Mnyampaa
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 244
- 58
Kutokana na mchango wao katika kushawishi na kushabikia mgomo wa madaktari na kuushawishi umma kuamini kuwa vurugu na migomo ndio njia pekee ya kudai maslahi nadiriki kusema kundi hili la jamii ni hatari kama vikundi vya kigaidi. Nielewavyo mimi vikundi hivi vinapaswa kuishia kutoa elimu na kuishauri au kuishawishi serikali au kikundi/taasisi nyinginezo kutimiza wajibu wake na si kuegemea upande mmoja. Kwa hili la mgomo wa madaktari nilitegemea wanaharakati kuwa wa kwanza hata kabla ya mgomo kuishawishi serikali kuboresha huduma za afya na si kudandia mgomo. Ninavyofahamu hali mbaya ya huduma za afya si jambo jipya hivyo walipaswa kuingilia kati kabla ya mgomo. Iwapo wao ni watetezi wa haki za watanzania wasingeshabikia mgomo wa madaktari kwani ni mgomo umechangia watanzania mamilioni kukosa haki zao za msingi kwa wanaharakati kushabikia mgomo na kusahau mateso ya wananchi walio wengi. Wanaharakati wanapaswa kupima kati ya haki ya msingi ya kuishi ya watanzania na maslahi ya kuishi kifahari ya madaktari.