Wanafunzi wenye UKIMWI Kibaha wawekewa Label!

Mwalimu mkuu achapwe viboko hamsini kwa siku kumi,yaani vitano kila siku asubuhi mbele ya wanafunzi wote.
 
maybe wazazi wameamua hivyo ili kuwakinga watoto wao na maambukizi mapya nikimaanisha kuwa kwakuwa mafataki ni weng na wana mbinu nyng wakashauliana na kuona wakiwekewa lebel hawatafuatiliwa.inawezekana bwana! wakawa ni wazma 2 ila ni danganya fataki!!
 
Mungi & MODs ningeomba hii post ibakie hapa ili ijadiliwe na wengi. Ni muhimu sana kwa watu wengi kuona huu unyama unaofanywa huko Kibaha.

Hii ni aibu kwa Taifa zima, na ni kinyume kabisa na haki za binadamu. Lakini linalonisikitisha zaidi ni majibu aliyotoa waziri wa afya kwamba hawezi kusemam chochote mpaka uchunguzi ufanyike! Hivi waziri hajui kwamba hili ni kosa? Na inakuje BBC wawe wa kwanza kujua hii habari ni sio vyombo vyetu vya habari hapa Tanzania?

Yote hii ni madhara ya ujinga na umaskini uliokidhiri nafikiri ni wakati muafaka elimu kwa ujumla wake kutolewa kwa wananchi wote akiwemo na mheshimiwa waziri wa afya asiyeweza kuongea chochote mpaka akariri Kama sio kudesa what a shame to our government and nation at large!
 
mimi sijaipenda hii hali,
hawa watoto malaika hawana kosa, wamezaliwa wakajikuta tayari ni wagonjwa.
inapofikia kuvalishwa lebo ni unyanyapaa wa hali ya juu.
 
Naona tunahukumu haraka bila kujiuliza lengo hasa la kuvishwa hiyo red ribbon.
Wengine tunatumia simu za 'nhu ha' huhatuwezi kudown load , mleta hoja tueleze hasa sababu za wanafunzi kuvishwa hizo alama.
 
Hii habari si ya kweli. BBC na media zingine za magharibi ni watu wa chumvi sana. Mashule yote ya Tanzania watoto ambao wana matatizo mbali mbali ya kiafya (moyo, kifafa, kuanguka, sukari, ukimwi na mengineyo yote) bila kujali ni ugonjwa gani wanatakiwa kuweka nembo nyekundu ambayo si hii ya ukimwi kwenye colar ya shati ili iwe rahisi kuwatambua.

Hii inasaidia kuwapa msaada pale inapohitajika au kuangalia adhabu za kuwapa, kuwapunguzia kazi na mambo mengine ambayo mtoto mwenye matatizo ya kiafya anatakiwa kufanyiwa.

Tusiamini kila kitu ambacho west wanaandika. Mfano CNN imeomba msamaha juzi baada ya kuandika kutangaza kuwa kenya kuna machafuko wakati si kweli. Habari yenyewe ilitakiwa kuwa Al Shabab wameshambulia kituo cha basi lakini si machafuko kama walivyotangaza.
 
Hili suala ni pana kuliko tunavyolichukulia na lina sura nyingi sana

1. Mzazi mwenye mtoto mgonjwa
Huyu yeye anataka mtoto wake aishi vyema, na asiweke afya yake hatarini. Angependa mwanawe apunguziwe kazi ngumu za kufanya huko shuleni kama kuchota maji, kufagia, na kulima. Angependa pia kuona mwanawe haambukizi watoto wengine bila ya kukusudia.

Masuali anayojiuliza ni pamoja na
a. Kwa nchi iliyojaa maradhi ya ngozi kama majipu, na vigae na mabati vilivyotupwa tupwa ovyo usalama wa watoto wengine ukoje wanapocheza pamoja?
b. Kwa kudhoofisha afya yake kwa kazi ngumu ama kazi zinazomuweka afya yake hatarini, anakuwa amemlinda mwanawe kiasi gani?

Hatua anazoweza kuamua kuchukua ni pamoja na kuwaambia walimu na wanafunzi kuhusu ugonjwa wa mwanawe


2. Mzazi mwenye mtoto asiye na ugonjwa
Anataka kumlinda mwanawe na maradhi yoyote ikiwezekana lakini pia anataka kumwacha mwanawe acheze na kuchangamka na watoto wenziwe wote huko shuleni.
Anajua mtoto wa Bi. Mboga anaesoma darasa moja na mwanawe kuwa ana VVU pia

Yanayompitikia kichwani ni pamoja na
a. Nimzuwie tu mwanangu kucheza na mtoto wa Bi.Mboga kwa sababu bado hajui namna ya kujikinga kuzuwia maambukizi ?
b. Niwaambie na jirani zangu, ili na wao wawalinde watoto wao?

Hatua anazoweza kuchukua ni kueneza habari za ugonjwa wa mtoto kwa kificho na mtoto huyo kukuta anatengwa shule na wenziwe bila ya yeye kujua sababu


3. Walimu wa wanafunzi
Wao wanataka kutoa elimu kwa wote na wakati huo huo kuwalinda wanafunzi wagonjwa ili maradhi yao yasiwazidie na pia wasiwaambukize waliokuwa wazima.
Wanajua pia kuwa katika shule ambazo uwiano wa walimu kwa wanafunzi ni 1 kwa 200, si rahisi walimu kuwepo na wanafunzi wakati wote. Jee inapotokea dharura kama ya mwanafunzi mgonjwa kuumia na kuchuruzika damu na wanafunzi wenziwe kumpa huduma ya kwanza itakuwaje?
Wanafunzi waliokuwa hawana maambukizi wakija shule na majipu na mapunye, wakacheza na wenye virusi bila ya wao kutambua na kuchukua hadhari itakuwaje?


* Nnachoweza kusema ni kuwa habari imeandikwa kwa kuegemea upande mmoja, kwa sababu haijatupa maelezo ya wazazi wa watoto hao wanasemaje? Pengine wao ni miongoni mwa waliopendekeza mpango huo
 
HUo ni uzushi wa kijinga kwani shule siku hizi zinapima wanafunzi ukimwi?Nakumbuka hata wakati nasoma hii system ilikuwepo kwa wagojwa bila kujari ni ugojwa gani anaoumwa mwanafunzi ili asifanye kazi pale shule ambazo zaweza zoofisha zaidi afya yake.
 
Mbona wale wanafunzi 100 mama Salma aliowachukua hapo ukweni akawapeleka pale Sauti mwanza hawana lebo?Au ni mkakati wa kuwamaliza wale madogo wa CDM pale Sauti?If they are doing that it is against humanity.
 
Kwa kweli VVU na UKIMWI, kwa pamoja vinaleta dilema sana!

Mtu mwenye VVU sio lazima kwamba tayari ana UKIMWI. Na wengine wana VVU lakini kwa sababu hawajapima (na hawalazimiki kupima) hawajui lolote na hivyo suala la kuzuia/kupunguza maambukizi linakuwa kitendawili kigumu sana. Unawawekea ribon waliopima na kujijua wana VVU, je wale wasiopima na wana VVU inakuwaje?

Maswali ni mengi lakini katika hili nadhani tunakosa maelezo ya hao wazazi, pengine yangesaidia kujibu baadhi ya maswali.
 
Hii si sawa! Tumesoma na watoto wenye allergies, asthma, disabilities mbalimbali! Kwani hao watoto wako wangapi hadi walimu wasiwajue? By the way, walimu wanapaswa kuwajua wanafunzi wote wanaohitaji special attention ili wawasaidie! Kama ni kwa ajili ya kuwatambua, ina maana wenye malaria na kuhara wanapewa label?
Isitoshe ukimwi sio ugonjwa jamani! Kwani mtoto mwenye hiv akichota maji atakuwaje? Mbona tuko na watu makazini na wanafanya kazi kama kawa na kusafiri pia? Na hao wazazi wanawafundisha watoto kujinyanyapaa!

Uko sahihi,,well sishangai,,wazee wenyewe wa Pwani! uelewa wao nao mdogo wengi shule teee! haf uvivu ndo asili ya watu wa pwani. Shule za siku hizi hazina kazi sana kama enzi zetu tunalima mashamba,tunasomba matofali,kuni,ambazo ndo kazi ngumu. so wanawakinga na kazi zipi leo hii? Nonsense!
 
Kweli ni suala tata ila halimaanishi halipaswi semwa,watoto wanajifunza kamchezo wakiwa shuleni..sasa watalindwaje hawa wenzao ambao hawana maambukizi?Mimi bado napenda pia na wao waathirika nao wajue wanalojukumu la kuwalinda wengine.Huku uswahili hata uzunguni waathirika hawana huruma kabisa. wanagombania wapenzi.Na vipimo si issue ya kuwenza fanya kwa urahisi kila mara au kila mahali kihivyo.Watoto wana curiosity, na wanajaribu vitu wanavyokatazwa ikiwepo na Ngono. Tuache ujinga tufikie mahali tujifunze heshimu waathirika ila wawe wazi kuwa wana VVU na kila mtu kati yetu aheshimu hilo.
Cha msingi tusiulize wamepataje wala kuwanyima haki zao.Mnatupa shida sana na hizi culture za kutosema kitu km kilivyo.mambo ya dawa ya mboga, kujisaidia, sehemu za siri wakati siku hizi zipo wazi, napata shida tafsiri albino, napata shida ,mwita kipofu,napata shida mwita kiziwi, au bubu, basi hii misamiati itolewe ktk vitabu vyetu.Soon hata haya maneno mbadala nayo yatakuwa matusi tutahamia kwa wengine.. watu wanaambukizwa na hawa waathirika...tena wengine ndio sijui wana hamu zaidi au nini basi wapo mabaa, makanisani, etc wakijifanya wanatafuta mmoja wa kutulia.
 
hiyo ni kweli kabisa.Hivi vyombo vya habari kama BBC waandishi wake wengine si kama akina Majura?Watuleze wanapata wapi hizo habari?
 
Uko sahihi,,well sishangai,,wazee wenyewe wa Pwani! uelewa wao nao mdogo wengi shule teee! haf uvivu ndo asili ya watu wa pwani. Shule za siku hizi hazina kazi sana kama enzi zetu tunalima mashamba,tunasomba matofali,kuni,ambazo ndo kazi ngumu. so wanawakinga na kazi zipi leo hii? Nonsense!

Unashangaza kuja kupinga watu kunyanyapaliwa lakini wewe umewanyanyapaa watu wa Pwani.

Wengine tunaendeshwa kwa morals za nchi za Magharibi, na hatuangalii kwa mazingira ya kwetu nini kinafaa.

Habari haijeleza kama watoto wenye hizo red ribbon wananyanyapaliwa na wenzao au la kilichokupa kudhani kuwa wananyanyaswa na wenzao ni nini?

Unataka kusema upo radhi mwanao apangiwe kazi za kumdhoofisha afya yake na hata kupelekea kifo kuliko kujuulikana kuwa ni mgonjwa lakini akaishi bila ya mfumko wa maambukizi?
 
What a misconception!! Huo ni upotoshaji.
Hii taratibu si kuhusu HIV. Ni utaratibu upo muda mrefu tangu tunakua wengine. Mi nakumbuka sie primary watu walikuwa wanawekewa label ili wasipewe adhabu ama shughuli ambazo kiafya wameshauriwa wasifanye na madaktari. And it was quite okay.

Mi kwa mfano,nlikua na allergy,yani nkinusa vumbi tu ujue ntaumwa hadi kulazwa.so nikawekewa label kwa hiari ya mzazi wangu na hivyo nkawa sifagii wala kudeki shule hata aje mke wa rais kututembelea.

Kwa hivyo huyo anayesema ni ukimwi anapotosha sababu usually ugonjwa hauwekwi hadharani na ni mwalimu husika tu anayeidhinisha ndo anajua,tena si kwa kuambiwa ugonjwa bali kwa note ya daktari inayoeleza hivyo.
Acha longolongo, wengi wa wanaowekewa ni HIV positive. Mwalimu Mkuu amekiri hilo wewe hutaki!
 
Back
Top Bottom