Wanahabari acheni kuwa mahakimu wa ufisadi-KKKT

Kite Munganga

Platinum Member
Nov 19, 2006
1,773
952
Askofu: Wanahabari acheni kuwa mahakimu wa ufisadi



Na Mwandishi Maalumu, Tanga

VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kutokuwa mahakama au mahakimu katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

Rai hiyo ilitolewa juzi mjini hapa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Stephen Munga.

Askofu Munga pia aliipongeza Serikali kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi kwa mujibu wa sheria na utawala wa sheria, badala ya kuongozwa na hisia na shinikizo la vyombo vya habari.

Kiongozi huyo wa KKKT alisema hayo wakati akimkaribisha Rais Jakaya Kikwete kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali teule ya wilaya mpya ya Kilindi, katika siku ya kwanza ya ziara ya siku tisa ya Rais mkoani Tanga.

“Naipongeza Serikali yako, kwa kuiendesha nchi kwa mujibu wa Utawala wa Sheria na hasa katika vita dhidi ya ufisadi. Endeleeni hivyo hivyo nasi tutaendelea kuwaungeni mkono.

“Jambo moja msifanye; msiviruhusu vyombo vya habari kuwa mahakimu katika suala hili,” alisema bila kufafanua.

Kuhusu ujenzi wa hospitali hiyo, Dk Munga alisema wazo la kujenga hospitali hiyo lilibuniwa mwaka 2003 lakini ujenzi ukaanza Januari mwaka huu kwa ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).

Dkt. Munga alisema chini ya ushirikiano huo, KKKT itajenga hospitali hiyo na Serikali itaajiri na kulipa wafanyakazi na wataalamu wa hospitali hiyo iliyopangwa kuanza kutoa huduma Februari mwakani.

Hukumu ndio hiyo
 
Msanii mwingine huyu hana jipya. Sasa anampongeza Kikwete kwa kupambana na mafisadi kwa lipi alilolifanya linaonyesha anapambana na mafisadi? :confused:
Mafisadi wote bado wanapeta uraiani na utajiri wao walioupata kiharamu.
 
Askofu: Wanahabari acheni kuwa mahakimu wa ufisadi



Na Mwandishi Maalumu, Tanga

VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kutokuwa mahakama au mahakimu katika vita dhidi ya rushwa na ufisadi.

Rai hiyo ilitolewa juzi mjini hapa na Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Askofu Stephen Munga.

Askofu Munga pia aliipongeza Serikali kwa kuendesha vita dhidi ya ufisadi kwa mujibu wa sheria na utawala wa sheria, badala ya kuongozwa na hisia na shinikizo la vyombo vya habari.

Kiongozi huyo wa KKKT alisema hayo wakati akimkaribisha Rais Jakaya Kikwete kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa hospitali teule ya wilaya mpya ya Kilindi, katika siku ya kwanza ya ziara ya siku tisa ya Rais mkoani Tanga.

“Naipongeza Serikali yako, kwa kuiendesha nchi kwa mujibu wa Utawala wa Sheria na hasa katika vita dhidi ya ufisadi. Endeleeni hivyo hivyo nasi tutaendelea kuwaungeni mkono.

“Jambo moja msifanye; msiviruhusu vyombo vya habari kuwa mahakimu katika suala hili,” alisema bila kufafanua.

Kuhusu ujenzi wa hospitali hiyo, Dk Munga alisema wazo la kujenga hospitali hiyo lilibuniwa mwaka 2003 lakini ujenzi ukaanza Januari mwaka huu kwa ushirikiano kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).

Dkt. Munga alisema chini ya ushirikiano huo, KKKT itajenga hospitali hiyo na Serikali itaajiri na kulipa wafanyakazi na wataalamu wa hospitali hiyo iliyopangwa kuanza kutoa huduma Februari mwakani.

Hukumu ndio hiyo

Hawa ndiyo wale aliowasema Mzee Ruksa kuwa wamesoma lakini hawakuelimika. How sad......
 
Huyu naye Almeida nini? Inawezekana wasanii wa Almeida wameanza kuingia mpaka katika uongozi makanisani sasa.
 
Back
Top Bottom