Kero ya machinga huko barabarani hapati rais peke yake, kero ya machinga hapati waziri mkuu peke yake, kero ya machinga hapati RC, DC au mkurugenzi peke yake!
Kero hii ya machinga wanaipata wanainchi wengi wastaarabu wanaozingatia kanuni na sheria za inchi.
Kero ya machinga tunaipata sisi watumiaji wa barabara, kero ya machinga anaipata mwenye duka anaelipa kodi ya serikali, kero ya machinga anaipata TARURA na TANROADS, TANESCO. Kero ya machinga anaipata kila Mtanzania aliyestaarabika!
Bahati mbaya watanzanja wastaarabu huwa hawana msemaji lakini hili ni kundi kubwa sana kuliko wenye kelele!
Zoezi la kuwapanga machinga limefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 70%! Hiyo peke yake siyo kazi ndogo!
Viongozi na wakurugenzi wamefanya kazi kubwa sana inayohitaji kuungwa mkono na wadau wote wa maendeleo hususani wanasiasa na waandishi wa habari.
Bahati mbaya sana kwasababu ya sifa za kijinga baadhi ya wanasiasa wa makundi ya vyama mmeanza kujitokeza KULAANI ZOEZI BORA kabisa la kuwapanga machinga.
Nasema ni UJINGA kwasababu nyie wapingaji mnajiona kinanani hasa hadi kila mara mtangaze LAANA za kipuzi namna Hiyo?
Hivi kweli hamuoni kulikuwa na tatizo la machinga holela? Hivi kweli nyie hamuoni machinga walivyokuwa wanabana njia hadi kupelekea wapita njia kugongwa? Hivi ni kweli hamuoni machinga walivyowazibia biashara wenye maduka, hivi hamkuona uchafu wa machinga huko mitaroni?
Hivi hamuoni machinga na mantilie walivyokuwa wakiuza na kupikia chini ya transfoma za umeme? Hivi hamuoni machinga walivyokuwa wamejaza mabanda uchwara mbele za nyumba ya watu? n.k
Hivi yote hayo hamuyaoni kuwa ni kero hadi mthubutu kutangaza LAANA kwa viongozi wetu waliojitolea kusafisha mji?
HATA NG'OMBE unamtegemea akupe maziwa lakini akivamia shamba la mazao huwa ni lazima afukuzwe kwanza ndipo umtaftie MARISHO mengine.
Machinga ni ng'ombe waliovamia shamba, ni kweli tunawapenda wanatupa maziwa, lakini lazima tuwaondoe shambani kwanza!
Mvamizi habembelezwi lakini viongozi wametumia busara kubwa ya kuwabembeleza watoke. Zoezi ni kubwa hivyo vidosari vidogo ni kawaida lakini chanzo cha dosari ni wao machinga kutotii maagizo mapema.
Wanahabari na wanasiasa kama hamuwezi kuunga mkono zoezi hili basi kaeni kimya kama wanaharakati walivyokaa kimya! Lina faida kwetu sote Tuliostaarabika.
USIMUONEE HAYA MTU ALIYEKULA KWA KUBUGIA ANAPOANZA KUHARISHA.
Machinga walibugia sasa wasilaumu kuharisha.
Bahati nzuri hata Rais ni kundi la wastaarabu. Hana mda wa kusikiliza chokochoko za kutafta sifa za kijinga.
Kama mna ushauri au kupinga pelekeni barua kwa viongozi mtoe maoni lakini siyo kupinga na kulaani kwenye vyombo vya habari.
Kero hii ya machinga wanaipata wanainchi wengi wastaarabu wanaozingatia kanuni na sheria za inchi.
Kero ya machinga tunaipata sisi watumiaji wa barabara, kero ya machinga anaipata mwenye duka anaelipa kodi ya serikali, kero ya machinga anaipata TARURA na TANROADS, TANESCO. Kero ya machinga anaipata kila Mtanzania aliyestaarabika!
Bahati mbaya watanzanja wastaarabu huwa hawana msemaji lakini hili ni kundi kubwa sana kuliko wenye kelele!
Zoezi la kuwapanga machinga limefanikiwa kwa zaidi ya asilimia 70%! Hiyo peke yake siyo kazi ndogo!
Viongozi na wakurugenzi wamefanya kazi kubwa sana inayohitaji kuungwa mkono na wadau wote wa maendeleo hususani wanasiasa na waandishi wa habari.
Bahati mbaya sana kwasababu ya sifa za kijinga baadhi ya wanasiasa wa makundi ya vyama mmeanza kujitokeza KULAANI ZOEZI BORA kabisa la kuwapanga machinga.
Nasema ni UJINGA kwasababu nyie wapingaji mnajiona kinanani hasa hadi kila mara mtangaze LAANA za kipuzi namna Hiyo?
Hivi kweli hamuoni kulikuwa na tatizo la machinga holela? Hivi kweli nyie hamuoni machinga walivyokuwa wanabana njia hadi kupelekea wapita njia kugongwa? Hivi ni kweli hamuoni machinga walivyowazibia biashara wenye maduka, hivi hamkuona uchafu wa machinga huko mitaroni?
Hivi hamuoni machinga na mantilie walivyokuwa wakiuza na kupikia chini ya transfoma za umeme? Hivi hamuoni machinga walivyokuwa wamejaza mabanda uchwara mbele za nyumba ya watu? n.k
Hivi yote hayo hamuyaoni kuwa ni kero hadi mthubutu kutangaza LAANA kwa viongozi wetu waliojitolea kusafisha mji?
HATA NG'OMBE unamtegemea akupe maziwa lakini akivamia shamba la mazao huwa ni lazima afukuzwe kwanza ndipo umtaftie MARISHO mengine.
Machinga ni ng'ombe waliovamia shamba, ni kweli tunawapenda wanatupa maziwa, lakini lazima tuwaondoe shambani kwanza!
Mvamizi habembelezwi lakini viongozi wametumia busara kubwa ya kuwabembeleza watoke. Zoezi ni kubwa hivyo vidosari vidogo ni kawaida lakini chanzo cha dosari ni wao machinga kutotii maagizo mapema.
Wanahabari na wanasiasa kama hamuwezi kuunga mkono zoezi hili basi kaeni kimya kama wanaharakati walivyokaa kimya! Lina faida kwetu sote Tuliostaarabika.
USIMUONEE HAYA MTU ALIYEKULA KWA KUBUGIA ANAPOANZA KUHARISHA.
Machinga walibugia sasa wasilaumu kuharisha.
Bahati nzuri hata Rais ni kundi la wastaarabu. Hana mda wa kusikiliza chokochoko za kutafta sifa za kijinga.
Kama mna ushauri au kupinga pelekeni barua kwa viongozi mtoe maoni lakini siyo kupinga na kulaani kwenye vyombo vya habari.