Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,474
- 39,987
Sielewi kwanini wanaharakati wanataka kuandamana kulilalamikia Bunge kuhusu suala la Richmond. Hadi hivi sasa Bunge na wabunge wamefanya kazi yao vizuri na kwa umahiri mkubwa. Wameenda hadi pale ambapo kimadaraka wamefikia mwisho wao. Sehemu inayofuatia ni sehemu ya Rais.
Ni sawasawa watu wanaofanya kazi kwa kupokezana; unalima kuanzia hapa hadi pale, halafu wengine wanachukua kuanzia hapa hadi pale hadi shamba linakwisha. Tangu mwanzo wa sakata la Richmond ni Bunge pekee ambalo limekuwa likilima na kulima weee huku Rais akiangalia pembeni kana kwamba shamba halimhusu!
Sasa wabunge wamefikia mahali na kusema tumelima tayari na tumejitahidi kulima wewe sasa tulipofikia panahitaji Rais naye alime.
Kinachonishangaza wanaharakati wanataka wabunge waendelee kulima tu hadi mwisho na wapande, kutia mbolea na kupalilia. Mwisho wake Rais aje avune na kupewa sifa jinsi shamba lilivyopendeza. Halatu atapita na kutaka kuonekana jinsi gani alisaidia kulima!!
Hivyo, maandamano dhidi ya Bunge na wabunge wapiganaji hayana maana kwani hadi hivi sasa hayajaangalia ukweli. Ukweli ni kwamba Bunge limefanya kazi yake na wanastahili maandamano ya kupongezwa. Anayehitaji kushinikizwa ni Rais kwani Bunge limemuachia kipande chake cha kulima.
Kipande hicho:
a. Kumuwajibisha Dr. Hosea wa PCCB
b. Kuhakikisha bilioni 30 walizopakuliwa Dowans/ Richmond zinarudishwa
c. Kutaifisha mitambo ya Dowans
d. Kuwawajibisha wengine ambao ameachiwa na Bunge kuwawajibisha
e. Kuliomba msamaha taifa kwa uzembe uliotokea ndani ya serikali yake na kuwapotezea muda wananchi.
Hizo ndizo sababu kiasi za kufanya maandamano; nje ya hapo ni kutaka kuandamana ili waoneshwe mwanasesere!
Ni sawasawa watu wanaofanya kazi kwa kupokezana; unalima kuanzia hapa hadi pale, halafu wengine wanachukua kuanzia hapa hadi pale hadi shamba linakwisha. Tangu mwanzo wa sakata la Richmond ni Bunge pekee ambalo limekuwa likilima na kulima weee huku Rais akiangalia pembeni kana kwamba shamba halimhusu!
Sasa wabunge wamefikia mahali na kusema tumelima tayari na tumejitahidi kulima wewe sasa tulipofikia panahitaji Rais naye alime.
Kinachonishangaza wanaharakati wanataka wabunge waendelee kulima tu hadi mwisho na wapande, kutia mbolea na kupalilia. Mwisho wake Rais aje avune na kupewa sifa jinsi shamba lilivyopendeza. Halatu atapita na kutaka kuonekana jinsi gani alisaidia kulima!!
Hivyo, maandamano dhidi ya Bunge na wabunge wapiganaji hayana maana kwani hadi hivi sasa hayajaangalia ukweli. Ukweli ni kwamba Bunge limefanya kazi yake na wanastahili maandamano ya kupongezwa. Anayehitaji kushinikizwa ni Rais kwani Bunge limemuachia kipande chake cha kulima.
Kipande hicho:
a. Kumuwajibisha Dr. Hosea wa PCCB
b. Kuhakikisha bilioni 30 walizopakuliwa Dowans/ Richmond zinarudishwa
c. Kutaifisha mitambo ya Dowans
d. Kuwawajibisha wengine ambao ameachiwa na Bunge kuwawajibisha
e. Kuliomba msamaha taifa kwa uzembe uliotokea ndani ya serikali yake na kuwapotezea muda wananchi.
Hizo ndizo sababu kiasi za kufanya maandamano; nje ya hapo ni kutaka kuandamana ili waoneshwe mwanasesere!