Wanahabari wa Clouds mna uwezo wa kuondoa upuuzi huu wa wanahabari wa Tanzania!

sifi leo

JF-Expert Member
Mar 30, 2012
5,014
8,364
Niandikapo uzi huu natambua yakuwa naweza pingwa sanaaa na ili kundi la wanahabar nchini Tanzania!

Awali ya mengi nianze kutoa pole kwa Ndgu yetu Rugemalira ambaye ni mkurugenzi wa vipindi hapo clouds tv.
Baada ya pole niwe wazi kuwa binafis nilipokea habar ya kumchangia ndgu Rugemalira matibabu yake kwa furaha na nilifanya hivyo kupitia no ya simu iliyotangazwa na mdgo wake Ruge!

Bila shaka mchango wangu utakuw umefika na utasaidia kidgo!

Niende kweny hoja! Ndgu zangu Tasnia ya habar nchini Tanzania imekuwa Tasnia ambayo uonekana kama Tasnia ya hovyo hasa kwa sababu mbalimbali kwanza ikiwemo ya wanahabar wenyewe kuishi maisha magumu ambayo wao hawawezagi kujisemea kwa kutaka haki zao!
Ni nchini Tanzania ambapo unakuta mwanahabar analipoti watumishi wa kiwanda fulani kuto kulipa mshahara kwa miezi mitatu ili hali yeye mwanahabar hajalipwa mwaka au zaid ya mwaka lakini hajisemei.

Niseme ili kwangu lilikuwa moja ya jambo lilironifanya nichukie kufanya kazi ya uandishi wa habar ambayo ni taaluma yangu!

Nakumbuka, haipiti miez miwili bila kukutana na andiko la wanahabar waliopo kweny media ya star tv wakilalama kuwa hawalipwi ila anaewasemea ni mtu mwingime kbsa na si wao!

Juzjuzi Rais wa Tanzania alikwenda kweny ofisi za kituo cha uhuru media chombo kinachomilikiwa na chama cha mapinduzi ccm!

Wanahabar ambao walikuwa wafanyakazi wa chombo kile walimwambia mh Raisi hali ngumu ya maisha waliyokuwa wakioshi wao kama waandishi wa habar wa chama ambacho yeye ndo Rais.

Jambo ili ili lilimsikitisha Rais, na aliwauliza kwa nini hawandiki habar zinazo wahusu?

Lakini sambamba na ilo, miaka kadhaa iliyopita mkurugenz wa vipindi kupitia Tv Clouds ndgi ruge mutahaba, kupitia kipindi cha 360 aliamasisha watangazaji mbalimbal wa kituo hicho kuendesha kampeni ya kupata pesa za kufanyia operation watt walio kuwa wakisumbuliwa na ugonjwa wa moyo niseme tu kampeni hiyo ilifanikiwa sanaa!

Sasa swali linakuja kwa nini clouds haikuendesha kampeni kama ile watu tukamchangia ruge hata kama familia haitaki ruge ni wa taifa sio familia

Naomba kuwasilisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wema usizidi kipimo

Nenda kamchangie yule muhitaji ambae hana watu nyuma yake kama Ruge.

Hana ndugu , hana chochote na hakuna anayemjua huyo ndio anayehitaji msaada.
 
Back
Top Bottom