Wanahisa wa DSE Kutopata gawio

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Kuna tetesi za ndani kabisa nimezisikia kutoka soko la hisa la dar es salaam (DSE) kwamba wanahisa wake hawatapata gawio mwishoni mwa mwaka wa kiserikali unaoisha mwezi wa sita tarehe 30. Hii ni kutokana na mauzo kidogo ya hisa katika soko hilo, kutopata gawio itakuwa pigo kubwa sana kwa wanahisa. Tukumbuke kuwa ni mwaka jana tu dse waliingia katika soko la hisa na hatujui undani kabisa. Sasa kama uliwekeza basi utatoka kappa. Sababu nyingine inayochangia kutopata gawio ni kufanya vibaya kwa hisa za voda ambapo mpaka sasa wanashindwa kuziweka sokoni kwani ziliuzwa kwa asilimia 40 tu huku 60 zikikosa mnunuaji. Kwakweli hisa c eneo la kuwekeza hasa katika nchi ya KIMAKANIKIA kama Tanzania.
 
NDO MANA TUNAAMBIWA KILA SIKU KUWA BIASHARA YA HISA INA CHANGAMOTO SANA
 
Unajua unachokiongea lakini au umekurupuka.?unaijua DSE ni nin.? Eti DSE wameingia mwaka jana kwenye soko la hisa duuuh
 
Pamoja na kukopa hela kununua hisa lakini hamna gawio. Hii ni hasara ambayo haikubaliki
 
Hisa kanunue Marekani tena uwe na hela ambazo huhitaji zitumia
Kwa hapa Tanzania bora ukauze nyanya tu
 
Kwanza mwenye ujuzi na faida za hisa gawio lake linakuwaje maana sielewi namna ya mgawanyo wa faida
 
Back
Top Bottom