Wanaharakati wa tanzania ni hatari kwa usalama wa nchi

Tuliporuhusu shetani awe MHISANI wetu, MFADHILI wetu, MSHAURI wetu na MWEKEZAJI wetu matokeo ni kama yanavyoonekana! Hizi ni rasharasha tu MVUA haijanyesha. Sehemu ya MUNGU akae MUNGU na si mzungu!
 
wanaharakati wanatumia mabilioni kwenye warsha na makongamano kwanini wasitumie fedha hizo wanazopata kwa wafadhili kuchangia kuboresha huduma za afya kama kweli ni wazalendo wa kweli. Mimi nipo bongo na ni mhanga wa mgomo wa madaktari

umevurugwa ww
 
umezungumza hoja ya msingi kabisa,kwa mgomo huu wa hawa wauwaji hawana tofauti na vikundi vyote vya kigaidi ulimwengumi kwani hutumia hujuma kwa kuripua mabomu na kuuwa wananchi wasio na hatia ili waishinikize serikali kukubali matakwa yao!
na hawa hutumia hujuma kwa kuuwa wagonjwa!

Na wanaokufa kwa kukosa madawa na vifaa nani muuaji!
 
Kwa kutishia au kuondoa uhai wa binadamu kushinikiza maslahi yao ni nguzo ya ugaidi
 
Meneja na sio director wa tanapa analipwa tsh 4m daktari kulipwa sh 3.5 kuna tatizo gani?
 
Meneja na sio director wa tanapa analipwa tsh 4m daktari kulipwa sh 3.5 kuna tatizo gani?

1) Mameneja wa Tanapa wapo wangapi Tanzania hii na madaktari wapo wangapi?

2) Hujui kuwa baadhi ya hizo fedha wanazolipwa madaktari zinatokea hukohuko TANAPA? kwenye wazalishaji wachache?

3) Madaktari wa Tanzania wanaoona kuwa hapa hawalipwi vya kutosha wamepewa ruksa kwenda kufanya kazi nje ya Tanzania na kujipatia kipato cha ziada. Jee, hilo hulijui?

4) Daktari wa Tanzania atuoneshe mapato yake kamili ya mwaka mzima, kuanzia allowance za vikao, mikutano, pesa wanazopokea kwenye ma NGO wakiwaandikia paper zao, biashara binafsi, malipo ya private hospitals, halafu tulinganishie na za huyo meneja wa TANAPA. Kumbuka kipato cha madaktari hakipo kwenye mshahara tu.
 
Osama aliua raia wa marekani ili kushinikiza marekani itoke katika ardhi za kiislamu.....madaktari wanaua wagonjwa wakidai mshahara wa milioni tatu kwa daktari anayeanza kazi leo.....ILA NA NYIE BUNGE MNACHOCHOEA KWA KUJIONGEZEA VIPATO ....!
 
'non-profit' smart-assing is a new threat to our nation, no doubt about that..serikali itupie jicho lake huku nako, hakuna haja ya kuwapa free-pass watu wasioleta input kwa jamii..sheria kali ya kuwa-regulate itungwe..wengine wanaandika mapropozo feki na kuombea fedha kwa madhumuni mbalimbali na kuishia kwene matumbo yao. time to act is NOW.
 
Osama aliua raia wa marekani ili kushinikiza marekani itoke katika ardhi za kiislamu.....madaktari wanaua wagonjwa wakidai mshahara wa milioni tatu kwa daktari anayeanza kazi leo.....ILA NA NYIE BUNGE MNACHOCHOEA KWA KUJIONGEZEA VIPATO ....!

uko sawa kabisa mkuu. Kila upande unawajibika ila kushinikiza jambo kwa kutishia uhai ni ugaidi
 
Kuna watu humu ndani sijui wametumwa au hawana ndugu wanaoumwa!msipende kushangilia mambo tu swala la migomo ya madaktari kunawatu wanakufa kwny mahospital huu mgomo hauna maana na hawa nanaoitwa wanaharakati ndio chanzo wao kaziyao kuchochea mambo tu tusielewane mujue wanalipwa wale na wanawafazili ulaya uko hawafai hata kidogo ningekuwa na uwezo ningewakamata afu NIKAWAULIMBOKA.
 
mnyampaa now you are talking......na pia tukichukua definition ya TERRORISM/UGAIDI ni hali ya kuua,kuogofya,kuharibu wasio na hatia ili kupata malengo fulani ya ki-maslahi au kisiasa kutoka serikalini ama eneo fulani!

Poor and innocent guy yet ignorant ina maana kwa mtazamo wako na hiyo definition hata walimu wakija kugoma ni magaidi nani gaidi kati ya serikali na wanaodai haki yao
 
Kwa hiyo na yule aliyeshindwa kutibiwa Bombo kwa hospitali kukosa vifaa vya xray, hilo nalo ni madaktari?? Mbona umeegemea upande mmoja sana?
 
Adui yetu ni serikali na wala sio wanaharakati na madaktari! Laiti kama ingekuwa ni sheria kuwa kiongozi yeyote haruhusiwi kutibiwa nje ya nchi na ni shurti atibiwe kwenye hospitali za serikali......mngeshaona mabadiliko!
 
wanaopata tabu ni wananchi masikini,nao wananchi masikini ni dhaifu kwa kosa la kuchagua viongozi dhaifu
 
Ulimsikia uamsho akimwambia daktari agome?

Wacha wewe, huu ni ugaidi na hakuna haki ya kwanza duniani ila haki ya kuishi na madaktari wanafiki wachache wanajifanya wao mungu watu kuwa wanaweza kuwaweka rehani wagonjwa na kutumia maradhi yao kujipatia maslahi yao. Hao malipo yao ni hapa hapa tena hayachukui muda mrefu.

Msiwakandamize madaktari eti kisa wapo kwenye sekta muhimu na kuwaacha watu walosimama mbele ya kadamnasi tena kwa kiburi kabisa na kusema liwalo na liwe kwa vile tu wao hawatoathirika na huo mgomo!! Wagonjwa hawajaanza kufa kwenye mgomo tu, wengi wamefia njiani kwa kukosa facilities zikiwemo ambulance na barabara kuwa mbovu ilihali hao hao wanahusika na huduma za wananchi wao wanaongezewa posho! Wengi wamekufa kwa kukosa madawa hospitalini na vifaa vya kitabibu huku bajeti za kwenda kutibu viongozi nje zikiongezeka.......mbona hayo hamuyaoni?? Ndo kusema ni halali mwananchi kufa kwa kiburi cha serikali? Acheni masikhara.......
 
Back
Top Bottom