Wanaharakati kuandamana kupinga maamuzi ya Bunge kuhusu Richmond

Luteni

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
2,274
301
(kutoka Gazeti la Habari Leo)

WANAHARAKATI wa usawa wa jinsia, haki za binadamu na demokrasia, wamedai Bunge limeshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuisimamia Serikali kwa kuridhia kuzika masuala ya Richmond na Kiwira katika mkutano wake uliomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma.

Muungano wa Asasi za Kiraia zinazotetea Usawa wa Jinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo ya Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct), umetoa tamko ambalo pamoja na mambo mengine, linawataka wanaharakati hao waandamane kwa lengo la kuonesha kutoridhishwa na Bunge hilo.

Katika kile kinachoonesha ni kuibua mjadala na mgongano wa kimawazo kati yao na wabunge, wanaharakati hao wamesisitiza kwamba uamuzi wa kulinyooshea Bunge kidole, hauwezi kuwa mgogoro, kwani chombo hicho hakiko juu ya wananchi.

“Bunge haliko juu ya wananchi. Kimsingi wananchi tunataka. Huu si mgogoro, huwezi kuwa na mgogoro na mtu unayemwajibisha,” alisema mwakilishi wa Shirika la Fordia, Buberwa Kaiza na kusisitiza kwamba tamko hilo halitokani na kuwaridhisha wafadhili kama ambavyo imekuwa ikidhaniwa.

Wanaharakati hao katika tamko lao lililosomwa jana Dar es Salaam na wawakilishi wanne kwa nyakati tofauti, zaidi ya kusema Bunge halikutimiza wajibu katika taarifa zilizofikishwa katika mkutano wake wa 18, hawakuweka bayana kasoro za Bunge katika kushughulikia masuala ya Richmond, TICTS, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu ulioathiri binadamu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Loliondo.

Baadhi ya wanaharakati waliwasuta wabunge waliosadikiwa kuwa vinara wa kupambana na ufisadi bungeni, kuwa wameonesha kwamba kauli zao zilikuwa za kisanii, kwa kuwa wameshindwa kusimama kidete hadi mwisho kuhakikisha Serikali inawajibika si tu kwa Richmond, bali pia kwa kashfa zingine likiwamo suala la Kiwira.

Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananilea Nkya, akichangia tamko hilo, alisema, “wabunge wangeendelea kusimama kidete. Hata kama wangefukuzwa chama, ingesaidia. Lakini hakuna aliyesimama hadi mwisho…hatulilii kwenda bungeni.”

Akisoma sehemu ya kwanza ya tamko hilo lililosainiwa na asasi hizo zinazounda FemAct, pamoja na taasisi nyingine likiwamo Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kaiza alisema mfumo mbaya wa madaraka na uwajibikaji kati ya Serikali na Bunge, unaruhusu maslahi ya chama tawala kuchukua hatamu kuliko ya wananchi.

Wanaharakati hao walitaka Baraza la Mawaziri lisitokane na wabunge. “Mfumo huu umedhoofisha demokrasia shirikishi ambayo ingewezesha wananchi na makundi yao kuwa na uwezo wa kuliwajibisha Bunge, wabunge na madiwani,” alisema Kaiza.

Kaiza ambaye hata hivyo alikiri kwamba hata katika asasi za kiraia, wapo wanafiki wanaonyooshea vidole Serikali bila wao kumaanisha, alisisitiza kwamba tabia hiyo ni ya mtu mmoja mmoja.

“Wapo maprofesa wanaochoka kuandika, wanaamua kwenda bungeni kudai posho, hata wanaharakati wapo wanaochoka. Huyo aliyechoka amepotea tunamwacha, lakini huo uangaliwe kama udhaifu wa mtu na si wanaharakati wote,” alisema.

Alisema katika muktadha wa mfumo unaolimbikiza madaraka kwa walio wachache na kuvuruga uwajibikaji, ni vigumu kwa Bunge kuiwajibisha Serikali kama inavyotazamiwa.

“Ndiyo maana Bunge limefunika kisiasa kashfa za Richmond, Kiwira, TRL na TICTS, ingawa kashfa hizi zimelisababishia Taifa hasara kubwa ya mabilioni ya fedha na madhara makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwafanya wawe masikini na fukara zaidi,” alidai Kaiza.

Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Usu Malya, alidai kuwa Sh bilioni 173 zilizopotea katika kashfa ya Richmond zingewezesha kujenga nyumba 19,211 za walimu wa shule za msingi nchi nzima. Mwakilishi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga, alisisitiza kwamba utawala uliopo haukidhi haja ya kusimamia rasilimali za nchi.

Alisema panahitajika mapinduzi makubwa na ya haraka katika mfumo wa uwajibikaji na uongozi, muundo wa sera za utawala, siasa na uchumi.

Kiwanga alisema, “Uchaguzi Mkuu wa 2010 ni fursa pekee kwa wananchi kufanya mapinduzi yanayotarajiwa. Wabunge wetu wa sasa wameshindwa kutetea na kulinda haki na maslahi ya Taifa na wananchi.”

Ingawa Spika Samuel Sitta hakupatikana jana kuzungumzia shutuma za wanaharakati, katika mkutano wa 18, Bunge lilipokea na kuridhia taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu mkataba baina ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni ya Richmond Development Company (LLC) pamoja na mkataba wa ubinafsishwaji wa mgodi wa makaa ya mawe, Kiwira.

Kuhusu North Mara, baada ya kupokea taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Serikali ilielekezwa kuchunguza haraka ili walioathirika na kemikali za sumu walipwe fidia.

Taarifa ya Loliondo haikufikishwa bungeni wakati TICTS na TRL hazikujadiliwa kutokana na Bunge kubaini kwamba hakukuwa na utekelezaji uliofanywa na Serikali.
 
Kiwanga alisema, "Uchaguzi Mkuu wa 2010 ni fursa pekee kwa wananchi kufanya mapinduzi yanayotarajiwa. Wabunge wetu wa sasa wameshindwa kutetea na kulinda haki na maslahi ya Taifa na wananchi."

I see we see eye to eye.....Haya tuone ni kwavipi wata wamobilise wananchi ili waseme NO to mafisadi dis coming election.
 
Wanaharakati waliponda Bunge
Imeandikwa na Stella Nyemenohi; Tarehe: 17th February 2010

Habarileo

WANAHARAKATI wa usawa wa jinsia, haki za binadamu na demokrasia, wamedai Bunge limeshindwa kutekeleza wajibu wake wa kuisimamia Serikali kwa kuridhia kuzika masuala ya Richmond na Kiwira katika mkutano wake uliomalizika wiki iliyopita mjini Dodoma.

Muungano wa Asasi za Kiraia zinazotetea Usawa wa Jinsia, Haki za Binadamu, Maendeleo ya Ukombozi wa Wanawake Kimapinduzi (FemAct), umetoa tamko ambalo pamoja na mambo mengine, linawataka wanaharakati hao waandamane kwa lengo la kuonesha kutoridhishwa na Bunge hilo.

Katika kile kinachoonesha ni kuibua mjadala na mgongano wa kimawazo kati yao na wabunge, wanaharakati hao wamesisitiza kwamba uamuzi wa kulinyooshea Bunge kidole, hauwezi kuwa mgogoro, kwani chombo hicho hakiko juu ya wananchi.

“Bunge haliko juu ya wananchi. Kimsingi wananchi tunataka. Huu si mgogoro, huwezi kuwa na mgogoro na mtu unayemwajibisha,” alisema mwakilishi wa Shirika la Fordia, Buberwa Kaiza na kusisitiza kwamba tamko hilo halitokani na kuwaridhisha wafadhili kama ambavyo imekuwa ikidhaniwa.

Wanaharakati hao katika tamko lao lililosomwa jana Dar es Salaam na wawakilishi wanne kwa nyakati tofauti, zaidi ya kusema Bunge halikutimiza wajibu katika taarifa zilizofikishwa katika mkutano wake wa 18, hawakuweka bayana kasoro za Bunge katika kushughulikia masuala ya Richmond, TICTS, TRL, taarifa ya uchafuzi wa mazingira kwa kemikali za sumu ulioathiri binadamu katika mgodi wa North Mara na ukiukwaji wa haki za binadamu katika eneo la Loliondo.

Baadhi ya wanaharakati waliwasuta wabunge waliosadikiwa kuwa vinara wa kupambana na ufisadi bungeni, kuwa wameonesha kwamba kauli zao zilikuwa za kisanii, kwa kuwa wameshindwa kusimama kidete hadi mwisho kuhakikisha Serikali inawajibika si tu kwa Richmond, bali pia kwa kashfa zingine likiwamo suala la Kiwira.

Mkurugenzi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa), Ananilea Nkya, akichangia tamko hilo, alisema, “wabunge wangeendelea kusimama kidete. Hata kama wangefukuzwa chama, ingesaidia. Lakini hakuna aliyesimama hadi mwisho…hatulilii kwenda bungeni.”

Akisoma sehemu ya kwanza ya tamko hilo lililosainiwa na asasi hizo zinazounda FemAct, pamoja na taasisi nyingine likiwamo Baraza la Habari Tanzania (MCT), Kaiza alisema mfumo mbaya wa madaraka na uwajibikaji kati ya Serikali na Bunge, unaruhusu maslahi ya chama tawala kuchukua hatamu kuliko ya wananchi.

Wanaharakati hao walitaka Baraza la Mawaziri lisitokane na wabunge. “Mfumo huu umedhoofisha demokrasia shirikishi ambayo ingewezesha wananchi na makundi yao kuwa na uwezo wa kuliwajibisha Bunge, wabunge na madiwani,” alisema Kaiza.

Kaiza ambaye hata hivyo alikiri kwamba hata katika asasi za kiraia, wapo wanafiki wanaonyooshea vidole Serikali bila wao kumaanisha, alisisitiza kwamba tabia hiyo ni ya mtu mmoja mmoja.

“Wapo maprofesa wanaochoka kuandika, wanaamua kwenda bungeni kudai posho, hata wanaharakati wapo wanaochoka. Huyo aliyechoka amepotea tunamwacha, lakini huo uangaliwe kama udhaifu wa mtu na si wanaharakati wote,” alisema.

Alisema katika muktadha wa mfumo unaolimbikiza madaraka kwa walio wachache na kuvuruga uwajibikaji, ni vigumu kwa Bunge kuiwajibisha Serikali kama inavyotazamiwa.

“Ndiyo maana Bunge limefunika kisiasa kashfa za Richmond, Kiwira, TRL na TICTS, ingawa kashfa hizi zimelisababishia Taifa hasara kubwa ya mabilioni ya fedha na madhara makubwa kwa wananchi ikiwa ni pamoja na kuwafanya wawe masikini na fukara zaidi,” alidai Kaiza.

Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Usu Malya, alidai kuwa Sh bilioni 173 zilizopotea katika kashfa ya Richmond zingewezesha kujenga nyumba 19,211 za walimu wa shule za msingi nchi nzima. Mwakilishi wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Francis Kiwanga, alisisitiza kwamba utawala uliopo haukidhi haja ya kusimamia rasilimali za nchi.

Alisema panahitajika mapinduzi makubwa na ya haraka katika mfumo wa uwajibikaji na uongozi, muundo wa sera za utawala, siasa na uchumi.

Kiwanga alisema, “Uchaguzi Mkuu wa 2010 ni fursa pekee kwa wananchi kufanya mapinduzi yanayotarajiwa. Wabunge wetu wa sasa wameshindwa kutetea na kulinda haki na maslahi ya Taifa na wananchi.”

Ingawa Spika Samuel Sitta hakupatikana jana kuzungumzia shutuma za wanaharakati, katika mkutano wa 18, Bunge lilipokea na kuridhia taarifa ya Serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu mkataba baina ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Kampuni ya Richmond Development Company (LLC) pamoja na mkataba wa ubinafsishwaji wa mgodi wa makaa ya mawe, Kiwira.

Kuhusu North Mara, baada ya kupokea taarifa ya Kamati ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, Serikali ilielekezwa kuchunguza haraka ili walioathirika na kemikali za sumu walipwe fidia.

Taarifa ya Loliondo haikufikishwa bungeni wakati TICTS na TRL hazikujadiliwa kutokana na Bunge kubaini kwamba hakukuwa na utekeleza
 
Kwa bunge la staili hii na uongozi wa staili hii, nchi hii umaskini kupungua au kuisha ni ndoto, matarajio ni umaskini kuongezeka na watanzania kuzidi kuumia. Mafisadi walioibia nchi hii wamefanikiwa kutengeneza mafia team kama iliyokuwepo huko Italy
 
Wanaharakati - What are you guys up to? Hamuwezi ku-root out corruption kwa kuongea na Waandishi wa Habari - Hiyo Njia imepitwa na Wakati - Kwa maana Hata Lyatonga ameanza kumsifia JMK kwa Njia hiyo!
 
Hakuna kitu hapo. Hivi wanawajua Watanzania kweli hao? Hiyo ni gimmick ya kupata financial support kutoka kwa wafadhili na wahisani wa nje ya nchi.
 
Wanaharakati - What are you guys up to? Hamuwezi ku-root out corruption kwa kuongea na Waandishi wa Habari - Hiyo Njia imepitwa na Wakati - Kwa maana Hata Lyatonga ameanza kumsifia JMK kwa Njia hiyo!

Lyatonga kaniacha hoi mie !!iweje leo??
 
Bunge letu hakika limenitia simanzi kwani ule moto ulioanza wa kashfa hizi ulizimika kama kibatari. Hapo kati lazima kuna kitu kimefanyika lakini WANANCHI tunayo turufu ya mwisho ya kuwarudisha Bungeni ama la. Kura yako iwe ndio mwamuzi. Tunahitaji Wabunge wenye msimamo na mwelekeo wa kutuondoa kwenye lindi la Umaskini.
 
Wanaharakati chini ya TGNP, wameonesha nia ya kutokubaliana na serikali juu ya maamuzi yalioyotolewa bungeni kuhusu kuwasafisha Mafisadi wa Richmond.

Wameamua kuandamana ili kuonyesha hisia zao za kutokubaliana na jinsi serikali na bunge wanavyoshindwa kutekeleza majukumu yao kwa umma. Nadhani ni wakati muafaka sasa kwa wanaJF kuwaandama na wenzetu hawa ili kuonyesha uzalendo wetu kuitetea nchi yetu dhidi ya watu wachache wanaojinufaisha na raslimari zetu.

Naomba tuungane nao sasa tusiishie kujadili tuuuuuu...hapa jamvini bila kuonyesha vitendo, tuungane kwa pamaoja kama tulivyoungana wakati wa mafuriko yaliyotokea Kilosa, maana hili nalo ni janga la kitaifa.

Hima sasa wanaJF tujitokeze kwa wingi kuandamana wa Wanaharakati kutetea nchi yetu......Saa ya Ukombozi imewadia.........!
 
Ndugu hili la kuandamana huku tukitumia majina ya BANDIA ni kujidanganya...... kipi kinakutisha mpaka uogope kutumia jina lako halisi na uitwe amba.nkya........??? Tukiachana na majina bandia na kuanza kutumia majina yetu HALISI hili linawezekana....... KWA NINI TUSIWE KAMA MSEMAKWELI na watu wake wa degree fake...........??? We should stop being more theoretical..

TUKIACHA WOGA WA MAJINA.....HADHARANI TUTAWEZA KUJITOKEZA. Maana kwa sasa tunatumia majina yetu kama vichaka vya kujificha ili tusijulikane tunaposti nini................
 
Ndugu hili la kuandamana huku tukitumia majina ya BANDIA ni kujidanganya...... kipi kinakutisha mpaka uogope kutumia jina lako halisi na uitwe amba.nkya........??? Tukiachana na majina bandia na kuanza kutumia majina yetu HALISI hili linawezekana....... KWA NINI TUSIWE KAMA MSEMAKWELI na watu wake wa degree fake...........??? We should stop being more theoretical.............. TUKIACHA WOGA WA MAJINA.....HADHARANI TUTAWEZA KUJITOKEZA. Maana kwa sasa tunatumia majina yetu kama vichaka vya kujificha ili tusijulikane tunaposti nini................
Mkuu, sitishwi kwa chochote, jina langu halisi ni Amba Nkya ni mwanaharakati, mpambanaji na mtetezi wa raslimali za taifa letu bila WOGA.
 
Serikali na bunge vinapoamua kukubaliana kumaliza mambo makubwa yenye maslahi kwa wananchi kimya kimya na kuwaacha wananchi katika kiza kinene ni hatari tupu kwa mustakali wa nchi hii. Kinachonishangaza zaidi hata wale waliokuwa mstari wa mbele nao wamefyata mkia. Lazima kuna siri kubwa sana kuhusu ufisadi uliofanyika na inawezekana wengi walinufaika na ufisadi huo. Hakika kama mtu sio msafi huwezi kumkemea mwenzako. Ngoja tu wanaharakati nao wajaribu kete yao. Mungu ibariki Tanzania
 
Mzee Sitta hapa kabanwa kisawasawa, kwamba wangesanua kwa data kwamba yeye ndo aliileta Richmond toka awali akiwa mkurugenzi wa TIC.
Naye kwa ushawishi wake Bungeni kainyongea hoja hiyo baharini, ili mradi ulaji uendelee.
 
Dawa yao ni mwaka huu kukutaa kuwa na bunge la Chama kimoja kama ilivyo sasa hivi na kuona kuwa inakuwa bora zaidi
 
WANAHARAKATI wa FemAct na vikundi vingine vya kiraia nchini wameeleza kutoridhishwa na kushtushwa na utendaji wa Bunge na Wabunge baada ya kushindwa kuchukua hatua madhubuti dhidi ya kashfa ya Richmond na nyingine.

Kutokana na hatua hiyo wananaharakati hao, wametangaza kuandaa maandamano nchi nzima kuonyesha kutoridhishwa na utendaji wa Bunge.
 
Wanaharakati - What are you guys up to? Hamuwezi ku-root out corruption kwa kuongea na Waandishi wa Habari - Hiyo Njia imepitwa na Wakati - Kwa maana Hata Lyatonga ameanza kumsifia JMK kwa Njia hiyo!

What do you reccomend instead!
 
Hakuna kitu hapo. Hivi wanawajua Watanzania kweli hao? Hiyo ni gimmick ya kupata financial support kutoka kwa wafadhili na wahisani wa nje ya nchi.

Pamoja na gimmick kama hiyo misaada ya wafadhili wa nje wanaitumia kwa njia hii basi ni bora mara mia kuliko bunge kutumia kodi ya mlalahoi na kupitisha mikataba fake mimi nawa support.
 
ile ripoti ya richmond, kiwira nk zipo mtaani, na hizi taasisi wanazo. mimi nafikiri badala ya kuongea tu na vyombo vya habari, wa mobilize resources na wajaribu kufungua mashtaka kwa wahusika ili sheria ichukue mkondo wake badala ya kuishia kulaumiana tu.

CCM wanajuana vizuri hivyo ni ngumu sana kunyongana. ni vyema wananchi tubadilike tupambane na mafisadi na tusitegemee kuwa mafisadi kwa mafisadi watachomana hizo ni ndoto za mchana. hivi hawa wanaharakati wanajua katika CCM, kamati kuu ni akina nani? na pia NEC ni akina nani? kama wangejua wasingeshangaa
 
Katika hali ya ajabu sana katika historia ya Taifa letu na hasa tuhuma za ufisadi CCM walishangaza sana ulimwengu kuwa kuwafanya Watanzania ni wagumu kuelewa hata kujua nini hasa cha kufanya katika sakata la Richomond. CCM wanadai kuwa wamefunga mijadala wa Richomond Je maswali yafuatayo ndio yanapaswa kuulizwa kama kweli wana nia ya dhati na Taifa letu Tanzania...

1. Je ni nani hasa muhusika wa Richmond??
2. Na kama yupo walijuaje amehusika au amefanya makosa hayo na hasara kwa taifa letu??
3. Je Kuna nia gani ya kuunda kamati teule na kupoteza pesa nyingi sana za walipa kodi wa Taifa letu Tanzania na badala ya kutumia kwenye huduma nyingine muhimu za Taifa letu Tanzania

4 Je wao ndio wanhukumu na kutoa adhabu badala ya mahakama zetu??

5. Je walijuaje kuwa wahusika wakuu ni wao na walifanya mambo yote kwa ajili ya kisiasa au nia ya dhati kwa taifa letu

6.Je Ndani ya CCM ni nani fisadi??Je walikuwa wanajua mapema kuwa ni wao ndio walifanya taifa letu kuishi kwa hali ya umaskini kama hivi leo.

7.Je ni kwanini wao waamue kipindi hiki kuwa wamefunga mjadala badala ya wananchi wa Tanzania

8. Je wali walikuwa wanajiita kuwa wapigananaji wa Ufisadi ndani ya CCM walikuwa wanapigana na wakina nani??

9.Je ni kwanini walipoteza muda mrefu na kutumia pesa nyingi kwa ajili ya mambo ya ajabu kama Richmond na madudu mengine na huku majibu ya maswali yote wanayo.

10. Je wote waliotumiwa kuwa ni mafisadi wamejuaje au kujisafisha kuwa ni wazuri baada ya kamati yao kukaa Dodoma

NB: Kwangu Mimi jambo kama haya moyoni kwangu haliwezi kutoka mpaka pale wale wote walihusika na madudu haya kuchukuliwa hatua za kisheria kama watu wengine Watanzania na pia kuona pesa zote walizopoteza au kuiba wanazirudisha serikalini na kufanya mambo mengine ya msingi kwa taifa letu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom