Wanaharakati watishia kuzuia uchaguzi 2010

Kubwajinga

JF-Expert Member
Jan 23, 2008
2,194
297
Wanaharakati watishia kuzuia uchaguzi 2010

Na Richard Makore; 17th February 2010


Kiwanga(2).jpg

Mkurugenzi wa LHRC, Francis Kiwanga


Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kinatarajia kwenda mahakamani kusimamisha Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba, 2010 ikiwa serikali itakaidi kubadilisha vipengele vya sheria na kuweka mazingira mazuri ya kuruhusu mgombea binafsi.

Kadhalika, kituo hicho kimekerwa na kauli ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), Philip Marmo, kwa kutangaza kuwa serikali haitambui kuwepo mgombea binafsi.

Msimamo huo wa LHRC ulitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wake mkuu, Francis Kiwanga, alipozungumza na waandishi wa habari.

Alisema Mahakama Kuu ilishatoa hukumu mwaka 2006 na kutamka kuwa mgombea binafsi anaruhusiwa na kwamba kitendo cha serikali kudharau amri hiyo ni kosa kisheria.

Alisema ndani ya miezi minne lazima serikali ihakikishe inarekebisha vipengele vya sheria vinginevyo watakimbilia mahakamani ili kupinga uchaguzi usifanyike bila mgombea binafsi kushiriki.

Alisema kuna sheria nyingi zilizowahi kufanyiwa marekebisho na kupitishwa na Bunge katika kipindi kifupi hivyo hatua ya kuruhusu mgombea binafsi inawezekana.

Alitolea mfano wa sheria ya uchaguzi ambayo ilijadiliwa na wabunge na kupitishwa ndani ya siku mbili.

Alisema hukumu ya Mahakama Kuu haijatenguliwa na Mahakama ya Rufaa kama alivyosema Jaji Mkuu wa Tanzania, Augustino Ramadhani hivi karibuni.

Kiwanga alisema serikali inakataa kwa makusudi amri halali ya Mahakama na kwamba ubabe wake huo unakinzana na kifungu cha 14(3) cha Sheria ya utekelezaji wa haki za msingi za binadamu.

CHANZO: NIPASHE
 
Wazo zuri la kupigania. Tuombe Mungu wasije wakawa ni vibaraka wa JK.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom