Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Wanaharakati: Tanesco isiikatie rufaa Dowans | Send to a friend |
Tuesday, 11 October 2011 20:30 |
Geofrey Nyangoro BAADHI ya wanaharakati katika Jiji la Dar es Salaam, wamelitaka Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), liache mpango wa kukata rufaa ya kupinga tuzo ya Kampuni ya kufua umeme ya Dowans na kwamba suala hilo sasa litaamuliwa na wananchi.Wanaharakati hao pia wameitaka serikali ieleze sababu za kuhamisha mkataba wa Richmond kwenda Dowans. Akizungumzia mchakato huo wa rufaa ya dhidi ya Dowans, Mratibu wa Masuala ya Bunge wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Albania Marcossy, alisema kitendo cha Tanesco kutaka kukata rufaa kupinga tuzo ya mabilioni ya fedha kwa Dowans ni cha kusitajabisha hasa ikizingatiwa kuwa suala hilo lilipofikia haliwezi kuamriwa kwa kutumia sheria za nchi. Nimesikia leo (jana) Tanesco inatarajia kuwasilisha katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Dar es Salaam, ombi la kutaka kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa kuridhia malipo kwa Dowans. Hiki ni kitendo cha kustaajabisha, hivi ni kweli kuwa hadi leo Tanesco hajui kuwa kwa mjibu wa mkataba huo, baada ya hukumu kutolewa na tuzo kusajiliwa katika Mahakama kuu ya hapa nchini ,hakuna kukata rufaa, alisema Marcossy. Alisema, kwa mujibu wa sheria zilizopo suala hilo limefikia mwisho na hakuna mahakama inayoweza kubatilisha. Ndio sababu sisi kwa kutumia katiba ya nchi Ibara ya 27 (1) tunawahamasisha Watanzania ambao ndio wa miliki wa rasmali za nchi kujitokeza kwa wingi kutimiza wajibu wao wa kulinda rasmali zao zisiporwe,alisema. Kuhusu maadhimisho ya siku ya kifo cha Baba wa Taifa , Mwalimu Nyerere, wanaharakati wamewataka Watanzania kuingia katika nyumba za ibada kuliombea taifa ili Mungu awajalie uzalendo na ujasir wa kutetea rasimali za nchi yao kama alivyofanya kiongozi huyo. Mkurugenzi wa Shirila la Sikaka, Irenei Kiria, alisema katika kipindi hicho wanachi watatakiwa kuvaa nguo nyeusi na kujifunga bendera ya taifa kichwani kuashiria maombolezo.Alisema mavazi hayo yanapaswa kulivaliwa kuanzia Oktoba 14 siku aliyofariki muasisi huyo hadi Oktoba 23 alipozikwa. Tuvae nguo nyeusi za maombelezo tangu siku aliyofariki hadi kuzikwa kwake, tuingie kwenye nyumba za ibada kumuombea na kukumbuka msimamo wake wa kupinga vitendo vya kifisadi na matumizi mabaya ya rasmali za taifa,alisema kiria.Wanaharakati hao pia wameitaka serikali kutoa maelezo ya kina kuhusu sababu ya kupuuza ushauri wa kisheria wa kuvunja mkataba wa Kampuni ya kufua umeme ya Richmond. Kwa mjibu wa washauri wa Kimarekeni Hunton &Williams LLP, wakati Tanesco inaingia mkataba na Richmond. Kampuni hiyo haikuwa imesajiliwa achilia mbali kuwa haikuwa na uwezo wa kutekeleza majukumu yake chini ya mkataba,alisema Kiria. |