Mpandafarasi
Member
- Dec 7, 2008
- 57
- 11
Wanahabari wa vyombo mbali mbali mkoani Iringa leo jana walionyesha kuwa wao si watu wa kupelekwa pelekwa na chama cha mapinduzi (CCM) mkoa wa Iringa baada ya kugoma kulazwa katika gesti moja mji mafinga wilaya ya Mufindi ambayo CCM ilikuwa imewaandalia wanahabari hao zaidi ya watano ambao walikuwa katika msafara wa wanazi mkuu Mizengo Pinda baada ya kubaini kuwa gesti hiyo ni maarufu kwa biashara za shoti taimu a.k.a Danguro mjini Mafinga.
CCM ambayo ilikuwa imewaalika wanahabari hao ili kushiriki matembezi ya mshikamano pamoja na sehere za miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM sherehe zilizofanyika Ifwagi Mufindi kimkoa na kuhudhuriwa wa na waziri mkuu Mizengo Pinda ,walipata kuwaandalia wanahabari hao vyumba katika gesti hiyo iliyopo mjini Mafinga .
Ila baada ya waandishi kufika katika gesti hiyo na kuingia katika vyumba vyao ndipo walipobaini kuwa gesti hiyo si ya kawaida baada ya kupishana na wageni wengine mlangoni wakitoka kufanya mapenzi ya chapu chapu a.k.a shoti taimu katika vyumba hivyo.
Kilichofanya wanahabari hao kugoma kulazwa katika vyumba hivyo ni baada ya kuona mashuka na vyumba vyao vikiwa vimetapakaa uchafu wa kuime ambao unaonyesha kuwa vyumba hivyo kutumika kabla ya wao kuingia.
Kutokana na hali hiyo wanahabari hao walilazimika kuachana na vyumba hivyo vya CCM na kwenda kupanda hotel yao ambayo walihisi kuwa na hadhi na heshima tofauti na hiyo ya CCM. Wakati huo huo posho ya wanahabari hayo iliyoandaliwa kwa ajili yao inadaiwa kutafunwa na mmoja kati ya viongozi wakubwa wa CCM mkoa wa Iringa na kujitkuta wakielezwa kuwa itifaki imezingatiwa kwa wao kuambulia posho ya shilingi 15,000 kwa kila siku kwa muda wa siku bili.
Wakati viongozi wa CCM wilaya ya Mufindi wakimtuhumu mmoja kati ya viongozi wa juu wa CCM mkoa wa Iringa kuwa ametafuna posho za wanahabari hao ,mwenyewe ajitetea kuwa si kweli na kuwa itifaki imezingatiwa.
Source: Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima
CCM ambayo ilikuwa imewaalika wanahabari hao ili kushiriki matembezi ya mshikamano pamoja na sehere za miaka 35 ya kuzaliwa kwa CCM sherehe zilizofanyika Ifwagi Mufindi kimkoa na kuhudhuriwa wa na waziri mkuu Mizengo Pinda ,walipata kuwaandalia wanahabari hao vyumba katika gesti hiyo iliyopo mjini Mafinga .
Ila baada ya waandishi kufika katika gesti hiyo na kuingia katika vyumba vyao ndipo walipobaini kuwa gesti hiyo si ya kawaida baada ya kupishana na wageni wengine mlangoni wakitoka kufanya mapenzi ya chapu chapu a.k.a shoti taimu katika vyumba hivyo.
Kilichofanya wanahabari hao kugoma kulazwa katika vyumba hivyo ni baada ya kuona mashuka na vyumba vyao vikiwa vimetapakaa uchafu wa kuime ambao unaonyesha kuwa vyumba hivyo kutumika kabla ya wao kuingia.
Kutokana na hali hiyo wanahabari hao walilazimika kuachana na vyumba hivyo vya CCM na kwenda kupanda hotel yao ambayo walihisi kuwa na hadhi na heshima tofauti na hiyo ya CCM. Wakati huo huo posho ya wanahabari hayo iliyoandaliwa kwa ajili yao inadaiwa kutafunwa na mmoja kati ya viongozi wakubwa wa CCM mkoa wa Iringa na kujitkuta wakielezwa kuwa itifaki imezingatiwa kwa wao kuambulia posho ya shilingi 15,000 kwa kila siku kwa muda wa siku bili.
Wakati viongozi wa CCM wilaya ya Mufindi wakimtuhumu mmoja kati ya viongozi wa juu wa CCM mkoa wa Iringa kuwa ametafuna posho za wanahabari hao ,mwenyewe ajitetea kuwa si kweli na kuwa itifaki imezingatiwa.
Source: Francis Godwin Mzee Wa Matukio Daima