichukue jimbo hili. Kwa kuwa KAMPENI ZANGU ZINAANZA RASMI KUANZIA TRH 13/12/2010 - 30/10/2015

Naombeni kura zenu TAFADHALI
 
haujui hata chma gani unatangaza nia kugombea... kama CCM ni sawa tu .... au HR/CUF
 
Huo wivu na tamaa ya madaraka, kijana mdogo toka CDM kakamata jimbo juzi tu na hata bungeni kwenyewe vikao rasmi havijaanza ili tumpime mbunge mpya wewe umeishaanza kutaka kuleta machafuko na hujuma. Tunachagua viongozi ili wawe chachu ya maendeleo na kutupa mawazo mbadala ya kutuletea maendeleo, hatuchagui kutimiza ndoto zao. Hata kama una ndoto hatukuchagui kuwa mbunge wa Musoma mjini kwa kuwa Vincent Nyerere ndo kwanza ameanza kazi, wewe rudi shimoni kwako kaendelee kulala. Acha wivu Tata...
 
ndio maana jina lake kiherehere; upupu atakuwa ccm roho inamuuma na 2015 hata kata zilizobaki tunachukua musoma mjini ni ya Mwalimu nyerere, ni ya chadema maana chadema inamwenzai mwalimu kwa vitendo; dont waste your resources and time
 
Huo wivu na tamaa ya madaraka, kijana mdogo toka CDM kakamata jimbo juzi tu na hata bungeni kwenyewe vikao rasmi havijaanza ili tumpime mbunge mpya wewe umeishaanza kutaka kuleta machafuko na hujuma. Tunachagua viongozi ili wawe chachu ya maendeleo na kutupa mawazo mbadala ya kutuletea maendeleo, hatuchagui kutimiza ndoto zao. Hata kama una ndoto hatukuchagui kuwa mbunge wa Musoma mjini kwa kuwa Vincent Nyerere ndo kwanza ameanza kazi, wewe rudi shimoni kwako kaendelee kulala. Acha wivu Tata...

Ukwilokwitanga, siyo vwivu kaka, na tusiwe na imani kuwa KUTANGAZA NIA, ni kumuonea wivu aliyepo. Tukumbuke mambo ya KUONA KWAMBA FLANI ANAONEWA WIVU ndio kumeleta maneno kuwa JIMBO NI FULANI. Monduli,mtera nk. Nategemea kuwa nitapata CHALLENGE kutoka kwa wanajamii Ili waweze kujua ni mtu makini kiasi gani au dhaifu kiasi gani katika suala nililoliweka hapa. Naomba challenge siyo kuvunjwa moyo...
 
Nikumbushe nia yako ikifika 2014. Nahisi nitakuwa nishaisahau.

Harakati za mambo ya msingi huwa zinaanza kwa muda mrefu.Kwa hiyo tegemea hii post kuwepo kwa kipindi chote.Pia nategemea challenege toka kwako na support tokea kwako. Tuko pamoja Hsninyo
 
Muda bado, elekeza nguvu zako katika kushirikiana na mbunge wako

Jojipoji, hakuna muda wa kutosha katika jambo linalopaswa kupangwa kwa kina. Hata ulipoanza kidato cha kwanza kama mtu makini ULIANZA KUSOMA KWA BIDII na ukijua wazi kuwa mtihani wa taifa UNGEUFANYA BAADA YA MIAKA MINNE.tutegemee mipango iliyo bora, na ninategemea mawazo yako JOJIIII. Tafadhali wasilisha.
 
wanajamii, msoma mjini ni jimbo langu la kuwa mbunge tokea nimezaliwa, na nimezaliwa katika familia ya kisiasa ambayo baba yangu mzazi ALIUWAWA kwa mbinu na ishu za kisiasa

NINAYO DHAMIRA YA KWELI KATIKA KULETA MABADILIKO KATIKA JIMBO HILI.

Sasa ninaomba ushirikiano wenu nichukue jimbo hili. Kwa kuwa KAMPENI ZANGU ZINAANZA RASMI KUANZIA TRH 13/12/2010 - 30/10/2015

Naombeni kura zenu TAFADHALI

nyie ndiyo aina ya watu munaotoa pongezi kwa baraza la mawaziri hata kabla hawajaanza kazi.

vincent nyerere hajamaliza hata mwezi ulishaanza kuwaza kugombea.

una uchu wa madaraka.

utafulia kisiasa.

soon
 
wanajamii, msoma mjini ni jimbo langu la kuwa mbunge tokea nimezaliwa, na nimezaliwa katika familia ya kisiasa ambayo baba yangu mzazi ALIUWAWA kwa mbinu na ishu za kisiasa

NINAYO DHAMIRA YA KWELI KATIKA KULETA MABADILIKO KATIKA JIMBO HILI.

Sasa ninaomba ushirikiano wenu nichukue jimbo hili. Kwa kuwa KAMPENI ZANGU ZINAANZA RASMI KUANZIA TRH 13/12/2010 - 30/10/2015

Naombeni kura zenu TAFADHALI
kwa hiyo weye unagombea ubunge kwa sababu unatokea familia ya siasa tu na unafikiri hicho ni kigezo tosha na pili kwa ajili ya kulipiza kisasi cha babayo kuuliwa kisiasa.... heheh kweli tuna wanasiasa! na mie Geza, kwetu tusio na historia ya siasa nitangaze nia kivipi?
 
hivi haulewi lugha... kwa chama gani ????

Chama hakina tija, suala hapa chama kitakuja bbaadae. Cha msingi LAT, ni kuwafikia wapiga kura ILA MAPENZI YANGU YAPO kwa CHADEMA lakini hata kama hawatakuwa na dhamira ya kunisimamisha, ni kuangalia JE ninafit???? Siyo wote wanaogombea kwa kupitia chama flani, WANYAYO MAPENZI NACHO ila WANATUMIA TIKETI kuingia kupeleka mawazo yao. So chama kinafuata LAT baadae, naomba Challenge please au kama jibu halijatosheleza. Nawasilisha.
 
kwa hiyo weye unagombea ubunge kwa sababu unatokea familia ya siasa tu na unafikiri hicho ni kigezo tosha na pili kwa ajili ya kulipiza kisasi cha babayo kuuliwa kisiasa.... heheh kweli tuna wanasiasa! na mie Geza, kwetu tusio na historia ya siasa nitangaze nia kivipi?

Geza, SIYO KULIPIZA KISASI LAH!!!!! ninayo fikra hiyo muda mrefu, so nimeitoa KAMA HOJA nikijua wazi nitapata challenege kama uliyoileta. familia ya kisiasa ambayo MTU ANAWEZA KUSIMAMA PEKE YAKE ni nzuri zaidi KULIKO MWANAFALIA YA KISIASA ANAYEBEBWA. ni tofauti kubwa saaana kati ya Nape v/s Ridhwani Vinceny Nyerere v/s Karume raisi aliyemaliza muda wake, Jenista Muhagama v/s Vita Kawawa so pia utambilisho ni mzuri na haijarishi kuwa ni njia IPI inatumika so suala hili lilikuwa kama HOJA. Nimewasilisha GEZA
 
kwani kuzaliwa katika familia ya kisiasa nayo ni sera?

mpaka hapo umeshindwa ubunge.

fikiria kazi nyingine.

Ng'wanangwa kuzaliwa FAMILIA ya kisiasa haimaanishi kama ni hoja!!! kwanza swali kwako kaka, je UNAJUA siasa ninayozungumzia ni katika kiwango kipi?? Na shuri lililopo jukwaani kwa wanajamii, sio siasa ZA VYAMA NDO SIASA..... Sijaijadili siasa kama mfumo wa utegemezi wa vyama katika familia niliyoisema, HAPO ULIPO WEWE NI MWANASIASA lakini sio katika mfumo tuliouzoea , kwa imani yangu UNAWEZA KUICHANGANUA SIASA na ukawa mwanasiasa LAKINI siyo katika mfumo wa vyama. Kwa watu walio wengi kwa hapa Tz, TUNAAMINI KATIKA PARTIES POLITICS, lakini ipo individual politics ambayo ipo kwa mtu mmoja mmoja na mfano mzuri ni WEWE Ng'wangwa.
 
Ng'wanangwa kuzalifa FAMUILIA ya kisiasa haimaanishi kama ni hoja!!! kwanza swali kwako kaka, je UNAJUA siasa ninayozungumzia ni katika kiwango kipi?? Na shuri sio siasa ZA VYAMA NDO SIASA..... Sijaijadili siasa kama siasa ya vyama, HAPO ULIPO WEWE NI MWANASIASA lakini sio katika mfumo tuliouzoea. Kwa watu walio wengi kwa hapa Tz, TUNAAMINI KATIKA PARTIES POLITICS, lakini ipo individua politics na mfano mzuri ni WEWE Ng'wangwa.

wewe kweli kiherehere.

umenichekesha na maneno yako. kwamba na mimi ni mwanasiasa. evidensi?

kwa hiyo utakuwa mgombea binafsi? haipo kwenye katiba. sahau kuwa mbunge 2015.
 
Back
Top Bottom