Wanahabari Tanzania unganeni kwa Maombi / Dua Kabambe kwani Israeli hana Masihara kabisa!

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,544
108,865
Huyu Israeli alianza Kutuliza pale njia panda ya Coca Cola ambapo aliondoka na Wawili kisha akatusahaulisha kidogo akaja tena kuondoka na mwingine pande za Mikocheni Industrial area ambapo alituliza tena kutokana na Umuhimu wa huyo aliyemchukua na tukadhani kuwa ametusamehe kumbe alikuwa anatulia Timing tu na ni jana tu Israeli kaendelea kufanya yake na Safari hii ili kuonyesha kuwa ana Hasira ameondoka na Watano wa pande za Tabata Relini na tupo Majonzini tu.

Wanahabari Maombi Makali na ya haraka yanahitajika kwenu kwani sasa hatujui Kituo chake kinachofuata ni kipi kwani inavyoonyesha ni kwamba huwa harudi nyuma na wala harudii kule alikopita bali huwa anaenda tu mbele sasa hatujui baada ya Kuanza na Coca Cola Media kisha akaenda Mikocheni Media na jana Tabata Media Kituo chake Kinachofuata ni kipi / wapi.

Ewe Mwenyezi Mungu tusamehe sana kama labda tumekukwaza kwa lolote na tunakuomba huyu Israeli umuamuru sasa ahamie na ajikite zaidi kwa wale Watekaji wa Watanzania Usiku na Mchana, Waonevu wa Watanzania, Wauwaji wa Watu wasiokusudiwa nchini Tanzania na bila Kuwasahau wale Wanafiki wote popote pale walipo.

R.I.P Wanahabari wote
 
Back
Top Bottom